Matatizo ya Meno

kholo

JF-Expert Member
Jul 1, 2011
413
75
Ndugu wana jf, habarini za kutwa nzima! kwanza kabisa naomba niwapongeze kwa majukumu ya uelimishaji humu jamvini. ama baada ya salam naomba msaada wako wewe mdau wa jamvi hili namna n'takavyoweza kutatua hili tatizo;
Tatizo kuu nililonalo in "MENO", yanatoboka pia yanauma hivyo naomba mnisaidie nifanyaje ili kurecover maana mengine
yamechimbika kiasi kwamba hata kung'oa haiwezekani, ama unamfaham daktari au hospitali ye yote spesho kwa magonjwa ya meno basi naomba unifahamishe. Natanguliza shukrani wakuu wangu
 
Dawa ya Meni ni Kung'oa Muone Dr. Akim 0754-262280

Ana huduma nzuri sana yupo Msimbazi Street karibu na kituo cha mabasi yaendayo Muhimbili niling'oa na sikusikia maumivu na alinipa dawa kila baada ya masaa sita nameza kwa siku mbili zote sikusikia hata tone la maumivu... yaani maumivu niliyopata ni yake ya sindano ya ganzi tu....

Meno yote yanangoka hata kiwe kipande... ila nilisikia Meno ya Juu yakitolewa vibaya unaweza poteza hata maisha....
 
Kuna tunda linaitwa ndulele wengine wanaita ntulantu ukilipata hili yachukue kama kumi hv yaliyoiva(njano) then yachemshe upate supu yake kisha changanya na matone matano ya mafuta ya taa baada ya hapo safisha meno yako vizuru uhakikishe hakuna mabaki ya chakula kwenye matobo then sukutua hyo dawa, fanya asubuh na jioni na uhakikishe meno yako hayashindi na mabaki ya chakula ndani ya cku tatu utaona mabadiliko makubwa sana hata mimi nimesumbuliwa sana na meno ya kutoboka ila baada ya kutumia hyo dawa nimepona kabisa huwez amini
 
Ndugu wana jf, habarini za kutwa nzima! kwanza kabisa naomba niwapongeze kwa majukumu ya uelimishaji humu jamvini. ama baada ya salam naomba msaada wako wewe mdau wa jamvi hili namna n'takavyoweza kutatua hili tatizo;
Tatizo kuu nililonalo in "MENO", yanatoboka pia yanauma hivyo naomba mnisaidie nifanyaje ili kurecover maana mengine
yamechimbika kiasi kwamba hata kung'oa haiwezekani, ama unamfaham daktari au hospitali ye yote spesho kwa magonjwa ya meno basi naomba unifahamishe. Natanguliza shukrani wakuu wangu

Kuna dawa nzuri sana ipo pale Natural Therapy Center(adjacent na Hindu mandal) inaitwa RANOS.Ni Nzuri sana kwa meno na mie nishawahi kuitumia na sisumbuliwi na meno.Nakushauri ijaribu..
 
Meno kutoboka. Au kupata ganzi,ukipigwa upepo meno yanauma, maji ya baridi yanauma,maji ya moto yanauma. Kitaalamu ni tatizo linalosababishwa na kuondoka kwa tabaka la juu la meno. Inayosababishwa na sumu iliyopo ktk dawa nyingine zilizo na floride. Hii inaweza mtokea mtu yoyote anayetumia dawa za mswaki zenye floride. Nilimshauri mama angu mzazi aliyekuwa na tatizo hili pamoja na mdogo wangu. Wameacha kbs kungoa meno. Nilipatia absorbent c na aloe brightooth gel. Ka unahitaji ushauri call me 0713297066. Sina mda wa kuandika hapa sana.
 
Nilipatia absorbent c na aloe brightooth gel. Ka unahitaji ushauri call me 0713297066. Sina mda wa kuandika hapa sana.

Nilitumia Aloe bright tooth gel na meno yangu yalikuwa meusi kama ninaye vuta fegi... Kama mwezi umepita natumia Sensodyne..yaani yanang'aa kama fedha!! Ila nakubali kuwa aloe b toothgel ni kiboko ya meno mabovu na ganzi ...Tatizo ni hilo tu la meno kubadilika rangi
 
Dawa ya Meni ni Kung'oa Muone Dr. Akim 0754-262280

Ana huduma nzuri sana yupo Msimbazi Street karibu na kituo cha mabasi yaendayo Muhimbili niling'oa na sikusikia maumivu na alinipa dawa kila baada ya masaa sita nameza kwa siku mbili zote sikusikia hata tone la maumivu... yaani maumivu niliyopata ni yake ya sindano ya ganzi tu....

Meno yote yanangoka hata kiwe kipande... ila nilisikia Meno ya Juu yakitolewa vibaya unaweza poteza hata maisha....

Ahsante mkuu kwa ushaur wako japo n'likuwa nahitaji namna ya kutibu na c kung'oa maana nimeng'oa mpaka yameisha sasa
 
Kuna tunda linaitwa ndulele wengine wanaita ntulantu ukilipata hili yachukue kama kumi hv yaliyoiva(njano) then yachemshe upate supu yake kisha changanya na matone matano ya mafuta ya taa baada ya hapo safisha meno yako vizuru uhakikishe hakuna mabaki ya chakula kwenye matobo then sukutua hyo dawa, fanya asubuh na jioni na uhakikishe meno yako hayashindi na mabaki ya chakula ndani ya cku tatu utaona mabadiliko makubwa sana hata mimi nimesumbuliwa sana na meno ya kutoboka ila baada ya kutumia hyo dawa nimepona kabisa huwez amini

Ahsante kwa kunidadavulia maana nilishawahi isikia hii kitu ila sikuwa najua formular ya kutengeneza. Je, kila siku utakuwa unachemsha mpya au?
 
Ahsante mkuu kwa ushaur wako japo n'likuwa nahitaji namna ya kutibu na c kung'oa maana nimeng'oa mpaka yameisha sasa
Ok Mkuu Huyo Dr. anahuduma zote za meno unaweza ngoa na kuweka ya bandia mkuu... ila hiyo ya Ndulele ndio leo naisikia kwani na mimi ningekuwa nishaijarubu b4.... yaani tanzania hatuna watu wakaithibitisha kisha kuipaki vizuri kama Colgate...

Mkuu pia nimekumbuka Dawa ya kusafishia meno ya Sensodyne naypo ni kiboko ila kwa bei ipo juu... ila inamatokeo mazuri sana
 
"Tiba ya jino ni kung'oa", huo ni msemo ambao huko mtaani na hauna maana yoyote. Jino linaweza kutibiwa bila ya kung'olewa, kuna hospitali hapa Dar (kwa mfano Muhimbili, Temeke, Ilala, Agakhan) zinatoa huduma/tiba ya meno bila kung'oa. For more information, tembelea hospitali, onana na daktari wa meno (dentist), atakushauri nini cha kufanya.
 
ok! ahsante, ngoja nikamtafute kisha nitakuja na majibu
 
Ok Mkuu Huyo Dr. anahuduma zote za meno unaweza ngoa na kuweka ya bandia mkuu... ila hiyo ya Ndulele ndio leo naisikia kwani na mimi ningekuwa nishaijarubu b4.... yaani tanzania hatuna watu wakaithibitisha kisha kuipaki vizuri kama Colgate...

Mkuu pia nimekumbuka Dawa ya kusafishia meno ya Sensodyne naypo ni kiboko ila kwa bei ipo juu... ila inamatokeo mazuri sana
 
Hiyo yakusafisha meno kama yana rangi yanakua meupe
Umefukunyua thread ya miaka saba iliyopita dah!... Hata Dr. Wangu Akim alihamia NHC house Samora Avevue..

Meno Meupe Tumia Baking soda unachanganya na Ndimu kupiga mswaki mara mbili kwa wiki hadi weupe unaoutaka kisha acha. ila Yanadhoofisha meno ukitumia kwa siku mfululizo...
 
Back
Top Bottom