rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,412
tunajitahidi sana kuwasaidia Chadema wakamate dola,tunahatarisha maisha yetu na biashara zetu na familiya zetu ili waingie madarakani,lakini mategemeo yetu makubwa ni kuona mabadiliko mara watakapo chukua dola,itasikitisha sana kama Chadema watakuwa na mwelekeo wa kujineemesha kama watani zetu ccm,nasema hivyo kwa sababu tumegundua watanzania tuna mapungufu makubwa katika swala zima la uaminifu,imefika wakati tuseme ukweli tu,Chadema msituangushe kwani mkifanya hivyo mtakuwa mmeharibu kila nafsi inayotarajia mabadiliko,tunajuanyie ni binadam lakini inabidi mjitoe kwa moyo wenu wote kunusuru taifa letu,naandika haya nikiwa na woga na mashaka moyoni mwangu, iwapo mabadiliko yanayoitajika ndani ya taifa letu hayatatokea itakuwa ni tatizo kubwa,watanzania ni watu wa kuvunjika moyo haraka na hawana subira,kila la kheri chadema tupo nyuma yenu kuwaweka madarakani mlete mabadiliko