Mashushushu wa Fidel Castro walikuwa na hisia ya sita(Sixth Sense)

Sep 28, 2014
78
113
Mashushushu hawa ndio wenye mafanikio makubwa kuliko wote Duniani.

Njama 638 za mauaji aliyoepuka Fidel Castro.(Chini ya mashushushu wenye ustadi wa hali ya juu sana(skillful)

Njama ya kutumia sigara kumuua Fidel Castro ambayo ilitibuka inajulikana sana, lakini njama nyengine 637 dhidi ya maisha yake ni zipi?

Shirika la kijasusi nchini Marekani CIA na watu waliotoroka Cuba wakati wa uongozi wa Castro walitumia nusu ya karne moja kufanya njama za kumuua kiongozi ambaye taifa lake lina athari kubwa kwa Marekani, kulingana na balozi wa Marekani nchini Cuba Wayne Smith.

Wakati mmoja kiongozi huyo wa Cuba alinukuliwa akisema, iwapo kuepuka majaribio ya mauaji kungekuwa miongoni mwa michezo ya Olimpiki ningejishindia medali ya dhahabu.

Hatahivyo baadhi ya njama hizo hazikutekelezwa ,kulingana na aliyekuwa mlinzi wa zamani wa Fidel Castro, Fabian Escalante.

Stakhabadhi zilizofichuliwa wakati wa utawala wa Bill Clinton zilionyesha kuwa CIA wakati mmoja walianza kuwafanyia utafiti konokono wa eneo la Carebean.

Njama, ilikuwa kutafuta konokono mmoja ambaye angemvutia Castro anayependa sana kuogelea na kumjaza vilipuzi ndani yake kabla ya kumlipua Castro atakapomshika

Mpango mwengine ulikuwa ule wa kutengeza boya la kuogelea ambalo huvaliwa kama shati na ambalo lingetiwa ugonjwa mbaya wa ngozi ili kumuathiri kiongozi huyo.

Mipango yote hiyo ilitupiliwa mbali.

Ajenti huyo alisikitika na akataka mpango mwengine ambao sio rahisi kuugundua,ripoti hiyo ilisema. Mpenzi wa zamani wa Castro, Marita Lorenz alipewa dawa za sumu kumwekea katika kinywaji chake.

Alipewa dawa zenye sumu ili kuweka katika kinywaji cha Castro.Lakini Castro aligundua jaribio hilo na anadaiwa kumpatia bunduki yake badala yake atumie kumuua.

''Huwezi kuniua. Hakuna anayeweza kuniua,"Bbi Lorenzo alisema Bw Castro alimwambia, alipokuwa anahojiwa na gazeti la New York daily.

Castro alidaiwa kutabasamu na kuendelea kuvuta sigara yake.''Nilijihisi nimetolewa pumzi kwa sababu alikuwa na uhakika juu yangu.Alinikumbatia na tukafanya mapenzi''.

Jaribio jingine lililokuwa maarufu dhidi ya maisha ya Castro ni lile la 2000, wakati ambapo mpango uliwekwa kuweka vilipuzi vingi katika jukwaa ambalo alitarajiwa kuhutubia nchini Panama.

Mpango huo ulitibuliwa na vikosi vya usalama vya Castro.

Watu wanne ikiwemo mtoto mmoja wa Cuba pamoja na ajenti wa CIA kwa jina Luis Posada walifungwa lakini baadaye wakaachiliwa.

Pia kulikuwa na mipango ya kumfanya Castro ambaye pia anajulikana '' The Beared'' aonekana kama chombo cha kukejeliwa badala ya kumuua.

Mpango mmoja ulikuwa kumwagia viatu vyake chumvi ya thallium wakati wa ziara yake ya ughaibuni kwa lengo kwamba anaposhika ndevu zake zingeweza kukatika.

Lakini mpango huo ulitibuliwa baada ya Castro kuahirisha ziara hiyo.Castro alichukua tahadhari ya hali ya juu ili kuwakwepa watu waliopanga mauaji yake.

Mwaka 1979 alipokuwa akielekea mjini New York ili kuhutubia mkutano wa Umoja wa Mataifa hakuweza kuwazuia wanahabari waliomuuliza iwapo alikuwa amevaa fulana ya ndani ambayo ina kinga dhidi ya risasi, alivua shati lake na kuwaonyesha kifua chake.
''Nimevaa fulana ya kawaida'',alisema.

Miongo kadhaa awali mwaka 1975, tume ya bunge la seneti nchini Marekani ilifichua maelezo ya njama nane dhidi ya maisha ya Castro kwa kutumia vifaa ambavyo tume hiyo inasema ''vinachosha akili''.

Njama moja iliopangwa na ambayo karibu ifaulu mara mbili ilikuwa ile ya kutuma dawa za sumu Cuba na kuwapeleka watu kumuua kiongozi huyo.

Ndevu za Fidel Castro pia zililengwa katika njama hizo za mauaji.

Ulikuwa wakati kama huo ambapo rais Kennedy, ambaye aliruhusu uvamizi wa kumuondoa madarakani rais Castro mwaka 1961 aliuawa, ambapo ajenti wa CIA alikuwa anatoa kalamu yenye sumu ilio na sindano kwa ajenti mmoja wa Cuba ili kumuua kiongozi huyo.

NYONGEZA 1

Nitaanzia mbali kidogo..

Baada ya fidel kutwaa madaraka kwa kumpindua Batista ndani ya siku 100 za mwanzo alifanya mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kutwaa baadhi ya mashamba ya miwa, kusogeza huduma za jamii karibu, kupiga marufuku ubaguzi wa rangi nk..

Nchi ya Cuba ilikuwa na idadi kikubwa ya watu ambao hawajasoma zaidi ya asilimia 60 ya watu wale walikuwa hawajui kusoma na kuandika, chini ya Castro akaanzisha utaratibu wa wale wachache wanaojua kusoma na kuandika wawafundishe wale wasiojua, wakasambaa kote nchini chini ya msemo maarufu wa 'kama hujui jifunze ujue na kama unajua fundisha'.

Kupitia mpango huo watu wengi wa Cuba wengi walijua kusoma na kuandika na elimu ilitolewa bure.

Pia nchi hiyo wakati wa Fidel anaingia madarakani ilkuwa na jumla ya madaktari 6000 tu na wengi walikuwa hapoHavana, kule vijijini huduma zilikuwa hakuna na watoto wengi walikufa kwa kukosa huduma. Castro akawaambia madaktari wale waliorundikana mjini wasambae mpaka vijijini wakatoe huduma. Wengi waligoma na kukimbia nchi, ndio chanzo cha wengi kwenda miami na pia watu wengi waliokuwa na uchumi mzuri ambao mali zao zilitaifishwa walimchukia Fidel na kuikimbia nchi, ndio hao walokuwa wakishangilia juzi.

Ili kuleta huduma za afya karibu Fidel alianzisha vyuo vitatu maalum kwa ajili ya kupambana na uhaba wa madaktari na alifanikiwa sana, vifo hasa vya watoto vilipungua sana kuliko baadhi ya miji huko USA wakati huo.

Maadui wa Castro waliongezeka toka nje na ndani ya nchi, CIA walitumia mbinu chafu za kumuondoa Fidel duniani na mipango mingi iliwahusisha wacuba wengi waliokimbia nchi hasa waliokuwa wakiishi Miami.

Sasa Fidel alipambana na mbinu hizo kwanza kitengo cha ujasusi kilikuwa chini yake, kiliitwa DGI(Director General of Intelligence) na kitengo hiki kilikuwa kama mali binafsi ya Fidel, wengi wa waliofundishwa walikuwa nI vijana wadogo hasa walioungana nae huko kwenye milima ya Ciera Maestra wakati wakipambana na Batista na vijana hawa walikusanywa na mama mmoja aliyekuwa karibu sana na Fidel, aliitwa Celia Sanches, huyu alikufa kwa Saratani mwaka 1980.

Vijana hawa asilimia 95 walifanya kazi ya kijasusi bure bila malipo na wakati mwingine walichukuliwa vijana wadogo sana na kupelekwa ""shambani""ambako walipewa elimu ya ujasusi wa hali ya juu sana, na pia walikuwa wazalendo sana kwa nchi yao na watiifu kwa Fidel.

Hakuna CIA officer aliyeingia Cuba bila kufahamika, mipango ya mauaji iliyopangwa na Fidel iligundulika haraka kwani Fidel alifanikiwa kupenyeza vijana wengi kwenda USA hasa Miami na Florida na huko waliishi wakifuatilia kila Wamarekani wanachokipanga juu ya Fidel na wengi wa vijana hawa bila CIA kufahamu kwamba ni majasusi waliwatrain tena ili kufanikisha mipango yao ya kumuua Fidel Castro, vijana hawa walibaki watiifu kwa Fidel na hivyo mipango yote waliyopanga ilimfikia el comandante Fidel Castro bila wasiwasi.

Baada ya John F. Kennedy kuwa Rais wa Marekani alimkabidhi ndugu yake aliyeitwa Robert Kennedy jukumu la kumuua Fidel Castro kwa kupitia Counter Intelligence na Double Agent.

Vijana wa Fidel waligundua njama hizo na zikafika mezani kwa el comandante Fidel Aljandro Castro luz.

Akihojiwa na mwandishi wa Reuters, Fidel alitahadharisha Marekani kwa kusema jaribio lolote la kumuua kiongozi wa Cuba litakuwa na madhara kwa Marekani na wasitishe mipango yao, Wamarekani walisikia lakini walikaidi na Robert Kennendy akaendelea na mipango ya kumuua Castro.

November 22 Lee Oswald alimpiga risasi Rais wa Marekani John F. Kennedy na baada ya saa moja ikatangazwa raisi ameuawa, inaaminika Castro alifahamu mipango hiyo japo alikanusha sana.

Nitarudi.

NYONGEZA 2


Baada Kennedy kuingia madarakani CIA walimwambia ni lazima Fidel aondolewe madarakani hii ni baada ya Fidel kutaifisha mali nyingi zilizokuwa zikimiliwa na Wamarekani na pia alianza kuagiza bidhaa toka Soviet.

Baada ya pressure kubwa toka kwa CIA, Rais kenedy akaidhinisha kuondolewa madarakani kwa Fidel Castro na katika mpango huo Kennedy alisema hataki ijulikane kuwa Marekani ndio imehusika na mpango huo kwa hiyo akawataka CIA wahakikishe wanakamilisha mpango huo bila kuacha alama ya mhusika mkuu.

CIA wakaanza mpango huo kwa kuwahusisha wacuba waliokimbia nchi hasa wale waliokuwa Miami, jumla yao ilikuwa 1400 na kikosi cha watu hao kikapewa jina la kikosi 2506, wakapelekwa eneo maalumu na kuanza kupewa mafunzo ya kwenda kumwondoa madarakani El commandante Fidel Castro.

Mazoezi ya anga, majini na ardhini yalifanyika katika kundi hilo la wakimbizi waliokuwa wakipewa mafunzo walikuwepo maagent wa Fidel waliokuwa wakipenyeza taarifa zao havana.

Mazoezi yalipokamilika zilipangwa hatua tatu za mashambulizi ambazo Rais Kennedy alizipitisha, njia ya kwanza ilikuwa ni kutumia ndege za kivita kuzipiga air base zote za Jeshi la Anga la Fidel, walitaka kushambulia na kuzimaliza ndege zote.

Njia ya pili ilikuwa ni kwenda kumalizia mabaki yoyote ya ndege ambayo haikulipuka kwenye mpango wa kwanza na njia ya tatu ilikuwa ni kuingia kwa hao wakimbizi wa Cuba waliopewa mafunzo kwenda kushambulia na kumwondoa Fidel madarakani.

Njia ya kwanza ikaanza kutumika, marubani wavamizi walipewa ndege, ndege zile za kivita zilibadilishwa rangi na kufanana sana na zile za Jeshi la Cuba na pia zilipakwa matope ili zikiwa angani zionekane ni chakavu, jamaa wakaenda wakashambulia kambi ya anga ya Fidel na waliangamiza asilimia 80 ya ndege za Castro, Jeshi la Anga la Castro lilibakiwa na ndege sita tu na marubani saba, ilikuwa big loss kwa comrade.

Baada ya njia ya kwanza kuleta matokea chanya kwa Wamarekani, huko New York kiongozi wa Cuba Umoja wa Mataifa akaitisha kikao, akaituhumu Marekani, Marekan ikakataa katakata kuhusika, wakadai ndege zilizoshambulia ni za Wacuba wenyewe walioasi Jeshi.

Balozi wa Cuba akasema ndege za Jeshi la Cuba sio zilizoshambulia, ndege zilizoshambulia zina mngurumo tofauti na ndege za Cuba, ndege zilizoshbulia ni za Marekani ila mmezibadilisha rangi zifanane na za Cuba ila mmeshindwa kubadili muungurumo.

Hapo rais Kennedy akaingiwa na ubaridi na akasitisha njia ya pili iliyokuwa imepangwa, Maafisa wa CIA walichukia sana kuona rais amekataa njia ya pili kutumika.

CIA wakaenda njia ya tatu ya kuwa deploy wale 1400 ili wavamie Cuba, kule Cuba Fidel mwenyewe aliingia front na kusema hii ni kazi ya Marekani na Cuba will respond in kind.

Baada ya kauli hiyo Fidel alizihamisha zile ndege sita zilizosalia na pia akaandaa mpango mkakati wa kujibu.

Wale wavamizi 1400 wa mara ya kwanza ilikuwa imepangwa waingie Cuba kupitia Trinidad lakini baada ya Kennedy kuigomea njia ya pili, Maafisa wa CIA nao wakabadili njia ya kuingia Cuba kwa hawa wavamizi, wakaelekezwa waingie cuba kupitia hapo the bay of pigs. Mahali hapo Fidel alipafahamu sana sana, lakini katika kujiandaa na adui mwonekano wa pwani ile ilibadilishwa kwa kiasi kikubwa, kiasi kwamba maadui walipokuwa wakija walishindwa kuona vizuri hasa ni wapi Majeshi ya Cuba yamejificha.

Meli zikiwa zimewabeba wavamizi zikafika Pwani ila Jeshi la Cuba likawa na taarifa. El Commandante Fidel akiwa mstari wa mbele kuendesha mapambano, wale wavamizi walishambuliwa sana na meli moja iliyobeba vifaa maalumu ilizamishwa na nyingine iliyowabeba hao wavamizi.

Walipigwa sana, zile ndege sita zilizosalia zikawa zinazunguka anga ya Cuba hasa hapo bay of pigs, wengi wa wavamizi waliuawa na wengine kuchukuliwa mateka. Taarifa zikafika Marekani juu ya hasara kubwa na kushindwa kwa zoezi hilo.

Rais Kennedy akatoa ndege sita za kijeshi kwenda kusaidia, hazikufua dafu kwani ndege nne zilidunguliwa na Jeshi la Cuba, ilikuwa loss kubwa kwa Marekani.

Mpango wa kumtoa madarakan Fidel ukafeli vibaya sana, hivyo ndivyo ilivyokuwa juu ya bay of pigs.


NYONGEZA 3

Na ukumbuke kuwa Jesuit Fathers ni shirika la Kipapa la Wamisionari maalumu kwa ajili ya Ulinzi wa kanisa.Hawa ndio majasusi wa kanisa katoliki.Ni shirika ambalo huchukua watu/Mapadre wenye IQ kubwa sana,ktk shirika hili,zaidi ya masomo ya kawaida ya Falsafa na Theolojia ambayo mapadre wote husoma,hawa Jesuit Fathers husoma masomo ya zaida ya "elimu dunia".Na huchukua hata miaka 20 kwa mtu kupewa upadre.

Mwalimu wa kwanza aliyemlea Fidel Castro na kumkuza alikuwa ni Padre wa Jesuit.Castro alisoma shule za Jesuit toka akiwa mtoto mdogo,kifupi Fidel Castro ni kijana wa Jesuit Fathers.Amesoma elimu ya awali mpaka chuo Kikuu kwa Jesuits Fathers na baadae akajiunga na chama cha Siasa cha "Orthodox or Christian Democrats Party" kilichokuwa na "msaada" wa Jesuits Fathers.

There is a very BIG CONNECTION btn Jesuits Fathers na aina ya maisha yake ya kijasusi na kuwakwepa US.Licha ya kuwa "Atheist Communits Party" ya Cuba haimini uwepo wa Mungu,lkn % kubwa ya watu wa CUBA ni wakatoliki na Kanisa liliwaruhusu kujiunga na chama hicho kisichotambua uwepo wa Mungu.

Safari ya pili ya Papa kuingia Havana ilikuwa ni Papa aliyetokana na Jesuits Fathers,na ujio wa Papa huyu ulikuwa ni utangulizi wa ufunguzi wa Ubalozi wa US pale Havana,na safari hii ya Papa kule Havana ilimchukua mpaka Florida na Washington DC ambapo alihutubia Congress na walifuatana na Raul Castro toka Cuba mpaka US,ambapo kukawa na mkutano kati ya Papa(Ambaye ametoka Jesuits Fathers,Obama na Raul).

Fidel Castro aliwahi kusema "The US will come to talk to us,when they will have black president and the Catholic Church have Pope from Latin America".Hii imetokea,ni wakati wa Obama ndipo Ubalozi wa US umefunguliwa Havana na siku kadhaa kabla ya kufunguliwa Papa Francis ambaye ni mkulia wa Argentina alitembelea Havana.Haya yalikuwa ni maneno ya "unabii" a Fidel Castro na muda mchache baada ya unabii huo kutimia,Fidel kaenda kupumzika.

Ni sahihi tukitafakari nukta hizi:

1) Cuba is overwhelmingly Roman Catholic.

2) Roman Catholics are allowed to join the atheist Communist Party.

3) Fidel Castro himself is a graduate of several Jesuit institutions, and
is in good standing with the Pope.

4) He was a member of the Roman Catholic Christian Democrat party before
starting his Marxist/Leninist revolution.

Albert Rivera, the former Jesuit priest who became a Protestant preacher,
said that Castro is a fourth-degree, professed Jesuit. The circumstantial
evidence strongly corroborates that statement.




a96ceb9f73069797766e86b8017cdf32.jpg
6fffb81d183eeb7a8bf8c35dcb4cb309.jpg


DOCUMENTARY: 638 Ways To Kill Castro

 
Na hatimaye amekufa kwa amri ya Mungu.
Wakati wa utoto tulisikia simulizi nyingi sana kumuhusu Castro,ikiwa ni pamoja na kusema huyu jamaa alikuwa akivaa shati lenye vifungo ambavyo akiviunganisha vinatengeneza bastora.

Marafiki zake kama Huggo Chavez,Che Guavara na kina Samora Machel waliuwawa na CIA.Chevez kafa "juzi" tu tukiwa wazee na familia...CIA walimpandikizia liugonjwa lililomuua,na mwaka mmoja kabla ya kifo chake wakampa taarifa kuwa washammaliza,ndio maana siku za mwisho za maisha yake,Chavez alikuwa anawatukana sana Wamarekani na hasa akipata nafasi ya kuhutubia UN..

Marekani sio mtu mzuri hata kidogo,juzi nikaona wale ambao wengi ni mashoga waliokimbilia MIAMI wakishangilia kifo,wakati wale wa CUBA wa kweli wakilia kwa uchungu.
 
Nitaanzia mbali kidogo..

Baada ya fidel kutwaa madaraka kwa kumpindua Batista ndani ya siku 100 za mwanzo alifanya mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kutwaa baadhi ya mashamba ya miwa, kusogeza huduma za jamii karibu, kupiga marufuku ubaguzi wa rangi nk..

Nchi ya Cuba ilikuwa na idadi kikubwa ya watu ambao hawajasoma zaidi ya asilimia 60 ya watu wale walikuwa hawajui kusoma na kuandika, chini ya Castro akaanzisha utaratibu wa wale wachache wanaojua kusoma na kuandika wawafundishe wale wasiojua, wakasambaa kote nchini chini ya msemo maarufu wa 'kama hujui jifunze ujue na kama unajua fundisha'.

Kupitia mpango huo watu wengi wa Cuba wengi walijua kusoma na kuandika na elimu ilitolewa bure.

Pia nchi hiyo wakati wa Fidel anaingia madarakani ilkuwa na jumla ya madaktari 6000 tu na wengi walikuwa hapoHavana, kule vijijini huduma zilikuwa hakuna na watoto wengi walikufa kwa kukosa huduma. Castro akawaambia madaktari wale waliorundikana mjini wasambae mpaka vijijini wakatoe huduma. Wengi waligoma na kukimbia nchi, ndio chanzo cha wengi kwenda miami na pia watu wengi waliokuwa na uchumi mzuri ambao mali zao zilitaifishwa walimchukia Fidel na kuikimbia nchi, ndio hao walokuwa wakishangilia juzi.

Ili kuleta huduma za afya karibu Fidel alianzisha vyuo vitatu maalum kwa ajili ya kupambana na uhaba wa madaktari na alifanikiwa sana, vifo hasa vya watoto vilipungua sana kuliko baadhi ya miji huko USA wakati huo.

Maadui wa Castro waliongezeka toka nje na ndani ya nchi, CIA walitumia mbinu chafu za kumuondoa Fidel duniani na mipango mingi iliwahusisha wacuba wengi waliokimbia nchi hasa waliokuwa wakiishi Miami.

Sasa Fidel alipambana na mbinu hizo kwanza kitengo cha ujasusi kilikuwa chini yake, kiliitwa DGI(Director General of Intelligence) na kitengo hiki kilikuwa kama mali binafsi ya Fidel, wengi wa waliofundishwa walikuwa nI vijana wadogo hasa walioungana nae huko kwenye milima ya Ciera Maestra wakati wakipambana na Batista na vijana hawa walikusanywa na mama mmoja aliyekuwa karibu sana na Fidel, aliitwa Celia Sanches, huyu alikufa kwa Saratani mwaka 1980.

Vijana hawa asilimia 95 walifanya kazi ya kijasusi bure bila malipo na wakati mwingine walichukuliwa vijana wadogo sana na kupelekwa ""shambani""ambako walipewa elimu ya ujasusi wa hali ya juu sana, na pia walikuwa wazalendo sana kwa nchi yao na watiifu kwa Fidel.

Hakuna CIA officer aliyeingia Cuba bila kufahamika, mipango ya mauaji iliyopangwa na Fidel iligundulika haraka kwani Fidel alifanikiwa kupenyeza vijana wengi kwenda USA hasa Miami na Florida na huko waliishi wakifuatilia kila Wamarekani wanachokipanga juu ya Fidel na wengi wa vijana hawa bila CIA kufahamu kwamba ni majasusi waliwatrain tena ili kufanikisha mipango yao ya kumuua Fidel Castro, vijana hawa walibaki watiifu kwa Fidel na hivyo mipango yote waliyopanga ilimfikia el comandante Fidel Castro bila wasiwasi.

Baada ya John F. Kennedy kuwa Rais wa Marekani alimkabidhi ndugu yake aliyeitwa Robert Kennedy jukumu la kumuua Fidel Castro kwa kupitia Counter Intelligence na Double Agent.

Vijana wa Fidel waligundua njama hizo na zikafika mezani kwa el comandante Fidel Aljandro Castro luz.

Akihojiwa na mwandishi wa Reuters, Fidel alitahadharisha Marekani kwa kusema jaribio lolote la kumuua kiongozi wa Cuba litakuwa na madhara kwa Marekani na wasitishe mipango yao, Wamarekani walisikia lakini walikaidi na Robert Kennendy akaendelea na mipango ya kumuua Castro.

November 22 Lee Oswald alimpiga risasi Rais wa Marekani John F. Kennedy na baada ya saa moja ikatangazwa raisi ameuawa, inaaminika Castro alifahamu mipango hiyo japo alikanusha sana.

Nitarudi.
 
El Comandante de'levis tunakusubiri

Japo sijui ni kweli Fidel alikuwa na taarifa za mipango ya kumuua Kennedy ,kuna aide wake Fiorentino Aspillaga wanasema huyu alikuwa kwenye jumba fulani la mawasiliano na alipewa kazi maalumu ya kufuatilia mawasiliano ya CIA na ile siku ya mauaji basi Fiorentino akapewa order asiendelee kufuatilia hayo mawasiliano ..na badala yake akusanye taarifa zozote kutoka Texas kumbuka Kennedy alipigwa risasi Dallas

Ingawa wakati Fidel anapewa taarifa za kupigwa risasi Kenedy wakati akiwa kwenye beach house yake wakila chakula cha mchana alijua kwa vyovyote lazima atahusishwa na mauaji ya Kennedy hivyo hakuwa na uoga wowote kwa sababu siku zote za maisha yake alikuwa kwenye hatari pamoja na hayo alipata hofu kwamba kumuua raisi wa Marekani sio jambo dogo ,Marekani inagusa karibia dunia nzima hivyo kupotelewa kwa raisi sio tu kutaathiri Cuba bali dunia nzima

Ila pia wanahisi Castro alihusika kwa sababu huyu Oswald aliyempiga risasi Kennedy kuna wakati aliomba visa ya kwenda Cuba kwenye embassy yao iliyopo Mexico akanyimwa visa basi kwa hasira akaropoka atampiga Kennedy risasi ...na inaaminika ubalozi huo wa Mexico ulikuwa center ya ujasusi ya Cuba hivyo chochote kinachofanyika pale Castro lazima anajua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom