Japhari Shabani (RIP)
R I P
- Jan 16, 2007
- 721
- 176
Kasoro nyingi zajitokeza siku ya uchaguzi
Sunday, 31 October 2010 17:09
Waandishi Wetu
PAMOJA na amani kutawala katika maeneo mengi nchini wakati wa kupiga kura, kasoro nyingi zimeripotiwa kwenye sehemu mbalimbali ambazo zilisababishwa na upungufu na ucheleweshaji wa vifaa vya kupigia kura pamoja na majina ya wapigakura kutoonekana.
Mkoani Dodoma mjini dosari hiyo ilionekana baada ya kukamatwa kwa masanduku ya kupigia kura yakiwa na karatasi za kura kwenye nyumba ya mtu binafsi nje kidogo ya kituo cha kupigia kura.
Masanduku hayo mawili yaliyokuwa yamesheheni karatasi za kura yalikamatwa Oktoba 30 mtaa wa Majengo Mjini Dodoma saa 2:00 usiku kwenye nyumba hiyo ya mtu aliyejulikana kwa jina la Mwalimu Walburga Tarimo.
Aidha ambaye pia ilidaiwa kuwa mwalimu huyo ndiye atakayekuwa msimamizi wa kituo cha uchaguzi cha Makole.
Sunday, 31 October 2010 17:09
Waandishi Wetu
PAMOJA na amani kutawala katika maeneo mengi nchini wakati wa kupiga kura, kasoro nyingi zimeripotiwa kwenye sehemu mbalimbali ambazo zilisababishwa na upungufu na ucheleweshaji wa vifaa vya kupigia kura pamoja na majina ya wapigakura kutoonekana.
Mkoani Dodoma mjini dosari hiyo ilionekana baada ya kukamatwa kwa masanduku ya kupigia kura yakiwa na karatasi za kura kwenye nyumba ya mtu binafsi nje kidogo ya kituo cha kupigia kura.
Masanduku hayo mawili yaliyokuwa yamesheheni karatasi za kura yalikamatwa Oktoba 30 mtaa wa Majengo Mjini Dodoma saa 2:00 usiku kwenye nyumba hiyo ya mtu aliyejulikana kwa jina la Mwalimu Walburga Tarimo.
Aidha ambaye pia ilidaiwa kuwa mwalimu huyo ndiye atakayekuwa msimamizi wa kituo cha uchaguzi cha Makole.