Kwa wanaojua sheria naomba kujua maswala ya likizo za kinamama wanapojifungua. Mtu akijifungua huwa office ya serikali au binafsi zinampa likizo ya muda wa miezi mitatu. Na je hii likizo ikishaisha huwa kuna likizo ya nusu siku kwaajili ya kwenda kunyonyesha au la. Kwani watu wamekuwa wanaiongelea lakini aijulikani mtu anatakiwa apewe muda gani kwa wafanyakazi wa office binafsi na za serikali. Naomba nipewe ufananuzi na wataalamu wa haya mambo.