Marufuku kubeba petroli kwenye vidumu

sasa kama nataka kusafiri safari ndefu na inanilazimu nibebe mafuta ya ziada ndio nafanyaje?

Hapo ndipo tunapoona kuwa nchi haina viongozi wanaofikiria beyond their own interests. Ningekuwa mimi ni muhusika ningesema mtu asiuziwe mafuta kwenye kidumu mpaka aoneshe kadi ya gari au aje na gari kituoni au aoneshe leseni au risiti ya kumiliki chombo kinachotumia mafuta ambacho hakiondosheki. Ukweli ni kwamba sheria hii ya kijinga inatekelezwa na wenye vituo kwa sababu inawapatia mwanya wa kuwaibia wananchi through faulty pumps. Kamaa ingekuwa inawabana wasingeitekeleza asilani. Nafikiri wahusika wanatakiwa kuja na tamko jipya kuhusu huu upuuzi. Maamuzi ya kukurupuka ni mabaya sana, walitakiwa kufanya utafiti kwanza wa kwa nini wtu hutumia vidumu?. Je kuna petrol stations za kutosha kwenye barabara kuu?, halafu wajiulize je kuna usalama katika barabara kuu kwa mtu kutembea na kiasi kikubwa cha pesa ili kununulia mafuta?, majibu yote haya ndiyo yangepelekea kuana na maamuzi sahihi.
 
dira ya kigari chako cha mkopo haifanyi kazi, gari inakuzimikia kisa mafuta hakuna, unafungua buti, unatoa kidumu cha rita 5 haraka unaenda kituoni ili ununue mafuta safari iendelee, ghafla muuza mafuta anakwambia ni marukufu kuja na vidumu hapa, unamueleza hali ulitonayo kuwa gari imekuzimikia hivyo huna jinsi HATAKI KATUKATU. ghafla linakuja daldala limejaZa watu pomoni. anakuacha wewe pale unashangaa anakwenda kumuhudumia konda wa daladala. WANA JF nisaidieni hivi ile sheria ya kujaza mafuta huku gari likiwa na abiria imefutwa.....? NA HII YA KUTONUNUA MAFUTA KTK VIDUMU NDIO MBADALAAAAA..........?

Niliudhika juzi kiasi cha kutaka kumwaga matusi ya nguoni kwa wauzaji mafuta, Umeme wa mgao, mimi nimeshasahau kuhusu Tanesco ninakijenereta changu miaka nenda rudi, nafika kituo cha mafuta eti kidumu hakiruhusiwi, mbaya zaidi siku hiyo kulikuwa na msiba hivyo tulihitaji sana mwanga hivyo genreta ndiyo ilikuwa mkombozi wetu! Sasa jamani hivi viongozi wetu wanachowaza kwa watanzania wa hali za chini ni kuwaudhi na kuwaumiza tu!! Mbona hivyo jamani? mbona mna mambo ya..............mbu, ......zenu........wako@******##$$&&& sitaki hata kutamka hayo maneno kwa kujali maadili ila kama tungekutana ana kwa ana bila ushahidi anangejuta huyo mwenye mawazo ya kuzuia vidumu.
 
Na sisi ambao tunaishi vijijini umbali wa kilomita 50 toka mjini itakuwaje? manake huko kwetu abiria wanasafirishwa ktk malori ambayo yamebeba madumu ya mafuta ya dizeli kwa ajili ya mashine za nafaka,sheria inasemaje?
 
"Wenye majenereta na mashine za nafaka wazibebe mpaka Petrol Station...."

Mwisho wa kunukuu....
 
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), imepiga marufuku matumizi ya chupa za plastiki (vidumu) kuhifadhi au kubebea mafuta jamii ya petroli, kwa kuwa zina uwezo mkubwa wa kulipuka.

Pia imewataka wauzaji wa nishati hiyo katika vituo vyote vya mafuta nchini, kukataa kuhudumia wateja watakaohitaji petroli bila kuwa na magari yao vituoni kama njia ya kuwaelimisha juu ya athari za matumizi ya chupa au vidumu hivyo

Source: Habari leo


Maoni yangu

  1. Sisi tunaotumia magenereta kwenye biashara zetu na majumbani tufanye nini?
  2. Sheria hii inataka kutuaminisha kwamba mwenye gari akiishiwa mafuta ghafla basi ni mzembe. Tuchukulie mazingira kwamba umebakiwa na mafuta kidogo kwenye gari, lakini yanatosha kufika sheli iliyo umbali wa kama KM 25, then unafika na gari yako kwenye sheli hiyo, unakuta mafuta wameishiwa au hawa operate. The next sheli ni KM 25 zingine, uliskume gari mpaka huko?

Licha ya kukuta mafuta hakuna petrol station, foleni tu za mjini zinaweza kupotezea timing.
 
Chupa ya plastiki ndio vidumu????????????? mbona chupa ni chupa dumu ni dumu na material yanayotengeneza dumu sio yanayotengeneza chupa za plastic. Labda mtoa hoja ajikague tena, vituo vya mafuta wanakaataa chupa za plastic na sio madumu bana.

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), imepiga marufuku matumizi ya chupa za plastiki (vidumu) kuhifadhi au kubebea mafuta jamii ya petroli, kwa kuwa zina uwezo mkubwa wa kulipuka.

Pia imewataka wauzaji wa nishati hiyo katika vituo vyote vya mafuta nchini, kukataa kuhudumia wateja watakaohitaji petroli bila kuwa na magari yao vituoni kama njia ya kuwaelimisha juu ya athari za matumizi ya chupa au vidumu hivyo

Source: Habari leo


Maoni yangu

  1. Sisi tunaotumia magenereta kwenye biashara zetu na majumbani tufanye nini?
  2. Sheria hii inataka kutuaminisha kwamba mwenye gari akiishiwa mafuta ghafla basi ni mzembe. Tuchukulie mazingira kwamba umebakiwa na mafuta kidogo kwenye gari, lakini yanatosha kufika sheli iliyo umbali wa kama KM 25, then unafika na gari yako kwenye sheli hiyo, unakuta mafuta wameishiwa au hawa operate. The next sheli ni KM 25 zingine, uliskume gari mpaka huko?
 
Back
Top Bottom