Matembo na al shaababu nani zaid

MASAMBI

Member
Feb 4, 2011
19
3
Binafsi nashindwa kuelewa utendaji wa jeshi polisi hasa kanda maalumu ya dsm.hivi hawajui kuwa kuna kikundi cha wahuni maarufu kama MATEMBO hapa ubungo mataa au ndio kulindana.Hiki ni kikundi chenye maskani yao nyuma ya msikiti wa ubungo maji na wametawala hadi stend ya mwenge.Hujipatia fedha kiharamu kwa kuwatoza ushuru wamajinga wote wa ubungo kuanzia riverside bar hadi sted ya kuelekea mwenge na maeneo yote yanayozunguka eneo hili.Viongozi wa kundi wanajulikana na baadhi yao walikuwa vijana wa kazi (Majambaz) ktk maeneo tofauti Tanzania hasa kanda ya kazkazin na sasa ni watu matajiri kwa shughuli hii.Matembo wana vyanzo vingne vya mapato kwa kujukua ushuru wa daladala na bodaboda zote zinazofanya kazi maeneo ya ubungo.Kuna kipindi polisi walifanya kuwasshtukiza ili wakamatwe wakaambulia patupu (inaonekana kuna network na jeshi la polisi).Matembo ndo husimamia vitendo vyote vya wahuni wa ubungo kuanzia uuzaji wa simu feki,uporaji,upigaji debe,uuzaji wa madawa ya kulevya na ubakaji.Jeshi la polisi hawana ubavu na watu hawa na wanaishi kujingamba kuishika serikali.Bora Al shaababu kuliko hawa jamaa ni hatari na wanatumika kwa shughuli za utekaji nyara,uuaji na wizi ktk sehemumbalimbali za nchi yetu.Naendelea na uchunguzi nitawaletea majina ya viongozi wao na sehemu wanazoishi.Kwa sasa matembo ndo walioshikilia kitengo cha ulinzi shirikishi hapa ubungo na huchukua malipo kwa wakazi wote wa ubungo kuzunguka terminal.kazi ipo watanzania kwa kweli naona bora ukolon kuliko nchi kuendeshwa kiimla.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom