Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Jana kwenye kituo cha Runinga cha Chanel 10 walirusha habari ikionyesha uchafuzi wa mazingira wa hali ya juu ambapo kuna kiwanda kimoja kimeruhusu sumu kutiririka kwenye bonde la Mto Msimbazi na kusababisha mauaji ya Samaki ambao walionyeshwa. Lakini pia kuna Mama mmoja alieleza kuwa kuku wake kadhaa walikufa baada ya kunywa maji ya mto huo.
Lakini kingine kilichojitokeza sambamba na hilo ni pale Mkuu wa Wilaya (wakati akitembelea eneo hilo kujionea uchafuzi wa mazingira huo) alipokutana uso kwa uso na Masela wakiendelea kuyasaka mahela kwa kuuziana Bangi na wengine wakilivita Bangi hilo kwenye Bonde hilo. Jamaa sijui ndo Bongi lilishawakolea au kutomfahamu mwenye himaya ya Wilaya hiyo wala hawakuonyesha msituko.
Mh. Magufuli kuna tofauti gani ya hawa wenye Kiwanda na wale Wavuvi wanaotumia Makokoro na Baruti, au hawa Samaki siyo wa Wizara yako.
Hili Jiji letu litaendelea kuwa chafu hivi mpaka lini/ Lukuvi uko wapi?
Lakini kingine kilichojitokeza sambamba na hilo ni pale Mkuu wa Wilaya (wakati akitembelea eneo hilo kujionea uchafuzi wa mazingira huo) alipokutana uso kwa uso na Masela wakiendelea kuyasaka mahela kwa kuuziana Bangi na wengine wakilivita Bangi hilo kwenye Bonde hilo. Jamaa sijui ndo Bongi lilishawakolea au kutomfahamu mwenye himaya ya Wilaya hiyo wala hawakuonyesha msituko.
Mh. Magufuli kuna tofauti gani ya hawa wenye Kiwanda na wale Wavuvi wanaotumia Makokoro na Baruti, au hawa Samaki siyo wa Wizara yako.
Hili Jiji letu litaendelea kuwa chafu hivi mpaka lini/ Lukuvi uko wapi?