kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
mastaa kama Jackson Makwaya Bambo , Hamis Changale Mtanga, Rashid Mwishekhe Kingwendu, Yusuf Hamis Zimwi Sunche na Kapeto wakiwa wamepanga foleni ya kuingia kwenye usaili mara baada ya kujaza fomu.
Chipukizi waliokuwa wakiwania nafasi hiyo, hawakufurahishwa na kitendo cha wasanii kwenda kugombania nao nafasi kwakuwa tayari wana majina makubwa hali iliyosababisha waanze kuwazodoa.
Hawa wamefuata nini hapa, si wameshaonekana kwenye runinga? Mbona wanakuja kutubania nafasi zetu? Hawaoni hata aibu kujipanga foleni na sisi? Alisikika akingaka underground mmoja huku akiwaangalia wasanii hao ambao walikuwa kama hawasikii.
Si ndiyo hapo hata mimi nashangaa! Badala ya kutuachia sisi wasanii wachanga tuuze sura kwenye kioo, wao wanakuja kubanana na sisi. Kwa staa kama Bambo hakuna asiye jua uwezo wake, inakuwaje aje kujidhalilisha hapa?Alidakia chipukizi mwingine.
Lakini baadaye, Mtanga aliamua kuvunja ukimya kwa kusema: Haya yote ni maisha tu. Tumekuja hapa kusaka nafasi hii adimu ya kujiachia kwenye runinga tunavyotaka. Hawa wasanii wanaojiita underground walie tu, tutakomaa nao humuhumu.
Hadi Paparazi wetu anangoa eneo hilo, wasanii hao walikuwa bado hawajaingia kwenye usaili kwani kulikuwa na bonge la foleni, hivyo kutojua kama walifanikiwa kupata nafasi au lah!
Chipukizi waliokuwa wakiwania nafasi hiyo, hawakufurahishwa na kitendo cha wasanii kwenda kugombania nao nafasi kwakuwa tayari wana majina makubwa hali iliyosababisha waanze kuwazodoa.
Hawa wamefuata nini hapa, si wameshaonekana kwenye runinga? Mbona wanakuja kutubania nafasi zetu? Hawaoni hata aibu kujipanga foleni na sisi? Alisikika akingaka underground mmoja huku akiwaangalia wasanii hao ambao walikuwa kama hawasikii.
Si ndiyo hapo hata mimi nashangaa! Badala ya kutuachia sisi wasanii wachanga tuuze sura kwenye kioo, wao wanakuja kubanana na sisi. Kwa staa kama Bambo hakuna asiye jua uwezo wake, inakuwaje aje kujidhalilisha hapa?Alidakia chipukizi mwingine.
Lakini baadaye, Mtanga aliamua kuvunja ukimya kwa kusema: Haya yote ni maisha tu. Tumekuja hapa kusaka nafasi hii adimu ya kujiachia kwenye runinga tunavyotaka. Hawa wasanii wanaojiita underground walie tu, tutakomaa nao humuhumu.
Hadi Paparazi wetu anangoa eneo hilo, wasanii hao walikuwa bado hawajaingia kwenye usaili kwani kulikuwa na bonge la foleni, hivyo kutojua kama walifanikiwa kupata nafasi au lah!