Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Matatizo ya kiafya katika kibofu cha mkojo yamekuwa
mengi hivi sasa, hasa kwa wanaume wenye umri kuanzia
miaka 50. Kazi kubwa ya kibofu ni kusaidia ukuaji wa
mbegu za kiume, kama kibofu kikiwa na matatizo, uzalishaji
wa mbegu za kiume nao hupungua sana na tatizo
lisipotibiwa haraka, husababisha ugumba. Aina nyingine ya
matatizo ya kibofu husababisha uvimbe sehemu za
siri.Inaelezwa kuwa matatizo ya kibofu mara nyingi huwa ni
ya kurithi, ingawa kuna sababu nyingine pia.
Ugonjwa unaweza kusambaa ukoo mzima, kutoka kizazi
kimoja hadi kingine. Sababu nyingine zinazosababisha
ugonjwa huu zinaelezwa kuwa ni kukaa kwa muda mrefu,
kuvaa nguo zinazobana, ukosefu wa choo na maambukizi.
Kupenda kujamiina sana nako kunaelezwa kuwa ni sababu
moja wapo. Pamoja na ukubwa wa tatizo hili ambalo
husababisha kansa pia, kuna habari njema kuwa matatizo
madogo ya kibofu yanaweza kutibiwa nyumbani kwa kula
vyakula na kufuata kanuna kadhaa na mtu akapona kabisa
au akazuia isimpate, lakini iwapo tatizo limeshakomaa na
kuwa sugu, unashauriwa kwenda hospitali na kuonana na
daktari haraka iwezekanavyo.
UTAJUAJE UNA TATIZO?
Dalili moja wapo ya mtu mwenye tatizo la kibofu ni kusikia
maumivu wakati wa kujisaidia haja ndogo. Dalili nyingine ni
kushindwa kukojoa kabisa licha ya kuhisi kubanwa na
mkojo. Dalili nyingine ni kusikia maumivu chini ya mgongo
na kwenye hips. Kwa kuwa mtu huwezi kujipima kama una
tatizo hilo, ina shauriwa kwenda hispitali kupima. Saratani
ya kibofu ni miongoni mwa matatizo yanayoweza kujitokeza
na inaweza kuuawa!
DONDOO ZA TIBA MBADALA..
Tiba mbadala ya matatizo ya kibofu hufanyakazi vizuri na
imeonesha mafanikio makubwa kwa watu waliowahi
kujaribu. Mbegu za maboga ni miongoni mwa tiba mbadala
za kutibu matatizo ya kibofu. Pondaponda kiasi cha mbegu
15 hadi 20 za maboga na changanya kwenye mlo wako wa
kila siku.Utaona mabadiliko ya haraka ya unafuu ndani ya
wiki mbili hadi tatu. Vitamini E ni kirutubisho muhimu sana
katika kutibu matatizo ya kibofu. Aidha, mboga za majani
rangi ya kijani, mayai na bidhaa zitokanazo na maziwa nazo
zina kiwango kikubwa cha vitamin E, hivyo viliwe kila
siku.Dawa nyingine mbadala ya matatizo ya kibofu ni
enema ya maji ya uvugu.
Enema ya aina hii ifanywe mara mbili au tatu kwa wiki ili
kurejesha utendaji wake wa kawaida. Uvutaji sigara na
unywaji pombe hauruhusiwi kabisa wakati wa kufanya tiba
hizi, hali kadhalika vyakula vilivyoungwa sana. Mwisho,
inashauriwa sana kuacha kunywa vinywaji vyote vyenye
caffeine, hii ni pamoja na chai na kahawa, kwa sababu
huzalisha matizo zaidi. Mazoezi ya nusu saa ya kukimbia au
kuendesha baiskeli yatasaidia zaidi. Kwa kuwa baridi ni
miongoni mwa sababu zinazochangia maradhi ya kibofu,
mgonjwa anayeishi sehemu yenye baridi anashauriwa
kuhamia sehemu yenye joto.
mengi hivi sasa, hasa kwa wanaume wenye umri kuanzia
miaka 50. Kazi kubwa ya kibofu ni kusaidia ukuaji wa
mbegu za kiume, kama kibofu kikiwa na matatizo, uzalishaji
wa mbegu za kiume nao hupungua sana na tatizo
lisipotibiwa haraka, husababisha ugumba. Aina nyingine ya
matatizo ya kibofu husababisha uvimbe sehemu za
siri.Inaelezwa kuwa matatizo ya kibofu mara nyingi huwa ni
ya kurithi, ingawa kuna sababu nyingine pia.
Ugonjwa unaweza kusambaa ukoo mzima, kutoka kizazi
kimoja hadi kingine. Sababu nyingine zinazosababisha
ugonjwa huu zinaelezwa kuwa ni kukaa kwa muda mrefu,
kuvaa nguo zinazobana, ukosefu wa choo na maambukizi.
Kupenda kujamiina sana nako kunaelezwa kuwa ni sababu
moja wapo. Pamoja na ukubwa wa tatizo hili ambalo
husababisha kansa pia, kuna habari njema kuwa matatizo
madogo ya kibofu yanaweza kutibiwa nyumbani kwa kula
vyakula na kufuata kanuna kadhaa na mtu akapona kabisa
au akazuia isimpate, lakini iwapo tatizo limeshakomaa na
kuwa sugu, unashauriwa kwenda hospitali na kuonana na
daktari haraka iwezekanavyo.
UTAJUAJE UNA TATIZO?
Dalili moja wapo ya mtu mwenye tatizo la kibofu ni kusikia
maumivu wakati wa kujisaidia haja ndogo. Dalili nyingine ni
kushindwa kukojoa kabisa licha ya kuhisi kubanwa na
mkojo. Dalili nyingine ni kusikia maumivu chini ya mgongo
na kwenye hips. Kwa kuwa mtu huwezi kujipima kama una
tatizo hilo, ina shauriwa kwenda hispitali kupima. Saratani
ya kibofu ni miongoni mwa matatizo yanayoweza kujitokeza
na inaweza kuuawa!
DONDOO ZA TIBA MBADALA..
Tiba mbadala ya matatizo ya kibofu hufanyakazi vizuri na
imeonesha mafanikio makubwa kwa watu waliowahi
kujaribu. Mbegu za maboga ni miongoni mwa tiba mbadala
za kutibu matatizo ya kibofu. Pondaponda kiasi cha mbegu
15 hadi 20 za maboga na changanya kwenye mlo wako wa
kila siku.Utaona mabadiliko ya haraka ya unafuu ndani ya
wiki mbili hadi tatu. Vitamini E ni kirutubisho muhimu sana
katika kutibu matatizo ya kibofu. Aidha, mboga za majani
rangi ya kijani, mayai na bidhaa zitokanazo na maziwa nazo
zina kiwango kikubwa cha vitamin E, hivyo viliwe kila
siku.Dawa nyingine mbadala ya matatizo ya kibofu ni
enema ya maji ya uvugu.
Enema ya aina hii ifanywe mara mbili au tatu kwa wiki ili
kurejesha utendaji wake wa kawaida. Uvutaji sigara na
unywaji pombe hauruhusiwi kabisa wakati wa kufanya tiba
hizi, hali kadhalika vyakula vilivyoungwa sana. Mwisho,
inashauriwa sana kuacha kunywa vinywaji vyote vyenye
caffeine, hii ni pamoja na chai na kahawa, kwa sababu
huzalisha matizo zaidi. Mazoezi ya nusu saa ya kukimbia au
kuendesha baiskeli yatasaidia zaidi. Kwa kuwa baridi ni
miongoni mwa sababu zinazochangia maradhi ya kibofu,
mgonjwa anayeishi sehemu yenye baridi anashauriwa
kuhamia sehemu yenye joto.