Marxism–Leninism

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Marxism–Leninism ni mfumo wa siasa au uliojulikana duniani kama Marxism na Leninism, lengo lilikua kuanzisha serikali za kijamaa na kuziendeleza zaidi. Marxist–Leninists walihodhi mfumo huu na waliusambaza pembe zote za dunia kutokana na uelewa wa sehemu ile, lakini kipaumbele cha mfumo huu ilikua chama kimoja cha kisiasa kitakacho endesha serikali ambayo itasimami uchumi, maswala ya kimataifa, elimu, afya, jeshi, na maswala mengine yote. Hii ilikuwa tofauti na siasa za kibepari ambayo kuna tabaka la mabwana ambao walimiliki uchumi wa nchi. Siasa hii imebakia katika serikali za China, Cuba, Laos na Vietnam na huu ndio ulikua mfumo wa Communist Party of the Soviet Union (CPSU) na nchi nyingine za ulaya Mashariki (Eastern Block).

Marxism-Leninism kwanza walianza filosofa hii kwa mawazo yaliyofanana katika Muungano wa Kisoviet mnamo miaka ya 1920, wakati Joseph Stalin na wengine waliomuunga mkono kuchukua madaraka ya Chama Cha Kikomunist cha Urusi (bolsheviks). Kilikataa wazo hili la Umoja la Marxists wakati dunia ikiwa kwenye mapinduzi umuhimu wa siasa za ujamaa (siasa mkusanyo wa mapato) na baadae kuhama kutoka ubepari mpaka kufikia Taifa la kijamaa. Mwisho walikuja na mpango wa miaka mitano. Kimataifa pia mpango huu ulianza kutangazwa na kuanza kusaidia mapinduzi ya nchi nyingine ili ziunge mkono mfumo huu wa siasa.

Lenintribune.jpg

Vladimir Lenin

Malengo ya Marxism-Leninism yaliendeleza taifa kuelekea kwenye jamhuri ya kisoshalist kupitia uongozi wa kimapinduzi, tabaka la watawaliwa ambao walianza kuona maonevu kutokana na nafasi yao katika jamii. Serikali ya kisoshalist inapinga ukandamizwaji wa tabaka la watu wa chini na chama tawala kinasimamia uongozi wa kidemokrasia unaoongoza nchi nzima kitu ambacho Vladimir Lenin alielezea kama "tunagawanyika katika mijadala lakini tunaungana kwa vitendo". Usoshalist ulilenga ujamaa ambao ni mfumo usio na matabaka, hakuna mmiliki wa mali na vitega uchumi vyote vimilikiwe na serikali na raia wote wawe na haki sawa katika jamii.

Kijamii.
Marxism–Leninism ilihakikisha huduma zote za jamii kutolewa bure bila ubaguzi. Uboreshaji wa huduma za afya, elimu, malezi ya watoto na huduma zote za jamii zigharamiwe na serikali. Soko la kazi na ajira kupanuliwa na watu waletewe maendeleo kutokana na makusanyo ya serikali. Watu wapewe elimu kuhusu uchumi na mipango ya nchi kwa njia ya elimu kwa wote bila ya matabaka.

Uchumi.
Serikali kuwa mmiliki na mwangalizi wa secta ya uzalishaji kupitia umilikaji wa jamii.Kwa kuzingatia uzalishaji bora na kupunguza hasara tekinologia ya sayansi ifuatwe bila kuangalia ufundi wa masoko na unafuu wa bei na nguvu ya nchi kufanya manunuzi kwa pamoja kufute nguvu ya soko huria na usawa kati ya uzalishaji uuzaji na ununuaji ufikiwe kutokana na utafiti wa kisayansi.

180px-Karl_Marx.jpg

Marxi

Kisiasa.
Marxism-Leninism waliunga mkono mfumo wa chama kimoja cha siasa kwa nchi nzima, chama hicho kitafuta sera za ujamaa na kuleta usoshalist katika jamii ya kijamaa. Nguvu na maamuzi ya chama yatawakilisha wengi kupitia kupitia uchaguzi wa kidemokrasia na utawala wa vitongoji mpaka taifa.
 
Sijaelewa lengo hasa la MADA.

Kuhusu matabaka mifuko yote ina matabaka labda lililo muhimu ni kutanabaisha matabaka yepi. Kwa mfano kwenye mfumo wa ujamaa kulikuwa na kungali na tabaka la watawala. Chini ya mfumo wa chama kimoja vigogo wa chama hugeuka kuwa tabaka la watawala na kufaidi "MEMA" ya nchi.
 
ni mfumo ambao unaamini katika kuafanya kazi kwa bidii kwa faida si yako tu bali jamii nzima.

baadhi ya wachambuzi wa kisiasa huuita kama udikteta kwa sababu unampa kiongozi na chama chake nguvu kubwa ya kuongoza jamii.

kwa ujumla mfumo huu ulipaswa utumike katika nchi zetu zinazoendelea, ubepari kwa sasa hau fit na hali yetu yakiuchumi
 
Sijaelewa lengo hasa la MADA.

Kuhusu matabaka mifuko yote ina matabaka labda lililo muhimu ni kutanabaisha matabaka yepi. Kwa mfano kwenye mfumo wa ujamaa kulikuwa na kungali na tabaka la watawala. Chini ya mfumo wa chama kimoja vigogo wa chama hugeuka kuwa tabaka la watawala na kufaidi "MEMA" ya nchi.
Hii haikuwa dhana ya waanzilishi wa ujamaa, mfumo wa ujamaa unazingatia kwenye collectiveness, mapato ya nchi yanakusanywa na kuboresha miundo mbinu pamoja na huduma nyingine kwa faida ya wananchi wote. Serikali ndiye mmiliki wa rasilimali zote za nchi.
 
N

AZIDI KUKUELEWA MFUMO HAUKUWA NA NIA YA UNYONYAJI SIO...?
Mfumo huu ulilenga kwenye usawa, hakuna bwana na mtwana, wote ni ndugu. Ndiyo maana huku kwetu neno Sir lilifutwa wote tulikua Ndugu, Ndugu Juma, Ndugu Peter....ect. Lakini cha ajabu hata waliouanzisha wameushindwa. Ni mfumo mgumu kuuteleza.
 
Hii haikuwa dhana ya waanzilishi wa ujamaa, mfumo wa ujamaa unazingatia kwenye collectiveness, mapato ya nchi yanakusanywa na kuboresha miundo mbinu pamoja na huduma nyingine kwa faida ya wananchi wote. Serikali ndiye mmiliki wa rasilimali zote za nchi.

Kwani huyo mwanzilishi/waanzilishi ni wapi walipoitumia "dhana" hii ikawa haina tabaka la watawala?
 
Ni mfumo mzuri lakini unahitaji nidhamu ya Hali ya juu. Kwa nchi kama yetu ilitakiwa tuendelee nao lakini ndio hivyo tena.!
 
Kwani huyo mwanzilishi/waanzilishi ni wapi walipoitumia "dhana" hii ikawa haina tabaka la watawala?
Kwenye ujamaa hakuna tabaka la watawala bali kuna viongozi wanaochaguliwa kidemokrasia kama wawakilishi wa wananchi.
 
Marxism–Leninism ni mfumo wa siasa au uliojulikana duniani kama Marxism na Leninism, lengo lilikua kuanzisha serikali za kijamaa na kuziendeleza zaidi. Marxist–Leninists walihodhi mfumo huu na waliusambaza pembe zote za dunia kutokana na uelewa wa sehemu ile, lakini kipaumbele cha mfumo huu ilikua chama kimoja cha kisiasa kitakacho endesha serikali ambayo itasimami uchumi, maswala ya kimataifa, elimu, afya, jeshi, na maswala mengine yote. Hii ilikuwa tofauti na siasa za kibepari ambayo kuna tabaka la mabwana ambao walimiliki uchumi wa nchi. Siasa hii imebakia katika serikali za China, Cuba, Laos na Vietnam na huu ndio ulikua mfumo wa Communist Party of the Soviet Union (CPSU) na nchi nyingine za ulaya Mashariki (Eastern Block).

Marxism-Leninism kwanza walianza filosofa hii kwa mawazo yaliyofanana katika Muungano wa Kisoviet mnamo miaka ya 1920, wakati Joseph Stalin na wengine waliomuunga mkono kuchukua madaraka ya Chama Cha Kikomunist cha Urusi (bolsheviks). Kilikataa wazo hili la Umoja la Marxists wakati dunia ikiwa kwenye mapinduzi umuhimu wa siasa za ujamaa (siasa mkusanyo wa mapato) na baadae kuhama kutoka ubepari mpaka kufikia Taifa la kijamaa. Mwisho walikuja na mpango wa miaka mitano. Kimataifa pia mpango huu ulianza kutangazwa na kuanza kusaidia mapinduzi ya nchi nyingine ili ziunge mkono mfumo huu wa siasa.

Lenintribune.jpg

Vladimir Lenin
Haya maandishi ni matamu sana...hawa watu walilenga kuleta usawa katika jamii, unfortunately equality is not an element of nature...napenda sana history, it seems that our future lie within out past.
 
Back
Top Bottom