Taifa_Kwanza
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 443
- 86
Mashirika haya NSSF, PPF, PSPF na mengine yenye muundo kama huo yanatakiwa kulindwa kwa nguvu zote hata kama ni kwa maandamano kuanzia sasa ili kuepusha ukwapuaji wa pesa ambao uko mbioni kufanywa na Serikali pamoja na CCM.
Baada ya ukosefu wa pesa serikalini kutokana na uongozi mbovu na matumizi ya kijinga sasa serikali na CCM wanatafuta pesa popote pale zilipo harari ama haramu. vyombo hivi viwili kama kawaida yao na hasa kama vilivyolifirisi shirika la Bima la Taifa (NIC), na kukwapua Mapesa kutoka BOT apo nyuma na kwa sababu hawawezi kurudi uko na kufanya ushenzi wao sasa wanayatolea macho mashirika haya ya hifadhi za jamii.
Hizi kauli za Jakaya za kutaka kulipa wazee wa Africa Mashariki na nyingine nyingi za kimatumizi zitakazoanza kutolewa hivi punde na hasa baada ya kuanza kuisonta CHADEMA juu ya vyanzo vya mapato yake na kwa sababu watanzania wanatabia ya kushangilia mambo ambayo kwa juu yamepakwa rangi nzuri za kizalendo, utu, maendeleo na uungwana ni utangulizi tu wa ukwapuzi wa mapesa kutoka kwenye taasisi hizi.
Na zaidi, msukumo wa ukwapuzi huu ni sababu zote walizonazo CCM na serikali katika kujisafisha mbele ya watanzania kutoka kwenye aibu ya kushindwa kusimamia hali tete ya uchumi wa watanzania kwa kadri ambayo CHADEMA wamedhamiria kuwavua nguo, na hasa uoga wa kufukuzwa kazi na UMA.
Sasa, kwa sababu wakati wanaanza kufanya ivyo mamalaka zilizopewa fursa ya kuzisimamia hazitakuwa na uwezo wa kukataa uso kwa uso kama ilivyokawaida. Chonde chonde watanzania tuwe nyuma yao na kupinga ukwapuaji huu ambao ndio unaweza kuwa wa kutumaliza kabisa watanzania.
TUYALINDE MASHIRIKA YETU YA HIFADHI YA JAMII DHIDI YA UFISADI KWA NGUVU ZETU ZOTE.
Baada ya ukosefu wa pesa serikalini kutokana na uongozi mbovu na matumizi ya kijinga sasa serikali na CCM wanatafuta pesa popote pale zilipo harari ama haramu. vyombo hivi viwili kama kawaida yao na hasa kama vilivyolifirisi shirika la Bima la Taifa (NIC), na kukwapua Mapesa kutoka BOT apo nyuma na kwa sababu hawawezi kurudi uko na kufanya ushenzi wao sasa wanayatolea macho mashirika haya ya hifadhi za jamii.
Hizi kauli za Jakaya za kutaka kulipa wazee wa Africa Mashariki na nyingine nyingi za kimatumizi zitakazoanza kutolewa hivi punde na hasa baada ya kuanza kuisonta CHADEMA juu ya vyanzo vya mapato yake na kwa sababu watanzania wanatabia ya kushangilia mambo ambayo kwa juu yamepakwa rangi nzuri za kizalendo, utu, maendeleo na uungwana ni utangulizi tu wa ukwapuzi wa mapesa kutoka kwenye taasisi hizi.
Na zaidi, msukumo wa ukwapuzi huu ni sababu zote walizonazo CCM na serikali katika kujisafisha mbele ya watanzania kutoka kwenye aibu ya kushindwa kusimamia hali tete ya uchumi wa watanzania kwa kadri ambayo CHADEMA wamedhamiria kuwavua nguo, na hasa uoga wa kufukuzwa kazi na UMA.
Sasa, kwa sababu wakati wanaanza kufanya ivyo mamalaka zilizopewa fursa ya kuzisimamia hazitakuwa na uwezo wa kukataa uso kwa uso kama ilivyokawaida. Chonde chonde watanzania tuwe nyuma yao na kupinga ukwapuaji huu ambao ndio unaweza kuwa wa kutumaliza kabisa watanzania.
TUYALINDE MASHIRIKA YETU YA HIFADHI YA JAMII DHIDI YA UFISADI KWA NGUVU ZETU ZOTE.