Rogie
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 7,581
- 6,675
Wakuu,
NECTA wametangaza matokeo tayari.
Kuyapata matokeo (kama yalivyotangazwa tarehe 18/02/2013), tembelea:
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 - (Hosted by JamiiForums)
QT Results 2012 - JamiiForums
NECTA wametangaza matokeo tayari.
Kuyapata matokeo (kama yalivyotangazwa tarehe 18/02/2013), tembelea:
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 - (Hosted by JamiiForums)
QT Results 2012 - JamiiForums
60% ya wanafunzi wafeli mtihani
Jumatatu, Februari 18, 2013
MATOKEO ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yametangazwa. Watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, huku wanafunzi 23,520 tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wamepata daraja la nne.
Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema watahiniwa walikuwa 456,137, wa shule wakiwa 397,136 huku wa kujitegemea wakiwa 68,806.
Kwa mujibu wa matokeo hayo, watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, wavulana wakiwa 1,073 na wasichana 568, daraja la pili ni 6,453, wavulana wakiwa 4,456 na wasichana 1,997.
"Matokeo ya mwaka huu yamekuwa mabaya sana, Serikali tunasikitika kutokana na hali hii lakini tuna mipango mbalimbali ya kuhakikisha tunaweza kutatua hili tatizo," alisema Dk Kawambwa.