Matatizo yanayowakabili watanzania yawaliza machozi wajapani

BONGOLALA

JF-Expert Member
Sep 14, 2009
16,507
11,883
Wajapani wanaojitolea wamebubujikwa na machozi baada ya kujionea hali halisi ktk shule walizokua wakifundisha.waliyasema hayo ktk ofisi ya rais menejimenti ya utumishi wa umma.Wamesikitishwa sana na serikali kutothamini watoto katika kuwapa elimu,afya na maji.Wanashangaa shule ipo karibu na ziwa lakini hakuna huduma ya maji kijijini.walimu wengi hawana vyeti wala ujuzi wa kufundisha.source gazeti habari leo!
 
Inasikitisha sana. Mgeni machozi yanamtoka lakini mwenyeji anafurahia hali hiyo.

Poleni sana waaTz
 
jaman hakuna nchi ambayo duniani imefanikiwa bila kuwekeza kwa watoto. watoto ndo msingi wa taifa lolote lile duniani.. hawa wenzetu walilia kwa sababu wanajua umuhimu wa mtoto katika taifa lolote, mfano kule japan wana program nzuri sana juu ya ukuaji na malezi ya mtoto, Naamini ni wakati muafaka kwa serikali yetu kuwekeza kwa watoto ili baadaye tuje tuwe na taifa lenye watu wanaothamini nchi yao. Serikali ijitahidi kuwekeza katika Elimu ya awali kwa kuhakikisha kwamba wanatoa huduma zote ambazo ni muhimu ambazo zinahamasisha Holistic Development kwa watoto wetu. Kuna vijana wanachukua Degree za Early Childhood Education katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Dar es salaam, kwa kweli kama serikali itashindwa kuwatumia hawa vijana vizuri wataleta mapinduzi katika nchi hii, mimi naamini kwamba katika nchi yetu ya Tanzania kuna wataalamu wachache sana wa masuala ya watoto. hii ni fursa ya pekee kwa serikali kuwaonesha wanachi kwamba imedhamiria kuleta mabadiliko ya malezi na ukuaji wa mtoto kwa ujumla.
 
Watu kama Mizengwe Pinda ndo wanasababisha hali hii, badala ya zile posho za waeshimiwa zifanye kazi ya kuweka miundo mbinu ya maji mashuleni yeye anatetea ujinga kwa point za kipumbavu hata mwehu hawezi kuziafiki1
 
Back
Top Bottom