Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
MATANGAZO HAYA VIPI JIJINI
Ndugu wananchi
Kama kuna mtu leo amepita barabara ya bagamoyo leo , kuna kitu cha ajabu pale Kituo cha Mafuta bamaga nacho ni Lile Tangazo la kisasa kwenye gari , toka kampuni ya Mile Stone , ule mwanga wa tangazo lile ni mkali sana nilipofika pale nilishtuka sana macho yangu yaliumia , nikafikiria je wazee ambao macho yao sio mazuri sana inakuwaje haswa wanaoendesha magari ? usalama wa waendesha magari pale unalindwaje ? Hivi jiji limekubaliana na watu hawa kuweka matangazo yao popote bila kufanya utafiti wa kutosha kuhusu athari zake mbali mbali ?
Lile tangazo liko karibu na TBC1 , ITV nimeshangaa hata katika taarifa zao za leo usiku hawajagusia jambo hili , hata kwenye vipindi mbali mbali vya usalama barabarani watangazaji hawaongelei suala hili la matangazo ya mwanga .
Naamini wahusika watafanyia kazi tatizo hili ili huko mbeleni lisije kupoteza maisha ya watu kwa ajali zinazosababishwa na mwanga ule .
Ila kama wakiendelea na tabia hizi basi usishangae siku moja kukuta tangazo juu ya taa za kuongozea magari , kama lile lilopo Benjamin mkapa towers linalotazamana na Kituo cha Mabasi , Mimi naona ni kosa Ile sio sehemu ya Tangazo , matangazo yawekwe angalau sehemu tulivu
Tusiweke matangazo kwa kuiga miundombinu yetu haijaandaliwa kwa ujio wa aina hii ya matangazo bado , hata jamii inapaswa kuelezwa , kufundishwa na kuelewa kisha wakubali wenyewe
Ndugu wananchi
Kama kuna mtu leo amepita barabara ya bagamoyo leo , kuna kitu cha ajabu pale Kituo cha Mafuta bamaga nacho ni Lile Tangazo la kisasa kwenye gari , toka kampuni ya Mile Stone , ule mwanga wa tangazo lile ni mkali sana nilipofika pale nilishtuka sana macho yangu yaliumia , nikafikiria je wazee ambao macho yao sio mazuri sana inakuwaje haswa wanaoendesha magari ? usalama wa waendesha magari pale unalindwaje ? Hivi jiji limekubaliana na watu hawa kuweka matangazo yao popote bila kufanya utafiti wa kutosha kuhusu athari zake mbali mbali ?
Lile tangazo liko karibu na TBC1 , ITV nimeshangaa hata katika taarifa zao za leo usiku hawajagusia jambo hili , hata kwenye vipindi mbali mbali vya usalama barabarani watangazaji hawaongelei suala hili la matangazo ya mwanga .
Naamini wahusika watafanyia kazi tatizo hili ili huko mbeleni lisije kupoteza maisha ya watu kwa ajali zinazosababishwa na mwanga ule .
Ila kama wakiendelea na tabia hizi basi usishangae siku moja kukuta tangazo juu ya taa za kuongozea magari , kama lile lilopo Benjamin mkapa towers linalotazamana na Kituo cha Mabasi , Mimi naona ni kosa Ile sio sehemu ya Tangazo , matangazo yawekwe angalau sehemu tulivu
Tusiweke matangazo kwa kuiga miundombinu yetu haijaandaliwa kwa ujio wa aina hii ya matangazo bado , hata jamii inapaswa kuelezwa , kufundishwa na kuelewa kisha wakubali wenyewe