..pamoja na hayo nakuhakikishia hakuna njia ya AMANI na KIUNGWANA ya kupinga uchaguzi na kutetea kuwepo kwa Tume huru zaidi ya hiki wanachokifanya Chadema.
Wakuu,
Hatua ya viongozi wa Chadema kutohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Mhe. Mizengo Pinda pale Ikulu ndogo ya Chamwino mnaionaje? Miye ninaiunga mkono kwa asilimia 120. Mtu mzima lazima uwe "Standar" na "Consistent" na mambo yako.
Wakuu,
Hatua ya viongozi wa Chadema kutohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Mhe. Mizengo Pinda pale Ikulu ndogo ya Chamwino mnaionaje? Miye ninaiunga mkono kwa asilimia 120. Mtu mzima lazima uwe "Standar" na "Consistent" na mambo yako.
kuna mtu humu ndani anamtambua jk kama mkuu wa nchi?
Nitawasaport by 1000% wakitoka nje ya Bunge kikwete atakapoanza kulihutubia bunge.
Bwn Ruta ni sawa kabisa wanachokifanya CHADEMA. Ni bora jumuiya ya kimataifa wakajua kuwa kuna chama kinapinga jambo baya lililo fanywa na tume ya uchaguzi NEC katika uchaguzi uliopita. Kuwachagulia Watanzania Raisi tofauti na kura halisi za kumchagua Raisi waliye mpenda.
Watu wengine wanakataa kujua au hawataki kujua kinacho endelea tusonge mbele tuu. Aluta Continua.
Happy are those who dream dreams and are ready to pay the price to make them come true. Leon J. Suenes
Hii inanikumbusha mambo niliyoyaona kwa jirani yangu mmoja ambaye alifiwa na mme wake. Baada ya muda wa miaka kama miwili hivi mama yule akampata mwanaume mwingine ambaye kiumri alikuwa karibu sawa na wanae aliozaa na marehemu mumewe. Vijana wake wakaonyesha dhahiri kutokubaliana na mama yao juu ya "baba yao" huyo wa kambo. Mama hakuwasikiliza hata kidogo. Ghafla siku hizi nawaona vijana wale ni marafiki wakubwa na huyo baba yao wa kambo. Amewasaidia mambo mengi tu.
sipati picha atakapoanza kuongea tu! wakatoka nje, hivi hawezi kuamuru wakamatwe na kuwekwa ndani?
kwa hiyo unataka kusema sisi chadema tumkubali huyu baba wa kambo (jk)?
Hayo ni mabaka ya nini? na yametokana nini, kama unafahamu.Jamani siyo vizuri kusema lakini kwa maoni yangu binafsi nimeona viongzi wengi waalikwa wana mabaka usoni.....................sijui hii nayo ni sifa ya kupata ulaji kwenye hii serikali ya CCM.......................ila sitayataja majina yao..............................mnisamahe tu kwa hilo......................hizi afya zao zaonekana zina mushkeli mkubwa...........................wenzangu mnaonaje kwenye hilo?
ITV wamethibitisha ya kuwa Wabunge na uongozi wote wa juu wa Chadema haujaja kwenye hafla hii kwa hiyo hii sasa siyo tetesi tena ila ni ukweli mtupu...kuwa Chadema wamesusa hafla hii kabisa...................