Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,486
- 86,002
Juzi nikiwa nipo home ndo nimetoka kwenye ujenzi wa Taifa hili lisilojengeka, alinijia Mke wa Jirani yangu na akaanza kunieleza hadithi ndefu ambayo kwa hakika ilikuwa ni mwendelezo wa hadithi ya toleo lililopita tu.
Kwa uchungu kaniambia; baba fulani amewekwa mahabusu baada ya mdhamini kutoweka...na hivyo atakua huko hadi tarehe 16 June, 2010. Nikajiuliza kwa uchungu, Ina maana jiarani yangu huyu sitamuona tena kwene Mechi za Kwanza za WC?
Huyu jamaa, kesi yake eti, kakamatwa na Trafic wale pale Kibaha, taa moja ya mbele ilikuwa haiwaki vizuri, baada ya kukataa kumpa kile alichokitaka askarii yule, akampeleka polisi na kumbadilishia mashitaka; kuwa amekamatwa baada ya ku-overtake magari saba! Baada ya kupelekwa mahakamani, Askari huyu alionekana siku moja tu na baada ya hapo hajawahi kuonekana tena mahakamani, huku kijana huyu akiteseka kwa safari za kutoka Dar kwenda Kibaha kusikiliza kesi isiyokuwa na kesi
Juzi, mdhamini wake kachoka na yeye akaamua kujitoa, Kule wanataka mdhamini ambaye anaishi Kibaha na si nje ya hapo, hivyo ikabidi apelekwe mahabusu huku askari yule akiwa haonekani.
Siandiki ili kumtetea, ila swali la msingi ni hivi: Kwa wale wenzangu ambao na madereva, hivi unaweza ku-overtake magari saba yote yakiwa yanatembea na mtu aliesimama kando, ayahesabu? Nauliza hivi kwani, ku-overtake gari moja ambalo pia lina mwendo hukuchuku takribani mita si chini ya 75- hadi 100, hivyo ku-overtake magari saba ni kama mita 500 hivi. Nikajiuliza kuwa, huyu askari alimwonaje?
Alikuwa hewani au wapi? Lakini, hivi na nyie Mahakimu, huwa hamuangalii logic ya makosa, au kwa sababu ni kosa tu basi halina mantiki?
Siamini kuwa, kila dereva wa dala dala ni mhuni, ila wapo baadhi tu kama vile ambavyo wapo pia polisi wanaotunga kesi.
Jioni njema
Kwa uchungu kaniambia; baba fulani amewekwa mahabusu baada ya mdhamini kutoweka...na hivyo atakua huko hadi tarehe 16 June, 2010. Nikajiuliza kwa uchungu, Ina maana jiarani yangu huyu sitamuona tena kwene Mechi za Kwanza za WC?
Huyu jamaa, kesi yake eti, kakamatwa na Trafic wale pale Kibaha, taa moja ya mbele ilikuwa haiwaki vizuri, baada ya kukataa kumpa kile alichokitaka askarii yule, akampeleka polisi na kumbadilishia mashitaka; kuwa amekamatwa baada ya ku-overtake magari saba! Baada ya kupelekwa mahakamani, Askari huyu alionekana siku moja tu na baada ya hapo hajawahi kuonekana tena mahakamani, huku kijana huyu akiteseka kwa safari za kutoka Dar kwenda Kibaha kusikiliza kesi isiyokuwa na kesi
Juzi, mdhamini wake kachoka na yeye akaamua kujitoa, Kule wanataka mdhamini ambaye anaishi Kibaha na si nje ya hapo, hivyo ikabidi apelekwe mahabusu huku askari yule akiwa haonekani.
Siandiki ili kumtetea, ila swali la msingi ni hivi: Kwa wale wenzangu ambao na madereva, hivi unaweza ku-overtake magari saba yote yakiwa yanatembea na mtu aliesimama kando, ayahesabu? Nauliza hivi kwani, ku-overtake gari moja ambalo pia lina mwendo hukuchuku takribani mita si chini ya 75- hadi 100, hivyo ku-overtake magari saba ni kama mita 500 hivi. Nikajiuliza kuwa, huyu askari alimwonaje?
Alikuwa hewani au wapi? Lakini, hivi na nyie Mahakimu, huwa hamuangalii logic ya makosa, au kwa sababu ni kosa tu basi halina mantiki?
Siamini kuwa, kila dereva wa dala dala ni mhuni, ila wapo baadhi tu kama vile ambavyo wapo pia polisi wanaotunga kesi.
Jioni njema