Mashindano ya U-miss TZ!

Moja ya mada nzuri za kujadili na kuzitolea maoni ni kama hii.Kiukweli mzee washiriki wote ni wana dini zao,siku hizi kila mtu ana dini yake.Sipaswi kuwalaum sana washiriki pengine hawajafikishiwa vizuri ubaya wa jambo lenyewe na viongozi wao wa dini.Kwa upande 1 mimi naweza kuwalaumu hata viongozi wa dini,wamebeba majukumu yasiyo yakwao zaidi na kusahau majukumu hasa ya kwao.We angalia kama kina Mufti simba anagombania wadhifa wakutangaza mwezi jambo dogo tu la kurekebisha wameshupaa kweli,wakati watoto wa kiislam wengi wanashiriki na hafanyi jitihada yoyote kuwanusuru.Waangalie kina Kadinal Pengo kila mara wanailaum serikali,nchi inakwenda pabaya sijui kuna hili na lile wakati watoto wa kikristo wengi wanashiriki wala hawafanyi jitihada zozote kunusuru janga hili.Hayo ni maoni wangu kwa hili.
 
Ni kweli bwana bajabiri na uyasemayo, hasa kwa watoto wa kike kutaka kuendesha gari, kupata vihela labda vya kuanzisha biashara na kujikomboa. Lakini kwa makampuni kuwatumia mabinti zetu namna hii ni hatari sana. Mabinti zetu itakua rahisi kwao kufikiria kuwa haya mashindano ndio yatakayowatoa kwenye umaskini, si kweli, zaidi ya kuwaletea madhara.<br />
Hatukatai kwa makampuni haya kutumia wanawake au wanaume, swala wanawatumia kwa njia zipi, kwanini wasi promote nembo na biashara zao kwa njia zilizotajwa nami na wadau wengine hapo juu?<br />
<br />
<b>Na hili swala la makelele mtaani ya promotions zao, litabidi nalo likomeshwe pia<br />
</b>
<br />
<br />
Hakuna faida wanazoPata! Ninaowafaham wote wana mitazamo ya kuwapata wanaume wenye vipato vizuri ili wawe karibu yao kimahusiano ili watimize malengo. Na huwapata kisha hutelekezwa! Sasa hayo si maadili mema kwa mabinti zetu.
Waamin wanatazamwa na kupata umaaruf kwenye hayo mashindano hivyo kupata matumain ya kutoka kwenye
 
Kila kukicha tunasikia na kuona mashindano ya u-miss, ina maana TZ kwa sasa haina njia nyingine ya kusaidia watoto wake wa kike zaidi ya kuwatembeza na kuwavalisha vichupi hadharani?
Kwani Voda, Airtel na TBL hawana mashindano mengine ya kusaidia watoto wa kike, kama ya business plan, kufanya vizuri O'level, A' level, vyuoni au kuwapa tuzo wale wanaosaidia jamii?
Wadau mnasemaje?

ukisema TANZANIA unawajumuisha na wazanzibar!.... ZNZ haina mashindano ya u miss.... ni sisi watanganyika na akili zetu za kuiga mambo ya kipumbavu ... na kuacha mambo mazuri...

Zanzibar ikijitenga itabidi nibadili uraia... tanganyika sio nchi ya kukuza mtoto akue na maadali mazuri..
 
Nilifurahishwa sana na mzee wa Kisomali aliyeenda kumtoa mwanae kwa fimbo katika haya mashindano ya utumwa, nadhani ilikuwa mwaka jana au juzi, sikumbuki. Huyo Msomali ni mfano wa kuigwa. Nasikia aliingia na bakora na akasema ataenizuwia ni mimi na yeye.
, ama zangu ama zake hapahapa, lakini kama huyu mtoto nimemzaa mimi ataondoka humu. Na kweli aliondoka nae kwa mikwaju.

Wazazi wengine wanashangilia. Kuna siku niliudhika sana niliona kwenye TV kuna shule katika sherehe zao ati wanawafanyisha watoto wadogo (walikuwa miaka 5 hadi 13 kama sikosei). Mashindano ya u miss? u miss? wa na miss nini zaidi ya maadili na waalimu na wazazi wanashadidia? Nikasema kuna siku ntakwenda kumuona Mwalim Mkuu wa hiyo shule niongee nane kiutu uzima. Mungu hajanipa uwezo huo lakini InshaAllah kuna siku ntakwenda.
 
<br />
<br />
Hakuna faida wanazoPata! Ninaowafaham wote wana mitazamo ya kuwapata wanaume wenye vipato vizuri ili wawe karibu yao kimahusiano ili watimize malengo. Na huwapata kisha hutelekezwa! Sasa hayo si maadili mema kwa mabinti zetu.
Waamin wanatazamwa na kupata umaaruf kwenye hayo mashindano hivyo kupata matumain ya kutoka kwenye

Maskini za mungu hawajui kuwa wanaume huwa wanawachukua kwa uchu wao wa mara moja tu. Lakini wanapotaka wanawake haswa wa kuwaoa basi hao wanaume ndio kwanza huchagua mwanamke wanaeona kuwa huyu anajisitiri na mwenye heshima na hajiachii hovyo.
 
<b><a href="https://www.jamiiforums.com/members/jebs2002.html" target="_blank"><b>jebs2002</b></a>,<br />
<br />
Ama kwa hakika hii ni moja katika mada nzuri sana nilizopata kuziona humu JF, nakupa pongezi kwa hilo.<br />
<br />
Watoto wa kike wa Kitanzania, Waislaam kwa Wakristo, walio na dini na wasio na dini. Wanatembezwa nusu uchi wakionesha uzuri na haiba zao kwa maslahi ya wengine. Kama si utumwa ni nini?<br />
<br />
Ukitazama hayo makampuni yanayo dhamini hayana zaidi ila ni kuhakikisha wanatangaza biashara zao kupitia watoto zetu wakike, wakipita kuonyesha maungo yao na jinsi walivyoumbika. Jee, kama huu si utumwa ni nini?<br />
<br />
Tunaiga mambo ambayo si mila wala desturi za Kitanzania wala za Kikristo wala za Kiislam ni za kishetani. Hao watoto maskini ya mungu utakuta wana support yote kutoka kwa wazee wao. Jee, ni tamaa ya maisha, ulimbukeni au ni ujuha? unaowapelekea wazee wa hawa watoto kuona kuwa wanafanya cha maana wanapofikia kuwauza watoto zao kwa njia hii?<br />
<br />
Halafu wengine utaona wakishindwa hujiliza kwa uchungu wa kukosa. Na wanaoshinda utaona eti wanajiliza kwa furaha! Ni nini wanacholilia? kukosa fedha za ushindi au furaha ya kuwa sasa watakwenda kuanikwa zaidi?<br />
<br />
Halafu kinachokera zaidi ni pale vyombo vya habari vinapowafanya hawa kuwa ni mabalozi wa mambo mema na kuwapeleka sehemu za kulelea watoto wadogo ili wawe mfano bora na waige dada zao wanafanya nini.<br />
<br />
Hii ni laana na ushetani na siungi mkono hata kidogo. Ndio hayo, leo mwanao anapita nusu uchi anajianika wewe mzee wake unashangilia. Khaaa.<br />
</b>


Mwenye kusimamia na kuratibu hayo mashindano ni dini gani?
 
Cha kushangaza sana,eti mratibu wa mashindano haya ni AL-HAJJ,anaitwa al-hajj Hashim Lundenga.Mufti Simba anamwangalia al-hajj huyu na wala hajawahi kumuita Bakwata japo kuja kumpa nasaha njema tu sisemi kumuadhibu,lakini akiwahiwa kutangaza mwezi na wenzake ugomvi mkubwa kweli mpaka anakusanya waandishi wa habari na TBC anafika kuwaeleza kuwa yeye peke yake ndio mwenye mamlaka ya kutangaza mwezi.Haya ya Lundenga alhaji kaziba macho na masikio kana kwamba hayamuhusu.
 


ukisema TANZANIA unawajumuisha na wazanzibar!.... ZNZ haina mashindano ya u miss.... ni sisi watanganyika na akili zetu za kuiga mambo ya kipumbavu ... na kuacha mambo mazuri...

Zanzibar ikijitenga itabidi nibadili uraia... tanganyika sio nchi ya kukuza mtoto akue na maadali mazuri..

You'll do us a favor...why not doing it now?
 
<b><a href="https://www.jamiiforums.com/members/jebs2002.html" target="_blank"><b>jebs2002</b></a>,<br />
<br />
Ama kwa hakika hii ni moja katika mada nzuri sana nilizopata kuziona humu JF, nakupa pongezi kwa hilo.<br />
<br />
Watoto wa kike wa Kitanzania, Waislaam kwa Wakristo, walio na dini na wasio na dini. Wanatembezwa nusu uchi wakionesha uzuri na haiba zao kwa maslahi ya wengine. Kama si utumwa ni nini?<br />
<br />
Ukitazama hayo makampuni yanayo dhamini hayana zaidi ila ni kuhakikisha wanatangaza biashara zao kupitia watoto zetu wakike, wakipita kuonyesha maungo yao na jinsi walivyoumbika. Jee, kama huu si utumwa ni nini?<br />
<br />
Tunaiga mambo ambayo si mila wala desturi za Kitanzania wala za Kikristo wala za Kiislam ni za kishetani. Hao watoto maskini ya mungu utakuta wana support yote kutoka kwa wazee wao. Jee, ni tamaa ya maisha, ulimbukeni au ni ujuha? unaowapelekea wazee wa hawa watoto kuona kuwa wanafanya cha maana wanapofikia kuwauza watoto zao kwa njia hii?<br />
<br />
Halafu wengine utaona wakishindwa hujiliza kwa uchungu wa kukosa. Na wanaoshinda utaona eti wanajiliza kwa furaha! Ni nini wanacholilia? kukosa fedha za ushindi au furaha ya kuwa sasa watakwenda kuanikwa zaidi?<br />
<br />
Halafu kinachokera zaidi ni pale vyombo vya habari vinapowafanya hawa kuwa ni mabalozi wa mambo mema na kuwapeleka sehemu za kulelea watoto wadogo ili wawe mfano bora na waige dada zao wanafanya nini.<br />
<br />
Hii ni laana na ushetani na siungi mkono hata kidogo. Ndio hayo, leo mwanao anapita nusu uchi anajianika wewe mzee wake unashangilia. Khaaa.<br />
</b>
<br />
<br />
FF usilie sana. Hii ni sehemu ya ajira milioni kadhaa ambazo mkuu aliahidi kuzitengeneza kila mwaka. Hongera Luteni Kanali Dokta Alhaji JK ongeza mashindano mengine zaidi kupromoti ajira
 
You'll do us a favor...why not doing it now?

Dude .. who are u ..?! btw Tanga yetu pia ilikuwa part ya sultan wa zanzibar wakijitenga tutahitaji tujiunge kule pamoja na mombasa ambao wameanza mchakato ... watu wa bara tuwachie na ustaarabu wenu ... pombe.. uzinzi.. kutembea uchi ..
 
Dude .. who are u ..?! btw Tanga yetu pia ilikuwa part ya sultan wa zanzibar wakijitenga tutahitaji tujiunge kule pamoja na mombasa ambao wameanza mchakato ... watu wa bara tuwachie na ustaarabu wenu ... pombe.. uzinzi.. kutembea uchi ..

Sasa naona tunapoteza mada, ilikua kuchanganua, kueleza experience yako kwenye mambo haya, ila sio kuanza kuukashifu muungano, wala watanganyika au wazanzibari, hakuna dini ambayo ni nzuri kuliko nyingine duniani, hio ni imani, na kila mtu ana yake kama alivyosema Vasco Da Gama! Nchi haina dini, ila watu ndio wenye dini.
Kusema usultani ulikua na mema kuliko na uongozi wa sasa utakua unawatukana na kuwadharau waliotuondoa kwenye ukoloni na utumwa wa wazungu na waarabu.
Swala ni makampuni yatumie vipi uwezo wao kuwasaidia watoto wetu wa kike zaidi ya kuwaburuza kwenye mashindano ya u-miss?
 
kwa kweli inashangaza sana, watanzania inabidi tuache ulimbukeni, mawazo ya kitumwa na tuanze kujiamini na kuendesha maisha yetu kulingana na maadili ya kitanzania.

Hivi sasa kwa mfano, kuna mashindano ya riadha ya dunia, mabinti kutoka kenya na hata botswana wameshinda gold medals, sisi wakwetu wanaonyesha mapaja na visaburi vyao kwa walafi. Jamani wabongo inabidi tuamke usingizini, tumelala muda mrefu sasa.
 
According to past JF threads nimeshindwa kuiweka hapa...Gazeti la dailynews la tr 11 June liliripoti TZ imeridhia kupeleka wasichana 40 kwenye Reed dance...

TAMWA walikemea, september ndio mwezi wa Reed dance ama ni lini na sie tuembrace tradition hiyo??? Ya mabinti vigoli kucheza nusu uchi kufurahisha wanaume, si heri hata umiss!!...
 
Binti yako akiingia tu kwenye mambo ya U-miss ujue umempoteza! Lazima tu atakuwa chakula cha wapenda ngono wa mjini, kwanza ujue hakuna miss mwenye heshima na uwezi kushinda U-miss mpaka utoe rushwa ya ngono kwa kamati ya miss Tanzania huo ndio utaratibu waliojiwekea baada ya hapo wanaanza kuwauza kwa mabosi.
Mimi nilikukuwa namuona jamaa yangu mmoja alikuwa aniletewa pale Protea Hotel, kuna siku aliletewa tumiss tuwili tunachecheka tu
 
hao wanaoendesha hao mashindano wanajiosevia hao mabinti, so mashindano ni chambo chao tu
 
<br />
<br />
FF usilie sana. Hii ni sehemu ya ajira milioni kadhaa ambazo mkuu aliahidi kuzitengeneza kila mwaka. Hongera Luteni Kanali Dokta Alhaji JK ongeza mashindano mengine zaidi kupromoti ajira

Tafadhali. Haya mashindano JMK kayakuta. Mbona unataka kutuingizia siasa kwenye hili jambo ambalo kila mmoja wetu linamuathiri, awe CCM awe CUF awe NCCR awe CDM awe Mkristo awe Muislaam awe Hana Dini. Jifunze mfano kutoka kwa bunge lililoisha, kwenye uzalendo waliungana wote na kuwa kitu kimoja kwa maslahi ya Taifa.

Kumbuka hawa vijana tunaowajenga leo ndio watakuwa mhimili wa Taifa hili kesho. Na tunapenda vizazi vyetu vikute Taifa lenye maadili mema zaidi kuliko maadili mabovu.

Sifa ya wazazi ni ulezi na si kuzaa.
 
According to past JF threads nimeshindwa kuiweka hapa...Gazeti la dailynews la tr 11 June liliripoti TZ imeridhia kupeleka wasichana 40 kwenye Reed dance...

TAMWA walikemea, september ndio mwezi wa Reed dance ama ni lini na sie tuembrace tradition hiyo??? Ya mabinti vigoli kucheza nusu uchi kufurahisha wanaume, si heri hata umiss!!...

Hakuna heri mama, "mtoto umleavyo ndivyo akuavyo" na "ukitaka kumkunja samaki awe mbichi, ukimwacha akavunda atakupatisha taabu".

Hayo ya kuwapeleka mabinti huko ni mwanzo tunae binti wa Kitanzania kajianika huko Play boy, uchi wa mnyama na tunamuona yule ni star.

Kwa mwenendo huu, sasa hivi tutaona mapicha ya ngono za Kitanzania yakiuzwa wazi wazi na kupewa baraka na wizara ya utamaduni na kwenda kuzinduliwa na huyo aliyeridhia kuwapeleka mabinti wetu wakaanikwe nusu uchi. Ndio tuna promote biashara za kuuza binaadam, halafu tunajidai hakuna utumwa!
 
Hakuna heri mama, &quot;mtoto umleavyo ndivyo akuavyo&quot; na &quot;ukitaka kumkunja samaki awe mbichi, ukimwacha akavunda atakupatisha taabu&quot;.<br />
<br />
Hayo ya kuwapeleka mabinti huko ni mwanzo tunae binti wa Kitanzania kajianika huko Play boy, uchi wa mnyama na tunamuona yule ni star.<br />
<br />
Kwa mwenendo huu, sasa hivi tutaona mapicha ya ngono za Kitanzania yakiuzwa wazi wazi na kupewa baraka na wizara ya utamaduni na kwenda kuzinduliwa na huyo aliyeridhia kuwapeleka mabinti wetu wakaanikwe nusu uchi. Ndio tuna promote biashara za kuuza binaadam, halafu tunajidai hakuna utumwa!
<br />
<br />
Halafu nikiwaza nina mabinti tupu sijui jamani hii dunia na utandawazi utatupeleka wapi

Juzi nilialikwa iftaar movenpick na kula na warembo wa vodacom miss TZ vibinti vyembamba vinaogopa hata kuchota chakula na kuishia fruits na juice tu...maongezi so artificial wote wanataka wamfurahishe uncle ....I felt sorry on their behalf
 
Back
Top Bottom