Mutwale
Member
- Oct 20, 2010
- 67
- 19
Ukipita Barabara ya Uhuru ambayo hapo awali ilitumika kupitisha viongozi wakitafa, nakumbuka Mzee Mandela, Walter Sisulu, Papa John Paul(Mwenyeheri) na wengine wengine wengi; utakutana na mahandaki kuanzia Buguruni pale Kiomboi Kisiriri, polisi, Rozana ndo balaa maana kuna mshimo wa kina kirefu kwani pia umejaa maji! Malapa, Bungoni, kisha Kariakoo Shule ya Uhuru karibu na Round about ya Msimbazi rd., Kisha kwenye mataa ya makutano ya Uhuru na Bibi Titi! Shimo lingine liko pale Mtaa wa Jamuhuri na Azikiwe, mbele kabisa ya NMB House, pembeni mwa Benjamini Mkapa Tower! Mashimo yote haya yako katika kati ya Jiji la Dar es Salaam, aibu iliyoje?
Je manispaa zinazo husika hazioni uozo huu? na kama barabara za katikati ya Jiji, (Tanzania) je barabara za Kisukuru, Mwitongo, Rubya, Litumbadyosi, Kiwele, au Kifyulilo ambazo hazionekani mbele ya macho ya watawala atazijenga nani!
Je ile kodi ya Road License inakwenda wapi? je kuna sababu gani ya kulipa Road License na ilihali asilimia 95 linapopita gari lenye stika hiyo ni mashimo matupu?
Chonde chonde wanasi hasa, acheni longo longo, za kujivua Magamba fanyeni kazi, kujivua gamba kwa ukweli ni kutumia kodi zetu kwa malengo kusudiwa na si kuzunguka nchi na kujitambulisha, kwani hakutatusaidia.
Ingefaa misafara ya rais irejeshwe tena kupitia barabara ya uhuru! pengine itasaidia, pia Rais anapowaambia watendaji wake watoke maofisini, ingefaa naye siku moja afanye ziara ya ghafla maeneo ya mitaa ya Sinza kwa wajanja na viunga vyake ajionee, hapo atajua kama kweli wamejivua gamba, au wanapaswa kujiua gamba! watanzania wa leo tumechoka siasa, kwani hazitusaidii bali walio karibu na hao wakuu wa Kaya.
Mungu ibariki Tanzania.
Je manispaa zinazo husika hazioni uozo huu? na kama barabara za katikati ya Jiji, (Tanzania) je barabara za Kisukuru, Mwitongo, Rubya, Litumbadyosi, Kiwele, au Kifyulilo ambazo hazionekani mbele ya macho ya watawala atazijenga nani!
Je ile kodi ya Road License inakwenda wapi? je kuna sababu gani ya kulipa Road License na ilihali asilimia 95 linapopita gari lenye stika hiyo ni mashimo matupu?
Chonde chonde wanasi hasa, acheni longo longo, za kujivua Magamba fanyeni kazi, kujivua gamba kwa ukweli ni kutumia kodi zetu kwa malengo kusudiwa na si kuzunguka nchi na kujitambulisha, kwani hakutatusaidia.
Ingefaa misafara ya rais irejeshwe tena kupitia barabara ya uhuru! pengine itasaidia, pia Rais anapowaambia watendaji wake watoke maofisini, ingefaa naye siku moja afanye ziara ya ghafla maeneo ya mitaa ya Sinza kwa wajanja na viunga vyake ajionee, hapo atajua kama kweli wamejivua gamba, au wanapaswa kujiua gamba! watanzania wa leo tumechoka siasa, kwani hazitusaidii bali walio karibu na hao wakuu wa Kaya.
Mungu ibariki Tanzania.