Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Maslahi ya taifa kwanza, siasa baadaye-Mengi
Na Omari Moyo, Arusha
SERIKALI, vyama vya kisiasa na viongozi wa kidini wametakiwa kushirikiana katika utatuzi wa migogoro inayojitokeza nchini hasa ya kisiasa kuhakikisha amani ya
nchi haichafuki kama ilivyowahi kutokea kwenye nchi za Rwanda na Burundi.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Bw. Reginald Mengi wakati akizungumza kwenye mahafali ya 19 ya kidato cha sita cha Shule ya Sekondari Ilboru, mjini Arusha.
Alisema kwamba malumbano ya kisiasa yanayoendelea nchini na matamko mbalimbali ya viongozi wa dini na wa kisiasa hayana faida kwa mustakabali wa taifa la Watanzania, kwa kuwa matamko hayo yanaashiria machafuko, siyo kuleta amani.
Bw. Mengi alishauri kuwa ni vyema dini zingekuwa zikitoa matamko yasiyokinzana na yasiyokuwa na muelekeo wa kisiasa na kuwataka viongozi wa kisiasa badala ya kuchafua zaidi hali ya hewa, wakae chini na kukubaliana kuhusu tofauti zao, kwa mustakabali wa Tanzania.
âHawa viongozi wa dini, wa siasa na serikali zisifanye maamuzi kwa ajili ya matakwa ya wachache, lazima waelewe wazi kwamba hakuna jambo muhimu kama la kuweka maslahi ya taifa mbele. Wakubaliane kwenye hoja za kuliondoa taifa kwenye machafuko, kwanza wazungumze ya kwao, na wajue kwamba yaliyotokea nchi za Burundi na Rwanda hata Tanzania yanaweza kutokea,â� alisisitiza Bw. Mengi.
Aliongeza, âmimi mmenialika hapa Arusha shuleni kwenu, na nimekuja kwa raha kabisa na kifua mbele, je, kungekuwa hakuna amani ningekuja? Kwa hiyo ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha suala la amani ya Watanzani mbele ndipo yafuate mambo mengine,â� alisema Bw. Mengi.
Na Omari Moyo, Arusha
SERIKALI, vyama vya kisiasa na viongozi wa kidini wametakiwa kushirikiana katika utatuzi wa migogoro inayojitokeza nchini hasa ya kisiasa kuhakikisha amani ya
nchi haichafuki kama ilivyowahi kutokea kwenye nchi za Rwanda na Burundi.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Bw. Reginald Mengi wakati akizungumza kwenye mahafali ya 19 ya kidato cha sita cha Shule ya Sekondari Ilboru, mjini Arusha.
Alisema kwamba malumbano ya kisiasa yanayoendelea nchini na matamko mbalimbali ya viongozi wa dini na wa kisiasa hayana faida kwa mustakabali wa taifa la Watanzania, kwa kuwa matamko hayo yanaashiria machafuko, siyo kuleta amani.
Bw. Mengi alishauri kuwa ni vyema dini zingekuwa zikitoa matamko yasiyokinzana na yasiyokuwa na muelekeo wa kisiasa na kuwataka viongozi wa kisiasa badala ya kuchafua zaidi hali ya hewa, wakae chini na kukubaliana kuhusu tofauti zao, kwa mustakabali wa Tanzania.
âHawa viongozi wa dini, wa siasa na serikali zisifanye maamuzi kwa ajili ya matakwa ya wachache, lazima waelewe wazi kwamba hakuna jambo muhimu kama la kuweka maslahi ya taifa mbele. Wakubaliane kwenye hoja za kuliondoa taifa kwenye machafuko, kwanza wazungumze ya kwao, na wajue kwamba yaliyotokea nchi za Burundi na Rwanda hata Tanzania yanaweza kutokea,â� alisisitiza Bw. Mengi.
Aliongeza, âmimi mmenialika hapa Arusha shuleni kwenu, na nimekuja kwa raha kabisa na kifua mbele, je, kungekuwa hakuna amani ningekuja? Kwa hiyo ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha suala la amani ya Watanzani mbele ndipo yafuate mambo mengine,â� alisema Bw. Mengi.