Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Nadhani nitakuwa sawa kama nikisema kwamba Tanzania haijawahi kuwa na post election fever and enxiety ndefu kama hii ya wakati huu.
Kadri hali ya siasa za Tz inavyozidi kuchacha, hali ya kiuchumi inavyozidi kuwa ngumu, serikali inavyoshindwa kuongoza, upinzani unavyozidi kuimarika, basi wananchi wengi wanazidi kuwa na shauku ya ni lini mabadiliko yatatokea.
Wafanya kazi wa serikalini, mashirika ya umma na asasi zisizo za kiserikali, wote wanafuatilia siasa za nchi hii wakati huu kuliko vipindi vingine vyote awali katika nchi hii. Vyanzo vya habari vinatumika barabara, iwe magazeti, runinga, blogu, simu, au mijadala ya ana kwa ana. Tofauti na zama nyingine zote Tanzania, wakati huu, hakuna mwananchi asiyejua nchi iko kwenye tatizo gani. Most public servants are blogging against their government!!
kwa sababu hiyo, utaona kwamba watz wengi sasa wana hamu ya kuona nini hatima ya haya mambo, ingawa haiko wazi hatima inayotarajiwa ni ipi ilimradi kila mtu anatarajia jambo fulani kubwa litokee. Kuna wanaoamini tunahitaji kufanya kama Tunisia, sasa hivi. Kuna wanatamani utokee muujiza viongozi wa juu wa serikali wabadilike ghafula. Kuna wanaotamani 2015 ifike kesho. Kuna wanatamani uchaguzi mkuu urudiwe leo! Kuna wanaoamini kwamba Bunge litakomesha hii hali, litaleta mabadiliko.
La msingi ni kwamba, fikra za watz wengi ziko kwenye matarajio ya mabadiliko na wanatumia muda mwingi kufuatilia na kutamani kinachoendelea kuliko wanavyofikiri na kufanya kazi zao. Haina maana kwamba kazi hazifanyiki kabisa, lakini nadhani siyo kwa tija kama ambavyo hii hali isingekuwepo. Ni kama kusema watu wanalazimika tu kuamka asubuhi na kwenda kazini, hawajisikii. Muda mwingi kutwa wanafuatilia habari kwa njia mbalimbali.
Kadri hali ya siasa za Tz inavyozidi kuchacha, hali ya kiuchumi inavyozidi kuwa ngumu, serikali inavyoshindwa kuongoza, upinzani unavyozidi kuimarika, basi wananchi wengi wanazidi kuwa na shauku ya ni lini mabadiliko yatatokea.
Wafanya kazi wa serikalini, mashirika ya umma na asasi zisizo za kiserikali, wote wanafuatilia siasa za nchi hii wakati huu kuliko vipindi vingine vyote awali katika nchi hii. Vyanzo vya habari vinatumika barabara, iwe magazeti, runinga, blogu, simu, au mijadala ya ana kwa ana. Tofauti na zama nyingine zote Tanzania, wakati huu, hakuna mwananchi asiyejua nchi iko kwenye tatizo gani. Most public servants are blogging against their government!!
kwa sababu hiyo, utaona kwamba watz wengi sasa wana hamu ya kuona nini hatima ya haya mambo, ingawa haiko wazi hatima inayotarajiwa ni ipi ilimradi kila mtu anatarajia jambo fulani kubwa litokee. Kuna wanaoamini tunahitaji kufanya kama Tunisia, sasa hivi. Kuna wanatamani utokee muujiza viongozi wa juu wa serikali wabadilike ghafula. Kuna wanaotamani 2015 ifike kesho. Kuna wanatamani uchaguzi mkuu urudiwe leo! Kuna wanaoamini kwamba Bunge litakomesha hii hali, litaleta mabadiliko.
La msingi ni kwamba, fikra za watz wengi ziko kwenye matarajio ya mabadiliko na wanatumia muda mwingi kufuatilia na kutamani kinachoendelea kuliko wanavyofikiri na kufanya kazi zao. Haina maana kwamba kazi hazifanyiki kabisa, lakini nadhani siyo kwa tija kama ambavyo hii hali isingekuwepo. Ni kama kusema watu wanalazimika tu kuamka asubuhi na kwenda kazini, hawajisikii. Muda mwingi kutwa wanafuatilia habari kwa njia mbalimbali.