Kuna siku nilihudhuria harusi moja hapo Mayfair Plaza. Sheikh mfungisha ndoa akapewa nafasi atoe mawaidha japo kwa ufupi kwa wanandoa wale.
Yule sheikh akatoa mfano mmoja wa jinsi ambavyo ndoa zote zina matatizo na ni muhimu kuvumiliana. Akasema:-
Kuna siku alikuwa msikitini akisikiliza mawaidha hayohayo ya mambo ya ndoa. Mtoa mawaidha akauliza wanaume. Wangapi humu ndani wamewahi kupigwa na wake zao? Kama wapo waje wasimame juu wasogee mbele. Kwa muda wengi wakasita, lakini baada ya muda mfupi wote wakasimama wakaenda mbele . Akabaki bwana mmoja ameketi. Wale wanaume kumwona jama kaketi, wakamsifu sana kwamba yeye kapata mke mwema na mtoa mawaidha akasema hebu mwenzetu atujulishe nini siri ya mafanikio yake.
Yule bwana kwanza akasikitika sana akasema jamani mimi sina unafuu wowote kwa huyo mke wangu, ni kwamba kipigo alichonipa ndio kinanifanya hata kusimama siwezi !!!
Tuliishia kucheka, na hotuba ikaishia hapo
Yule sheikh akatoa mfano mmoja wa jinsi ambavyo ndoa zote zina matatizo na ni muhimu kuvumiliana. Akasema:-
Kuna siku alikuwa msikitini akisikiliza mawaidha hayohayo ya mambo ya ndoa. Mtoa mawaidha akauliza wanaume. Wangapi humu ndani wamewahi kupigwa na wake zao? Kama wapo waje wasimame juu wasogee mbele. Kwa muda wengi wakasita, lakini baada ya muda mfupi wote wakasimama wakaenda mbele . Akabaki bwana mmoja ameketi. Wale wanaume kumwona jama kaketi, wakamsifu sana kwamba yeye kapata mke mwema na mtoa mawaidha akasema hebu mwenzetu atujulishe nini siri ya mafanikio yake.
Yule bwana kwanza akasikitika sana akasema jamani mimi sina unafuu wowote kwa huyo mke wangu, ni kwamba kipigo alichonipa ndio kinanifanya hata kusimama siwezi !!!
Tuliishia kucheka, na hotuba ikaishia hapo