Kamaka
JF-Expert Member
- Jun 7, 2010
- 563
- 33
Nahisi katika watu watakaokwenda kuwa milionea ni huyu bwana kwanza amewarahasishia watu mpaka waende TANGA anajiwekea tu kaservic chake karibu na bunge ...
True pale itakuwa kwa miguu,Zero distance.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nahisi katika watu watakaokwenda kuwa milionea ni huyu bwana kwanza amewarahasishia watu mpaka waende TANGA anajiwekea tu kaservic chake karibu na bunge ...
uthibitisho....uthibitisho....uthibitisho!!! Nchi hii itakuja kuangamia katika kutaka uthibitisho -- kitu ambacho ccm wanaking'ang'ania sana pindi ukigunduliwa ufisadi wao. Mramba atakuwa mbunge tena kwa sababu hadi sasa hakuna uthibitisho wa ufisadi wake!!!! Chenge atakuwa mbunge tena kwa sababu hakuna uthibitisho wa ki-bongo, uko ule wa majuu tu ambao serikali ya ccm haiutaki.
Lakini uthibitisho mmoja ni kwamba bashe ni mtu wa rostam 100 percent -- alimpatia kazi pale habari corporation, na mshahara wake unajulikana, alimnunulia pikipiki za kampeni ambazo aliibiwa kutoka ofisi za habari corp.
Lakini kwa upande mwingine matokeo ya kyela na urambo east ni pigo kubwa sana kwa rostam kwa sababu ameshindwa vibaya sana kuwang'oa wawili hawa waliomng'oa swahiba wake mkuu el. Ilikuwa faraja kubwa kwangu, na bila shaka kwa wengine. Bado mtataka ushahidi kwamba mwakyembe na sitta hawakuwa maadui wa rostam walipangwa kuangamizwa?
mara vipi kwa wasira hawajatwangana huko kweli? Vipi hapo kilimanjaro kwa mama malecela? Na vipi huko kyela shwari? Tupeni taarifa wadau mlioko huko.
Majimarefu awa majimarefu Korogwe
Mganga wa tiba za jadi, Bw. Stephen Ngonyani maarufu kama Majimarefu ameibuka kidedea baada ya kuwashinda wenzake 16 kwenye kinyang'anyiro cha Jimbo la Korogwe Vijijini kwa kura 12,441.
.....Bw. Ngonyani ambaye kwenye kampeni zake hakuwaficha watu kuwa yeye yake ni darasa la saba, alimbwaga msomi na mchumi mwenye Shahada ya Uzamivu, Dkt. Edmund Mndolwa aliyepata kura 2, 286, huku akiwaacha midomo wazi baadhi ya watu.
Nadhani kugombea ubunge , mgombea anatakiwa awe na elimu walao ya kidato cha nne. Sasa huyu prof. amekiri kuwa na elimu ya darsa la saba. Anaweza kuondolewa na wenzake huko ktk vikao vya CC na NEC kwa kigezo hicho. Iwapo atapitishwa na ccm , CHADEMA itapeta, maana atawekewa pingamizi kwa kukosa kigezo cha elimu ya chini (minimum) kinachotambulika kisheria ili kugombea ubunge.
Na January Makamba ameshinda for 85&....Lau Masha ameshinda pia...hahaha C.C.M!....
...... yote tuyaonayo hapa duniani yalitoka kwa NENO!. Nai-boomark hii nyuzi nikiamini kabisa na kujipa wajibu wa kuifufua siku ya kutimia kwa uliyosema Mkuu.
Kwanza hongera zako kushinda udiwani, pili hongera kwa Bashe kumshinda mpiganaji Seleli hata kama ni kwa kutumia masalia/mabaki ya Kagoda.
Wapenzi wa Selelii wasiwe na shaka, hata kama Bashe angeshinda kwa asilimia 99% na Selelii asilimia 01%, bado CCM itampitisha Selelii na kumtosa Bashe, kuna secret agreement kwa wabunge makamanda waliahidiwa kupitishwa no matter what, nao ndio wakakubali kuitosa CCJ.
Hivyo kama wana CCM wa Nzega, wanawakilisha wakazi wote wa Nzega, na chaguo lao ni Bashe, basi atakayekwenda upinzani na awe Bashe, asimame na Selelii kwenye sanduku la kura, hivyo Jimbo la Nzega tuanze kulihesabu upinzani.
Kama na kuchekelea ushindi, kambi ya Bashe, chekeni sana, mkisubiria panga la NEC na mtalia sana, piga ua CCM haiwatemi makamanda wake, almanusura waimege ikatike vipande viwili, wakakubali kuinusuru CCM, sasa ni zamu ya CCM kuwanusuru.
Bashe ajiandae kwa safari, the only choice ni Chadema, tatizo langu kwake ni jee Chadema itawakubali hawa makuwadi wa RA?. Jee itafungua milango yake kuwakaribisha nyoka?.
Mwito wangu kwa Chadema, acha milango wazi kwa yoyote ajaye bila kujali alikuwa akimtumikia nani, concetration yao kwa sasa, iwe ni idadi ya viti vingi bungeni.