Bei ya sido ni 1.5m na ya nje 2.5m
Wana JF naomba msaada wenu. Ninahitaji kununua mashine ya kukamulia mafuta ya alizeti. Ningependa kujua ni wapi naweza kupata mashine hiyo, pamoja na bei yake. Ninaishi Morogoro.
Natanguliza shukurani.
Mkuu hapo kwenye bei nadhan wadau wameshakusaidia, hivyo nitakaa kimya. Lakini ninakushauri katika mahesabu yako uongeze na gharama ya PURIFIER, kwan bila kufanya hivyo mafuta hayatakuwa na ubora unaostahiliWana JF naomba msaada wenu. Ninahitaji kununua mashine ya kukamulia mafuta ya alizeti. Ningependa kujua ni wapi naweza kupata mashine hiyo, pamoja na bei yake. Ninaishi Morogoro.
Natanguliza shukurani.
Mkuu kama walivyo kuambia, ila kwenye hizi mashine kuna Tatizo moja.
1. Mashine nyingi zinazo zalishwa Tanzania ni nzuri kwa uimara ila kwenye kukamua mafuta hazina uwezo wa kukamua kwa 100% zinakamua 50% hadi 70% yaani hazimalizi mafuta kwenye alizeti
2. Mashine za India ndo inasemekana zina presing kubwa ya angalau kukamua kwa 90% hadi 100%
NDO MAANA VIWANDA VYOTE ZAIDI YA 50 VYA KUKAMUA MAFUTA BABATI HAKUNA KINACHO KAMUA KWA 100% NA YALE MASHUDU HUWA YANANUNULIWA NA MHINDI MMOJA ANAITWA MOUNT MERU HUYU HUKAMUA KWA MARA YA PILI YALE MASHUDU NA KUPATA MAFUTA, YEYE ANA MASHINE ZA KUKAMUA KWA 100%
Mkuu hapo kwenye bei nadhan wadau wameshakusaidia, hivyo nitakaa kimya. Lakini ninakushauri katika mahesabu yako uongeze na gharama ya PURIFIER, kwan bila kufanya hivyo mafuta hayatakuwa na ubora unaostahili
mkuu asante sana kwa elimu ya mashine nilikuwa sijalifahamu hilo, mimi ninafahamu zile machine za mkono zinazofanana na za kubangua karanga na mbaya zaidi unapokwenda kununua machine label zake huwa hazioneshi efficiency ya ukamuaji. Hizo machine za india bei yake roughly inafika ngapi?