nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2]04 APRIL 2012[/h][h=3]
[/h]
Na Anneth Kagenda
MASHAHIDI wa utetezi upande wa Jamuhuri wamekiri mbele ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kufanya kosa la kisheria kwa kutosaini fomu za matokeo katika vituo vyao.
Wakiongozwa na wakili wa Serikali Bw. Seth Mkemwa, mbele ya Jaji Profesa Ibrahim Juma, mmoja wa mashahidi hao, Bw. Omar Muhando (54), ambaye alikuwa Msimamizi wa Kituo cha Kombo namba 4A, Kata ya Vingunguti, alikiri kutosaini fomu yake.
Alidai hakusaini fomu hizo kwa sababu ya uzee ambapo kosa hilo ameligundua baada ya kuoneshwa fomu hiyo mahakamani hapo.
Alipoulizwa na wakili wa upande wa madai Bw. Peter Kibatala kuwa baada ya kumaliza uchaguzi na kukabidhi fomu kwa wahusika aliambiwa nini kuhusu fomu hiyo, Bw. Muhando alidai pamoja na kusahau, hakuambiwa kitu chchote.
Shahidi mwingine Bi. Yusta Ngoda (30), alidai mahakamani hapo kuwa wakati wa uchaguzi huo alikuwa Msimamizi Mkuu wa Kata ya Vingunguti, Kituo cha Usisede, ambayo naye alikiri kusahau kuweka sahihi na jina lake katia fomu hizo.
Akiongozwa na wakili Bw. Mkemwa, shahidi huyo alidai yeye haoni kama kutoweka sahihi ni kosa kwani fomu hiyo ina vielelezo vinavyoonesha imetoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Mheshimiwa kama nilikosea kusaini fomu, waakala wa CHADEMA angeweka sahihi au angesema fomu namba 16 si halali kama ingekuwa na kasoro hivyo sikuona kama inakosa, alidai.
Alipoulizwa na wakili Bw. Kibatala kuwa wakati wa semina hakuambiwa kwamba kutosaini fomu hiyo ni kosa kisheria, Bi. Ngoda alijibu, Niliambiwa lazima niisaini.
Shahidi mwingine Bi. Alvera Laurence (46) ambaye alikuwa ni Msimamizi Kituo cha Hali ya Hewa C, namba 5, Kata ya Kiwalani, alikiri kufanya makosa tisa katika fomu hiyo ikiwemo kutoweka saini, jina, tarehe ya kufunga na kutojaza nafasi zingine na kudai kisheria alifanya makosa.
Alipoulizwa na wakili wa Serikali Bw. David Kakwaye, alikiri kufanya makosa hayo kutokana na uchovu, kuchelewa kuletewa gari na kuwaza jinsi atakavyobeba makasha yenye kura kichwani. Kesi imepangwa kuendelea leo.
[/h]
Na Anneth Kagenda
MASHAHIDI wa utetezi upande wa Jamuhuri wamekiri mbele ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kufanya kosa la kisheria kwa kutosaini fomu za matokeo katika vituo vyao.
Wakiongozwa na wakili wa Serikali Bw. Seth Mkemwa, mbele ya Jaji Profesa Ibrahim Juma, mmoja wa mashahidi hao, Bw. Omar Muhando (54), ambaye alikuwa Msimamizi wa Kituo cha Kombo namba 4A, Kata ya Vingunguti, alikiri kutosaini fomu yake.
Alidai hakusaini fomu hizo kwa sababu ya uzee ambapo kosa hilo ameligundua baada ya kuoneshwa fomu hiyo mahakamani hapo.
Alipoulizwa na wakili wa upande wa madai Bw. Peter Kibatala kuwa baada ya kumaliza uchaguzi na kukabidhi fomu kwa wahusika aliambiwa nini kuhusu fomu hiyo, Bw. Muhando alidai pamoja na kusahau, hakuambiwa kitu chchote.
Shahidi mwingine Bi. Yusta Ngoda (30), alidai mahakamani hapo kuwa wakati wa uchaguzi huo alikuwa Msimamizi Mkuu wa Kata ya Vingunguti, Kituo cha Usisede, ambayo naye alikiri kusahau kuweka sahihi na jina lake katia fomu hizo.
Akiongozwa na wakili Bw. Mkemwa, shahidi huyo alidai yeye haoni kama kutoweka sahihi ni kosa kwani fomu hiyo ina vielelezo vinavyoonesha imetoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Mheshimiwa kama nilikosea kusaini fomu, waakala wa CHADEMA angeweka sahihi au angesema fomu namba 16 si halali kama ingekuwa na kasoro hivyo sikuona kama inakosa, alidai.
Alipoulizwa na wakili Bw. Kibatala kuwa wakati wa semina hakuambiwa kwamba kutosaini fomu hiyo ni kosa kisheria, Bi. Ngoda alijibu, Niliambiwa lazima niisaini.
Shahidi mwingine Bi. Alvera Laurence (46) ambaye alikuwa ni Msimamizi Kituo cha Hali ya Hewa C, namba 5, Kata ya Kiwalani, alikiri kufanya makosa tisa katika fomu hiyo ikiwemo kutoweka saini, jina, tarehe ya kufunga na kutojaza nafasi zingine na kudai kisheria alifanya makosa.
Alipoulizwa na wakili wa Serikali Bw. David Kakwaye, alikiri kufanya makosa hayo kutokana na uchovu, kuchelewa kuletewa gari na kuwaza jinsi atakavyobeba makasha yenye kura kichwani. Kesi imepangwa kuendelea leo.