Maayo
JF-Expert Member
- Jul 21, 2011
- 317
- 48
Habari wana jf doctor. Mdogo wangu wa kike mwenye miaka 19 ana tatizo la matiti kusinyaa na kulegea kana kwamba alishawahi kunyonyesa. Nimejaribu kumuuliza amesema tangu akiwa primary waliwahi kumuhisi ni mjamzito ikabidi wapelekwe kuchekiwa nurse alipo angalia matiti yake alisema ametoa mimba ilhali kipindi hicho hakuwahi hata kufanya mapenzi. Hata alipokutana na mpenzi wake wa kwanza alimshangaa inakuwaje yeye ni bikra wakat matiti yake yanaonyesha kama amewahi kunyonyesha. Hii inatokeaje ndugu zangu?