zombi
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,618
- 1,333
katika siku mbili zilizopita, kuna tatizo ambalo limenitokea mimi na wateja wengine wa matandao wa tigo, inatokea unampigia simu mtu anapokea mtu mwingine ambae siyo yule uliyempigia (sio wrong number scenario), inakua kama simu yako imekua diverted, nimeongea na watu wengine wawili ambao wanapata tatizo kama hilo. hii ni hatari kwani inaweza kufunja ndoa za watu sababu imetokea kwangu mke wangu alivyopiga amepokea mwanamke na kumuuliza we ni nani?, kama kuna mtu mwingine aliyeexperience jambo hili na ana taarifa zake na sababu ya kuwa hivyo, atumwagie hapa JF, nimeona ni muhimu kushare jambo hili hapa JF kwani inaweza kuwa imetokea kwa watu wengi zaidi.