Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Wawakilishi wa kanisa la kiinjili la kilutheri la nchini Marekani wakipiga kura kuruhusu wasagaji na mashoga kuwa wachungaji na viongozi wa kanisa
Kanisa la kiinjili la kilutheri la Marekani limepiga kura na kuruhusu wasagaji na mashoga kuwa wachungaji na viongozi wa makanisa ya kilutheri nchini humo. Uamuzi huo wa kuwaruhusu mashoga na wasagaji kuwa wachungaji na viongozi wa makanisa ya kilutheri nchini Marekani unaonekana kuzusha mzozo na unaweza kuwagawanya wanachama wake milioni 4.6 waliopo nchini humo.
Kanisa la kiinjili la kilutheri la Marekani (ELCA) ambalo lina dayosisi zipatazo 10,000 nchini Marekani, lilipiga kura ijumaa jioni kubadilisha baadhi ya vipengele na kuwaruhusu mashoga na wasagaji kuwa wachungaji na pia kuwapa nafasi za kuwa na vyeo mbali mbali kwenye makanisa.
Baada ya majadiliano makali, wawakilishi wa kanisa walipiga kura 559 za kuunga mkono kulinganisha na kura 451 zilizokuwa zikipinga wazo hilo, alisema mkurugenzi wa habari wa kanisa hilo John Brook.
Kanisa la kiinjili la kilutheri la Marekani sio la kwanza nchini Marekani kutoa uamuzi huo wa kuwapa mashoga na wasagaji nafasi za uchungaji na uongozi katika makanisa. Kanisa la Episcopalian la nchini Marekani lilishawahi kutoa uamuzi kama huo.
Hata hivyo uamuzi huo wa kanisa la kilutheri la Marekani haukupita kirahisi, kwani kulikuwa na upinzani mkali kutoka kwa wachungaji mbali mbali akiwemo mchungaji Richard Mahan wa dayosisi ya Maryland magharibi, Virginia.
"Siwezi kuamini kanisa ambalo nimelijua kwa zaidi ya miaka 40 linaweza kuruhusu vitu ambavyo mungu alivipinga" alisema mchungaji Mahan na kuongeza "Hakuna sehemu yoyote katika maandishi ambayo inasema watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja au watu wanaofunga ndoa za jinsia moja wanakubalika mbele ya mungu".
Kwa upande wa watetezi wa uamuzi huo akiwemo askofu Gary Wollersheim wa dayosisi ya Illinois kaskazini walisema kwamba uamuzi huo ni sahihi.
"Ni uamuzi wa kutoa haki kwa wote, ni uamuzi ambao yesu angetutaka tuuchukue" alisema askofu Wollersheim
Source: nifahamishe.com