Avanti
JF-Expert Member
- Aug 24, 2010
- 1,209
- 239
Picha gazeti la Mwananchi leo na hata taarifa nyingi ndani ya JF na kwingineko zinaonesha Muhimbili sasa wanamtibu Ulimboka tu. Machine inayosaidia kuangalia kila kitu kuhusu afya ya binadamu imefungwa kwake ikianzia kupima mapigo ya moyo na kadhalika na viungo vyote vya mwili. Ni adimu sana raia mwingine asiye Dokta, hata awe ameumia kiasi gani, iwe kwa ajali ama vinginevyo kufungiwa machine kama hiyo. Ilinichukua siku 6 kwa mama yangu kuchunguzwa tatizo lake la kuumia nyonga baada ya kudondoka, tulipomleta toka mkoani walipoturefer Muhimbili. Kwa kusaidiwa na wanakijiji wenzangu tulikodi gari ili kuweza kuwahi matibabu Muhimbili, lakini baada ya kufika tulisubirishwa siku 6 zingine na mpaka anapata huduma tulishakata tamaa tukijua atatuacha hasa tokana na uchovu ambao tayari alikuwa nao, kumbuka hapo hata mgomo haukuwepo. Pamoja na kuwa yawezekana madaktari wanadai haki lakini ubinadamu nafikiri wanadhani upo kwa wao wenyewe tu, wanatibiana bila masharti na pia wanatumia vifaa vya Serikali hiyo hiyo wanayoilalamikia. To hell you doctors and your cockroach government all the same!