Matangazo haya - jiji wamelala

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
MATANGAZO HAYA VIPI JIJINI

Ndugu wananchi

Kama kuna mtu leo amepita barabara ya bagamoyo leo , kuna kitu cha ajabu pale Kituo cha Mafuta bamaga nacho ni Lile Tangazo la kisasa kwenye gari , toka kampuni ya Mile Stone , ule mwanga wa tangazo lile ni mkali sana nilipofika pale nilishtuka sana macho yangu yaliumia , nikafikiria je wazee ambao macho yao sio mazuri sana inakuwaje haswa wanaoendesha magari ? usalama wa waendesha magari pale unalindwaje ? Hivi jiji limekubaliana na watu hawa kuweka matangazo yao popote bila kufanya utafiti wa kutosha kuhusu athari zake mbali mbali ?

Lile tangazo liko karibu na TBC1 , ITV nimeshangaa hata katika taarifa zao za leo usiku hawajagusia jambo hili , hata kwenye vipindi mbali mbali vya usalama barabarani watangazaji hawaongelei suala hili la matangazo ya mwanga .

Naamini wahusika watafanyia kazi tatizo hili ili huko mbeleni lisije kupoteza maisha ya watu kwa ajali zinazosababishwa na mwanga ule .

Ila kama wakiendelea na tabia hizi basi usishangae siku moja kukuta tangazo juu ya taa za kuongozea magari , kama lile lilopo Benjamin mkapa towers linalotazamana na Kituo cha Mabasi , Mimi naona ni kosa Ile sio sehemu ya Tangazo , matangazo yawekwe angalau sehemu tulivu

Tusiweke matangazo kwa kuiga miundombinu yetu haijaandaliwa kwa ujio wa aina hii ya matangazo bado , hata jamii inapaswa kuelezwa , kufundishwa na kuelewa kisha wakubali wenyewe
 
MATANGAZO HAYA VIPI JIJINI

Ndugu wananchi

Kama kuna mtu leo amepita barabara ya bagamoyo leo , kuna kitu cha ajabu pale Kituo cha Mafuta bamaga nacho ni Lile Tangazo la kisasa kwenye gari , toka kampuni ya Mile Stone , ule mwanga wa tangazo lile ni mkali sana nilipofika pale nilishtuka sana macho yangu yaliumia , nikafikiria je wazee ambao macho yao sio mazuri sana inakuwaje haswa wanaoendesha magari ? usalama wa waendesha magari pale unalindwaje ? Hivi jiji limekubaliana na watu hawa kuweka matangazo yao popote bila kufanya utafiti wa kutosha kuhusu athari zake mbali mbali ?

Lile tangazo liko karibu na TBC1 , ITV nimeshangaa hata katika taarifa zao za leo usiku hawajagusia jambo hili , hata kwenye vipindi mbali mbali vya usalama barabarani watangazaji hawaongelei suala hili la matangazo ya mwanga .

Naamini wahusika watafanyia kazi tatizo hili ili huko mbeleni lisije kupoteza maisha ya watu kwa ajali zinazosababishwa na mwanga ule .

Ila kama wakiendelea na tabia hizi basi usishangae siku moja kukuta tangazo juu ya taa za kuongozea magari , kama lile lilopo Benjamin mkapa towers linalotazamana na Kituo cha Mabasi , Mimi naona ni kosa Ile sio sehemu ya Tangazo , matangazo yawekwe angalau sehemu tulivu

Tusiweke matangazo kwa kuiga miundombinu yetu haijaandaliwa kwa ujio wa aina hii ya matangazo bado , hata jamii inapaswa kuelezwa , kufundishwa na kuelewa kisha wakubali wenyewe

Lingekuwa Tangazo linahusiana na UFISADI wangekuwa washatangaza kwenye Taarifa ya Habari zao
 
Sijaona tatizo na hilo Tangazo,

Shy,

When did you last visit the "eye-clinic"? If not very recently you may need to see the optician ASAP.

Matangazo (Billboards) lazima ziwe zinalazimisha wananchi kulitazama na sio "eyesore"!
 
Back
Top Bottom