Matarajio ya mzazi anapomsomesha mtoto ni yapi hasa?

Mwiyuzi

JF-Expert Member
Jun 30, 2011
845
429
Habari zenu wanajamvi,

Katika familia yetu mimi ndo nilifanikiwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu, wengine waliishia std 7 na wengine form four, japo kwa sasa wengine ni wajasiriamali na wengine ni ma day worker viwandani.

Nilimaliza chuo na kukaa muda mrefu bila ajira, lakini nikabahatika kupata kazi ya tempo ambayo ni ya miez mitano. Baada ya kupata kazi nilimpatia mama hela kama zawadi akashukuru, baada ya mwezi akaniomba nimkopeshe laki moja ili alipe deni kwani anadaiwa, nikaamua nimpatie hiyo laki moja bila kumkopesha, Baada ya miezi kama miwili akaniambia nitoe mchango kwa aliyekuwa rafiki yangu wa primary aliyekuwa akitarajia kufunga ndoa, nilikataa kutoa huo mchango kwani mtoto wa shangazi yangu alikuwa akihitaji ada kwa ajili ya kwenda shule, kwa hiyo nikampatia kiasi yule wakusoma, mama akaniambia kuwa kama nimeshindwa kutoa mchango wa harusi ya yule rafiki basi nimchangie hela ya zawadi atakayoitoa kwani huyo rafiki huwa anamsalimia vizuri...kusema ukweli sikumpatia hiyo hela.

Juzi kanipib nikapiga akaniambia nimpunguzie vocha, nikampunguzia vocha ya elfu tano lakini nikashangaa kuona kimya wakati vocha imeenda, kumpigia simu akasema kuwa hakurespond kwani alijua niko kanisani lakini kabla sijakata simu akasema kuwa sakafu ya nyumba yetu imebomoka na rangi ya nyumba imepauka so inabidi nigharimie.

Sasa mimi nikajiuliza kwamba hivi huyu mama kwa nini hataki kuelewa kuwa kazi niliyonayo ni tempo tu? Mshahara wangu ni mdogo lakini anademand kiasi hiki...hivi anataka mimi nifanyeje? Na kwa nini asiwaambie pia kaka zangu na dada ili nao wachangie kwa kuwa mimi bado sijasettle kimaisha? Je anafanya hivi kwa sababu mimi peke yangu ndo niliyesoma kwenye familia?

Kwa kweli simuelewi mama yangu! Manake nimeona kuwa ukiwa umesoma kwenye familia ndo unakuwa kwenye wakati mgumu wa kulaumiwa kupita wote...kwani ukimpatia mtu leo hela anakushukuru kwa mikono miwili lakini siku ukimwambia sina utasikia lawama kibao! Hivi na wazazi wengine wako hivi?
 
Hizo ni challange za maisha tu! Itakuwa mama yako ana high expectations na wewe, ndo maana anaamini kuwa wewe ndo utamtoa! La msingi endelea tu kufight tu utapata kazi nzuri, na hela zitatosha kumtimizia Bi Mkubwa wako! We uspanick wala kukwazika nenda nae taratibu si unajua tena bi mkubwa itakuwa kazoea enzi zile wasomii wana maana sana katika jamii, na wanaheshimika sana! We mwambie mimi uwezo wangu ni kukupa kiasi flani kwa mwezi, then Bi Mkubwa amua mwenyewe ukitumieje, tukiachana hapa mpaka mwisho wa mwezi
 
Ushauri wa hapo juu ni mzuri sana.
Nami naongezea kuwa kwavile wewe ni msomi, organize nduguzo hao ili muanzishe kitu kama fund ya kumwezesha mama. Kila mtu atamke kiasi atakachomudu kutoa per month, then mama atajipangia mwenyewe namna ya kuitumia, ili mradi asionekane msumbufu kwako!
Mama Theresa wa Calcutta alisema kuwa hakuna Tajiri asiyehitaji chochote, wala HAKUNA MASIKINI ASIYEWEZA KUTOA CHOCHOTE!
 
Bora wewe Mama tu vipi kama ndugu zako wote wangekuwa wakikutegemea?
Anza kujituma ili upate hela zaidi
 
Mwiyuzi Pole sana... Tukiwa tunakua hua mara nyingi kama watoto tunaamini kuwa wazazi wetu wapo exceptional kuliko wanadamu wengine, na sometimes kua hawana kasoro. Ambayo mara nyingi sio kweli.

Wazazi tumetofautiana, na kila mmoja hum treat mtoto wake (kwa kujitegemea kwake) tofauti na wengine. La muhimu ni kua ni muhimu sana kumpa heshima yake mzazi lakini pia inabidi umjue mzazi wako na kumsoma. Ukisha jua hulka yake ni rahsi kuenda nae sambamba. Huyo mama yako ni moja ya wale wenye kati ya hizi tabia...


  1. Anaona kua pale mtoto wake apatapo kazi ndio chanzo cha pesa kwa shida yoyote ile... Hii haitakuja kuisha hadi uweze i control namna gani unaweza iepuka.
  2. Ana amini kuwa once mtu yeyote yule awapo msomi (na hii ni wengi) basi anakuwa kila mara ana pesa (naona tokana na imani ya kuamini kuwa wasomi wote wanazo, yaani haiingii akilini kuwa huwezi kuwa na pesa). Kwa hili inabidi pia umuweke sawa na kumuelewesha huku ukimpa matumaini kuwa ukiwa sawa mwenyewe atafurahia.
  3. Anaona ni wajibu wako, na hupaswi kukataa... Kuwa yeye kakulea na kukufikisha hapo ulipo (in a way she is right), na kama kashikilia hili inabidi uwe makini sana jinsi ya kumuelewesha akaelewa na kutokwazika. Mie naamini sana katika radhi ya mzazi.. Jitahidi tu usifike mahala ukagombana naye.


Kwa mtazamo wangu the best way ni kukaa na kuongea nae kwa kujadili, upole na upendo kuwa bado haupo sawa na kwamba hata hivo utajitahidi walau kumpatia kiasi fulani cha pesa kwa mwezi mara moja ama mbili. Kwamba ukisha mpa hizo pesa msijuane... (labda dharula za msingi) Hii labda yaweza siadia wewe na yeye pia kuwa na amani... La muhimu kuliko yooote kumbuka ni mama yako na upo responsible kwake, tafuta tu njia ya kusema muivane huku ukimsaidia sababu usipoangalia utakuja mchukia... Which will be a disaster!
 
Hizo ni challange za maisha tu! Itakuwa mama yako ana high expectations na wewe, ndo maana anaamini kuwa wewe ndo utamtoa! La msingi endelea tu kufight tu utapata kazi nzuri, na hela zitatosha kumtimizia Bi Mkubwa wako! We uspanick wala kukwazika nenda nae taratibu si unajua tena bi mkubwa itakuwa kazoea enzi zile wasomii wana maana sana katika jamii, na wanaheshimika sana! We mwambie mimi uwezo wangu ni kukupa kiasi flani kwa mwezi, then Bi Mkubwa amua mwenyewe ukitumieje, tukiachana hapa mpaka mwisho wa mwezi


asante sana kwa ushauri...itabidi nifanye hivyo
 
Hizo ni challange za maisha tu! Itakuwa mama yako ana high expectations na wewe, ndo maana anaamini kuwa wewe ndo utamtoa! La msingi endelea tu kufight tu utapata kazi nzuri, na hela zitatosha kumtimizia Bi Mkubwa wako! We uspanick wala kukwazika nenda nae taratibu si unajua tena bi mkubwa itakuwa kazoea enzi zile wasomii wana maana sana katika jamii, na wanaheshimika sana! We mwambie mimi uwezo wangu ni kukupa kiasi flani kwa mwezi, then Bi Mkubwa amua mwenyewe ukitumieje, tukiachana hapa mpaka mwisho wa mwezi

lara 1 umezungumza vyema, utafikiri si yule wa kufunguka aka mcharuko tunayemfahamu!
By the way ishu zako na Boss wako zimeishia wapi?!
 
Last edited by a moderator:
habari zenu wanajamvi,

katika familia yetu mimi ndo nilifanikiwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu, wengine waliishia std 7 na wengine form four, japo kwa sasa wengine ni wajasiriamali na wengine ni ma day worker viwandani.

Nilimaliza chuo na kukaa muda mrefu bila ajira, lakini nikabahatika kupata kazi ya tempo ambayo ni ya miez mitano. Baada ya kupata kazi nilimpatia mama hela kama zawadi akashukuru, baada ya mwezi akaniomba nimkopeshe laki moja ili alipe deni kwani anadaiwa, nikaamua nimpatie hiyo laki moja bila kumkopesha, baada ya miezi kama miwili akaniambia nitoe mchango kwa aliyekuwa rafiki yangu wa primary aliyekuwa akitarajia kufunga ndoa, nilikataa kutoa huo mchango kwani mtoto wa shangazi yangu alikuwa akihitaji ada kwa ajili ya kwenda shule, kwa hiyo nikampatia kiasi yule wakusoma, mama akaniambia kuwa kama nimeshindwa kutoa mchango wa harusi ya yule rafiki basi nimchangie hela ya zawadi atakayoitoa kwani huyo rafiki huwa anamsalimia vizuri...kusema ukweli sikumpatia hiyo hela.

Juzi kanipib nikapiga akaniambia nimpunguzie vocha, nikampunguzia vocha ya elfu tano lakini nikashangaa kuona kimya wakati vocha imeenda, kumpigia simu akasema kuwa hakurespond kwani alijua niko kanisani lakini kabla sijakata simu akasema kuwa sakafu ya nyumba yetu imebomoka na rangi ya nyumba imepauka so inabidi nigharimie.

Sasa mimi nikajiuliza kwamba hivi huyu mama kwa nini hataki kuelewa kuwa kazi niliyonayo ni tempo tu? Mshahara wangu ni mdogo lakini anademand kiasi hiki...hivi anataka mimi nifanyeje? Na kwa nini asiwaambie pia kaka zangu na dada ili nao wachangie kwa kuwa mimi bado sijasettle kimaisha? Je anafanya hivi kwa sababu mimi peke yangu ndo niliyesoma kwenye familia?

Kwa kweli simuelewi mama yangu! Manake nimeona kuwa ukiwa umesoma kwenye familia ndo unakuwa kwenye wakati mgumu wa kulaumiwa kupita wote...kwani ukimpatia mtu leo hela anakushukuru kwa mikono miwili lakini siku ukimwambia sina utasikia lawama kibao! Hivi na wazazi wengine wako hivi?

mshukuru mungu mzazi wako, mama kabisa yupo hai na yupo karibu na wewe, mama anakupenda may be kutokana na usikivu wako na juhudi zako ktk maisha, siyo rahisi mama kupenda watoto wote kutokana na tabia za watoto kuwa tofauti, kwa hiyo ukiwa nayo mpe kwa moyo mkunjufu utabarikiwa kabisa nani kama mama? Changamoto kama hii me pia ninayo lakini mama ni mwelewa anajua nikiwa nazo lazima nitoe matumizi ya nyumbani, nikiwa kimya najua mwanangu hana pesa kwani ananipenda na siku zote ananiombea nifanikiwe zaidi mpaka kesho nipo tayari kumpigania mama kwani mama ni mama***love your mum, and you will be blessed 4rever***********
 
yan mi nashangaa kwa kwel..npo chuo wazaz wang wanasema ukimaliza nkipata hakuna kuhama nyumban..wala hawak kuckia naolewa bila kupata kaz ..hv jaman kaz c majariwa so hata nikae miaka20 bila kupata kaz nciolewa ...na matarajio yao ni kwamba nkiolewa ctowalipa fadhira..
ukwel watt wa mkulima tunasomeshwa ili tusaidie familia zetu..tena kwa lazma co hiari...utackia tucnge kusomesha tungekua na nyumba na magar sahv..
 
Ila sio siri, hiyo ya wazazi noma, experience yangu ni mbaya sio nzuri kabisa,
Maana kila issue wewe ndio wa kusolve, pesa utaoata waoi hakuna ajuaye mama anakuwa mkali balaa, Lazima utoe pesa na usipotoa hamuelewani. Pata shida inayohitaji uwepo tu wa ndugu uone! na akija anakuwambia mpe nauli sijui hilo mnalionaje jamani
 
Muda mwingi hupati sapoti sanasana lawama tu kila ukitoa inaonekana kidogo,
Yaani hapo mimi sisemi nakwazika ile kinoma
 
Niliuguliwa nikawa natumia elfu 45 kila siku na mgonjwa anajua, hapo akija mtu kumuona, mgonjwa anakuuliza umeshampatia nauli. Imagine nauli ya kurudia na aliyokujia inabidi umpatie. Hapo angalia unavyokwazika. Hapo wengine ndio kama maisha yetu. Demand nyingi mpaka unakimbia
 
lara 1 umezungumza vyema, utafikiri si yule wa kufunguka aka mcharuko tunayemfahamu!
By the way ishu zako na Boss wako zimeishia wapi?!

Hahaaaa! Mimi mama ushauri umesahau!!!! (NANI KANUNA????) Bosi yupo bado anajilia vya bure! Mission ya bosi Nimeiabort nimeona iatanicost economically!!! We fikiria nikitoka nae hapo hata akinipunguzia OT siwez kulalamika manake ndo mtu wangu hivo! Watu wakimsema me ndo niumie badala ya kuongezea midongo! Hapo akiamua anakuomba uje jmosi bila OT! Akuuuuuu! hiyo itakuwainvestment ZEMBE. Amakweli PENZI KITOVU CHA UZEMBE!!!!!!
 
POle sana Mkuu,but jambo moja ni kwamba,tafuta pesa umfungulie biashara ili awe anapata pesa humo,hayo ni ya kawaida mkuu
 
Dah, napata picha ukija kuoa itakuwaje? My boyfriend alikuwa na tatizo kama hilo, yeye mamayake alikuwa akija home anamwambie siondoki hadi unipe one million! Kwa vile jamaa alilelewa na mama basi anajikamua hadi anampa mama 1 m, halafu anapigaje miayo??Be very careful na hayo masuala otherwise utayumba sana kiuchumi na hata kisaikolojia utaathirika. All in all mama ni mama, do the best you can to satisfy her whenever you get a chance ila kama ataendelea kuwa so demanding kaa nae na mueleweshe I believe atakuelewa tena do that as soon as possible before you get married!
 
Hahaaaa! Mimi mama ushauri umesahau!!!! (NANI KANUNA????) Bosi yupo bado anajilia vya bure! Mission ya bosi Nimeiabort nimeona iatanicost economically!!! We fikiria nikitoka nae hapo hata akinipunguzia OT siwez kulalamika manake ndo mtu wangu hivo! Watu wakimsema me ndo niumie badala ya kuongezea midongo! Hapo akiamua anakuomba uje jmosi bila OT! Akuuuuuu! hiyo itakuwainvestment ZEMBE. Amakweli PENZI KITOVU CHA UZEMBE!!!!!!

Ungeendelea tu, huwezi kujua labda ungepata ka-promotion!:redface:
Probably na visafari vya hapa na pale mkiwa naye, na kujikuta unajipatia per diem za bure na raha za bure, LOL!
 
Dah, napata picha ukija kuoa itakuwaje? My boyfriend alikuwa na tatizo kama hilo, yeye mamayake alikuwa akija home anamwambie siondoki hadi unipe one million! Kwa vile jamaa alilelewa na mama basi anajikamua hadi anampa mama 1 m, halafu anapigaje miayo??Be very careful na hayo masuala otherwise utayumba sana kiuchumi na hata kisaikolojia utaathirika. All in all mama ni mama, do the best you can to satisfy her whenever you get a chance ila kama ataendelea kuwa so demanding kaa nae na mueleweshe I believe atakuelewa tena do that as soon as possible before you get married!
Kama uwezo wako kwa siku unapata zaidi ya milioni moja.Kwani kumpa mama yako milioni moja kuna tatizo gani.Mama hawezi kumdai mwanae milioni moja kama hajui uwezo wake.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom