Mashahidi wa yehova-changamoto iliyofichika kwa wahudumu wa afya

Jackbauer

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,038
2,199
Mashahidi wa yehova(jehova's witnesses) ni kundi la kiimani kama yalivyo makundi mengine mfano waislamu, wakatoliki na waprotestanti.kundi hili ni maarufu katika suala la uongezwaji damu.kwa shahidi wa yehova,kuongezewa damu ni dhambi na hairuhusiwi(blood transfusion is prohibited among jehova witness members)

Hii ni imani kama zilivyo imani nyingine na kwa maoni yangu yafaa iheshimiwe. Hivi majuzi nilikuwa katika kituo kimoja cha afya(health facility) ambacho sitakitaja jina na kushuhudia mzozo mkali kati ya wahudumu wa afya daktari, nesi na mtoa dawa ya nusu kaputi wote hawa wakijaribu kumshawishi mama mjamzito kwamba kwa hali aliyonayo na kwa usalama wa maisha yake angehitajika kuongezewa damu wakati au mara baada ya operesheni ya kutoa mtoto. Mama huyu alikuwa shahidi wa yehova na alikataa kabisa na hatimaye alisaini maelezo nanukuu "ikitokea hali yoyote hata kama napoteza maisha nisiongezewe damu" hatimaye mama huyu aliingizwa kwenye chumba cha upasuaji na kufanikiwa kupata mtoto na yeye kutoka mzima ingawa hali yake ilikuwa si ya kuridhisha.

Hili jambo laweza kuonekana rahisi kuelezea lakini ni gumu kiutendaji kwani mama mjamzito anapofariki maelezo ya kifo chake lazima yafike wizara husika pia kwa namna moja au nyingine mhudumu wa afya huwajibishwa. Kwa upande mwingine mhudumu wa afya anaweza kushtakiwa iwapo ataenda kinyume na matakwa ya mteja(mgonjwa).

Kazi kwenu wanaJF mnaionaje imani hii haswa kwa mazingira yetu ya Tanzania? Nini kifanyike kuokoa maisha ya watu hawa?

Nawasilisha...
 
Kama mgonjwa ana akili timamu, yeye ndiye atakuwa na uamuzi wa mwisho na akishasaini kama alivyofanya mgonjwa tajwa hapo juu, mhudumu wa afya hana kosa, kifupi twasema "his/her ass is covered" - akishtakiwa likely atashinda.
 
Ni muhimu kwa serikali kuweka muongozo wa jinsi ya ku-handle wagonjwa wa namna hii, vifo vya kinamama vitapungua kweli iwapo kuna misimamo tete kama hii?
 
Kama ni life saving mtu awekewe damu kilazima akipona atubu dhambi zake!
 
kama mgonjwa ana akili timamu, yeye ndiye atakuwa na uamuzi wa mwisho. na akishasaini kama alivyofanya mgonjwa tajwa hapo juu, mhudumu wa afya hana kosa, kifupi twasema "his/her ass is covered" - akishtakiwa likely atashinda.

Mkuu unaweza kuishi na kovu la kumuona mwanadamu mwenzako anakufa huku ukijua wazi anaweza kuponywa?
 
mkuu unaweza kuishi na kovu la kumuona mwanadamu mwenzako anakufa huku ukijua wazi anaweza kuponywa?
Yes, mie nitafanya hivyo na sitakuwa na kovu kwa sababu ni uamuzi wake (sahihi according to his/her beliefs) na ndivyo inavyotakiwa. suppose unamlazimisha kumtia damu na akafa vilevile (maana yake anakufa kabla ya kupata fursa ya kutubu - kama anavyosuggest Uda) inakuwa umem-lostisha sio? (according to yeye, na nduguze, ama na jehova witness wenzake).
 
Naamini wenye imani hii wapo humu JF. Kwa nini hawataki kujustfy jambo hili?
 
Ningekuwa Dokta kama hali ya huyo mgonjwa itanilazimu kuvunja miiko ya imani yake basi naivunja na akishapona nitamwambia kuwa imani yangu haikuniruhusu kushuhudia mtu akifa ilhali nilikuwa na uwezo wa kumponya. Hata Yehova mwenyewe alishasema Jisaidie nami nitakusaidia, ametupa madaktari ili watuponye.. Mgawanyo wa majukumu..

My people perish from a lack of knowledge (Hosea 4: 6)
 
Tangu awali Yehova aliiona damu ni kitu kitakatifu ndiyo maana Mungu alimwambia Noa hivi kwenye mwa. 9:3-6 wanaweza kula kila mnyama anatembea aliye hai na kadhalika lakini aliwakataza wasile damu, Hata Yehova alipoandaa agano na watu wake aliendelea kusisitiza hivyo pia, Walawi 17:10-14,7:26,27, na ikiwa mtu angekiuka sheria na kula damu au matumzi yoyote ya damu angestahili kuuwawa kama mstari wa 14 unavyonyesha unavyomalizia.

Katazo hili la matumizi ya damu lilirudiwa mara kwa mara na mitume ndiyo maana mtume Paulo aliwakumbusha wakristo kwenye Matendo 15:28, 29, 21:25, kujiepusha na damu, vibudu,sanamu na kadhalika.
Kwa msingi wa maamdiko hayo mashahidi wa Yehova hujitahidi kufuata makatazo hayo ingawa hukabiliana na changamoto nyingi linapozuka suala kutiwa damu mishipani unaweza tembelea site yao Jehovah's Witnesses: Watchtower Society Official Web Site kwa maelezo zaidi.
 
Ningekuwa Dokta kama hali ya huyo mgonjwa itanilazimu kuvunja miiko ya imani yake basi naivunja na akishapona nitamwambia kuwa imani yangu haikuniruhusu kushuhudia mtu akifa ilhali nilikuwa na uwezo wa kumponya,, Hata Yehova mwenyewe alishasema Jisaidie nami nitakusaidia, ametupa madaktari ili watuponye.. Mgawanyo wa majukumu..

My people perish from a lack of knowledge (Hosea 4: 6)
Katazo la dumu ni la msingi wa maandiko matakatifu kama niyoyataja hapo juu rejea. Ni kweli Mungu anasema tujisaidie naye atatusaidia lakini hajasema tujisaidie kwa kuvunja kanuni na sheria zake ndiyo maana hata Sauli alipomtolea Yehova sadaka Mungu hakuibariki alimwambia kutii ni bora kuliko dhabuhi (sadaka) 1samw. 15:22, Mar. 12:30,33
 
Katazo la dumu ni la msingi wa maandiko matakatifu kama niyoyataja hapo juu rejea. Ni kweli Mungu anasema tujisaidie naye atatusaidia lakini hajasema tujisaidie kwa kuvunja kanuni na sheria zake ndiyo maana hata Sauli alipomtolea Yehova sadaka Mungu hakuibariki alimwambia kutii ni bora kuliko dhabuhi (sadaka) 1samw. 15:22, Mar. 12:30,33

Kwa mazingira ya Tanzania, unadhani mbadala wa damu ni upi? Kuna mpango wowote kwa kanisa la mashahidi wa yehova Tanzania katika kukabiliana na changamoto hii?
 
Tangu awali Yehova aliiona damu ni kitu kitakatifu ndiyo maana Mungu alimwambia Noa hivi kwenye mwa. 9:3-6 wanaweza kula kila mnyama anatembea aliye hai na kadhalika lakini aliwakataza wasile damu, Hata Yehova alipoandaa agano na watu wake aliendelea kusisitiza hivyo pia, Walawi 17:10-14,7:26,27, na ikiwa mtu angekiuka sheria na kula damu au matumzi yoyote ya damu angestahili kuuwawa kama mstari wa 14 unavyonyesha unavyomalizia.

Katazo hili la matumizi ya damu lilirudiwa mara kwa mara na mitume ndiyo maana mtume Paulo aliwakumbusha wakristo kwenye Matendo 15:28, 29, 21:25, kujiepusha na damu, vibudu,sanamu na kadhalika.
Kwa msingi wa maamdiko hayo mashahidi wa Yehova hujitahidi kufuata makatazo hayo ingawa hukabiliana na changamoto nyingi linapozuka suala kutiwa damu mishipani unaweza tembelea site yao Jehovah's Witnesses: Watchtower Society Official Web Site kwa maelezo zaidi.

Mafungu haya hayana uhusiano wowote na suala la mgonjwa kuongezewa damu ya binadamu mwingine ili kunusuru maisha yake. Kimsingi imani hiyo haina tofauti na imani ya madhehebu yanayokataza muumini akiugua asiende hospitali.

Matumizi ya damu ya wanyama kama chakula au kinywaji katika mambo ya walawi ilikuwa ni kulinda afya, ndio maana wanyama wanachinjwa ili kuondoa damu, japo haiondoki yote katika nyama. Lakini pia ulazi/unywaji wa damu una athari za kiroho na kimwili (Afya). Kanuni hizi zingali valid hadi leo, japokuwa watu hukaidi.
 
kwa mazingira ya Tz,unadhani mbadala wa damu ni upi?kuna mpango wowote kwa kanisa la mashahidi wa yehova Tanzania katika kukabiliana na changamoto hii?

Nakubaliana nawe Jackbauer... niliwahi kumwamsha senior/boss wangu usiku wa manane akanitukana...kisa ilikuwa mwanamke shahidi wa Yehova alikuwa mjamzito mimba miezi 9 lakini Hb 4! Ni msala kwa kweli! Alikuwa anaweza ingia labor anytime, mungu bariki siku hiyo alikuja na 'false labor'. Kumshauri tumlaze na tumpe damu ikawa balaa, si mgonjwa si mume hawataki kata kata. Nikampa somo yule mama akawa yuko 50/50 lakini mume kakataa kata kata. Mi niko zamu ikabidi msala nimrushie boss ili likitokea la kutokea 'my *ss will be covered' japo kinafsi ningejisikia vibaya. Boss akanikaripia sana lakini sikuwa na la kufanya.

Mwisho wa siku dada alijifungua salama bila kuongezewa damu (surprisingly!) lakini challenge kwa watoa huduma ya afya, especially kama mgonjwa atafariki.

Nikirudi kwa alichosema Jackbauer, kwa nini sasa hao waumini wa 'nashahidi wa yehova' wasiwe na mpango wa kuwafanya wasihitaji tiba ya damu? Sa kama huyu mumewe kashindwa kumlisha wakati wa uja uzito anakuna na severe anaemia...halafu unachapa mkwara hasiongezewe damu, angemlisha basi hasipate anaemia in the first place! Sio kwenda kuwataka ubaya wahudumu wa afya.
 
Kwa kweli ni changamoto, me nilishamwokoa binti wa miaka 16 alikuja na hb ya 4, familia ikasimika na mazingira ya field nikaita police fasta wakaja tukahangaika na binti akapona. Ila kuna deaths nyingi tu za hawa watu. Nishajaribu kukaa nao wakashindwa kunipa exactly mstar unaotoka kwenye Holy Bible. In collaboration with some UN Agency nilianzia programe ya kuwaelemisha health eating and how to prevent anaemia to pregnant and underfives. Maana hao ndio wako at more risk na hapa kwetu ndio tunaowapata.
 
Unajua imani ni kitu cha ajabu sana, mtu uko radhi afe kwa sababu ya imani fulani. Kwa kweli ni challenge kwa watumishi wa afya. Ila nadhani hata wao watakuwa wanakosea kwa kuruhusu mazingira ya kuishiwa damu. Kwa nini wasile vizuri? au kwa nini wasizuie?
 
Hao waanzisha hilo dhehebu kwao hakuna anemia kama huku third world countries. Waumini wafikirie na hilo. Basi waanzishe hata home gardening ku prevent anaemia, wa wadeworm watoto. Wajikinge na malaria pia waimprove food preparations na eating habits.
 
Hili jambo ni gumu kweli kwa pande zote. Upande mmoja matakwa ya mgonjwa yanastahili kuheshimiwa sababu imani yake haikubali kuongezwa damu. Upande mwingine daktari anawekwa katika muelekeo mgumu pale anapoona mgonjwa wake ambaye pengine hana fahamu yupo taabani sababu ya upungifu wa damu !!

Labda uongozi wa hospitali ungejaribu kuwaita na kuongea na kasisi na familia kujaribu kumshawishi mama kama inawezekana. Mwisho kama yote hayawezekani nadhani matakwa ya mgonjwa yaheshimiwe.
 
Back
Top Bottom