Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 58,781
- 78,451
Hivi wajameni yale mashindano ya SHIMIWI yanayotumia fedha nyingi kusafirisha timu toka wizara usika kwenda kushiriki michezo mikoa mingine yana faida gani? Naomba kujua maana naona kama ni njia fulani ya ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za taifa ukizingatia zinadaiwa kuwa finyu. Ni kwanini basi rasilimali hizo zisielekezwe katika kutengeneza ajira kwa vijana kwa kuwaaandaa wale wa mashuleni na mitaani wakiwa wadogo na kutoa fursa ya uwezekano wa kupata ajira hapo baadae ukizingatia kimichezo tupo nyuma sana! kwanini rasilimali hizo zisitumike kutengeneza kambi ya wanariadha au mchezo wa soka au basketiball au hata hata netball?
Hivi Pinda anafikiri haya kweli au ndo ile dhana ya kuwa unakula kwa urefu wa kamba yako yaani yule aliyekaribu na hazina hukarimiwa zaidi? Kwangu mimi binafsi sioni faida ya kumkirimu wazee wetu katika wizara wakati wanaweza kufanya michezo bila ya kuingia katika matumizi mabaya ya fedha zinazosemekana ni kidogo na bila ya kuwa na matarajio yeyote kutokana na michezo hiyo yaani kama kutengeneza ajira.
Hivi Pinda anafikiri haya kweli au ndo ile dhana ya kuwa unakula kwa urefu wa kamba yako yaani yule aliyekaribu na hazina hukarimiwa zaidi? Kwangu mimi binafsi sioni faida ya kumkirimu wazee wetu katika wizara wakati wanaweza kufanya michezo bila ya kuingia katika matumizi mabaya ya fedha zinazosemekana ni kidogo na bila ya kuwa na matarajio yeyote kutokana na michezo hiyo yaani kama kutengeneza ajira.