hovyohovyo
JF-Expert Member
- Jul 8, 2012
- 547
- 157
Wanajamvi, ktk utafiti wangu hapa Jf, nimegundua kuwa matatizo ktk ndoa yako mengi, na ama yalikuwepo siku zote au yanaongezeka au ni kwamba tu jf inatupa uhuru zaidi wa kuyaeleza. Haipiti siku hapa, hatujaona post, tena ya malalamiko kuhusu mke/mume/mpenzi, ama kuhusu tendo la ndoa, matumizi ya ndani, maamuzi, ndugu kuingilia ktk ndoa. Walau matatizo si haba. Hii crisis ya ndoa inatupeleka wapi? Tufanyeje ili ndoa ziwe mahali penye amani na upendo? Nini nafasi ya mume/mke ktk kuboresha ndoa? Ndugu/Jamaa wana nafasi gani au tuwape nafasi ipi ktk hili? TUJADILI