Marin Hassan wa TBC jichunguze...

Wa Mjengoni

JF-Expert Member
May 4, 2010
480
128
Leo asubuhi katika kipindi cha jambo TBC ulikuwa unamhoji Mama mmoja Katibu wa Chama cha Waandishi wa habari Tanzania alikujibu wazi kuwa kitendo cha Mwandishi wa habari kuegemea wazi upande mmoja kinamaanisha hajui aliyofundishwa kwenye taaluma hiyo na hivyo ana kiwango cha chini. Wewe ni mmoja wa hao waandishi wenye viwango hivyo kwa sababu unapenda kulitumia jukwaa la Jambo Tanzania hasa baada ya mapitio ya magazeti kukejeli vyama vya upinzani. Binafsi nishakusikia mara mbili:

Mara ya kwanza: "Hawa akina Dr. Slaa wasindikizaji tu...... au unasemaje Bw. (Msomaji wa magazeti)" ...bahati nzuri huyo msomaji anajua profession yake hakukuunga mkono, simply alisema tungoje oktoba mwishoni.

Mara ya pili: "Walisema watu wao wana viwango sasa huyu darasa la saba, vipi tena" ukimaanisha Mgombea mwenza wa CHADEMA.

Kwa taaluma yako hutakiwi kusema hivyo unless unavua utangazaji na kuja kwenye ulingo wa siasa. Vilevile usitumie kipindi hiki cha Jambo kujitetea kwa yale yaliyojiri siku ya ufunguzi wa kampeni za CHADEMA jangwani. Leo ulisema Mh. Lwakatare aliwafukuza waandishi wa TBC. Ni vizuri ukiongea hivyo na mwenyewe awepo hapo kwenye kipindi, na ndio taaluma inataka.
 
Wa mjengoni, kwanini unajitafutia maudhi? Why watch this TV station! Thank God mimi kwangu haipatikani!!
 
Kinachouma ni kuwa ni kodi zetu zinatumika....hawa wajinga wanadhani ni hela za mfukoni mwa Kikwete

Tatizo la watu kama akina Marin ni kwamba wanalinda mifumo inayowakandamiza wao wenyewe. Huyu Mwandishi ukimuona kwenye kipindi utajua ameukata lakini ukimkuta anagombania daladala utadhani naye ni miongoni mwetu. Akipewa ziara tu ya kwenda na hao mafisadi yeye tayari meno nje.

Kama angekuwa mbwa angekuwa anabiligisha (kutikisatikisa) mkia kwa kwenda mbele
 
Huyo Mzanzibara ndivyo alivyo, ana tabia za kujifanya mjuaji sana wa mambo.

Lakini inaonekana kuna mpango maalum wa kuitangaza ccm na kuwabania nafasi vyama vingine, issue ya jumamosi kwenye uzinduzi wa kampeni za chadema imewasaidia kutafuta kisingizio cha kutorusha hewani habari zao.

Lakini kwa kuwa wanatumia kodi zetu tutawabana hadi waache upuuzi wao.
 
Kile kibano alichopewa mpaka akaenda kujisalimisha kituo cha polisi bado hajakoma tu? TBC niliwataadhalisha toka mwaka 2005 kwamba kwa tabia yao ya upendeleo wa waziwazi haki yetu tutaitafuta kwa nguvu. Mkong'oto ameanza kuupata yeye tukimaliza hapo tunakwenda kwa Tido ambaye inaonekana ile tabia ya Mtukufu rais Daniel Arap Moi haijamtoka !
 
With time kama TBC kama Taasisi wanajirekebisha, leo tar 01/09/2010 niliweza kuona TBC ikicover hata wagombea wa vyama vya upinzani wanaotembea nyumba kwa nyumba.

Nashauri aliyeanzisha thread hii achukue hatua kuhusu matamshi ya Marin Hassan akitaja siku, tarehe na maneno ailyotamka na kwa kupeleka malalamiko hayo Baraza la Habari nakala TBC tuone kama hataacha kupayuka payuka
.

Hiyo ni haki ya wasikilizaji chini ya sheria zetu za habari.
 
Tatizo la watu kama akina Marin ni kwamba wanalinda mifumo inayowakandamiza wao wenyewe. Huyu Mwandishi ukimuona kwenye kipindi utajua ameukata lakini ukimkuta anagombania daladala utadhani naye ni miongoni mwetu. Akipewa ziara tu ya kwenda na hao mafisadi yeye tayari meno nje.

Kama angekuwa mbwa angekuwa anabiligisha (kutikisatikisa) mkia kwa kwenda mbele

......hana tofauti na EPHRAIM KIBONDE....all these two were failures kwenye nyumba ya kuta nne....nisisemaga hata kabla kampeni hazijaanza kuwa huyu marin....ana tatizo na nilitaka tujuwe kiwango chake cha elimu.......maana hata ushabiki wa mwandishi msomi hupelekwa kisomi...sio kijinga...

Kinginge ni kuwa Marin hata namna anavyohoji watu anakosa adabu....utaona namna wageni wake wanavyokuwa uncomfortable na yeye hushindwa kuwasoma..inawezekana anataka kuwaiga watu kama TIM SEBASTIAN ambaye huuliza maswali ya papo kwa papo...ambapo akimuhoji mtu mwenye akili nyepesi kama JK itaonekana kama anamdhalilisha...

Tatizo la Marin ni kutokuwa na ufahamu wa kutosha ...wakati anafanya mahojiano...na kujifanya mjuaji .....na zaidi analo tatizo kama la Mwakwaia la kutompa mtu anayemuhoji muda ..na kutaka kumpeleka kule anakoamini yeye badala ya kumuacha mgeni atoe mawazo yake .....
 
......hana tofauti na EPHRAIM KIBONDE....all these two were failures kwenye nyumba ya kuta nne....nisisemaga hata kabla kampeni hazijaanza kuwa huyu marin....ana tatizo na nilitaka tujuwe kiwango chake cha elimu.......maana hata ushabiki wa mwandishi msomi hupelekwa kisomi...sio kijinga...
You have said it well. Hawa watu walio shallow wakapewa vipaza sauti wamejipa kazi ya kuwa walimu wakuu. Kibonde sasa hivi amebobea katika kazi hiyo...anajitahidi kwa nguvu zake zote kuhamishia uwezo wake mdogo wa kufikiri kwenye fikra zetu watanzania.

Nampa pole sana maana kama hatabadilika safari yake mbona itakuwa ngumu sana kwenye hii world inayohitaji competence,
 
Huyu mtangazaji anapaswa aachishwe kazi hiyo mara moja, hasa kama anatangaza kwenye televisheni ya taifa. Amevunja maadili ya kazi.
 
Hasan marina na Kibonde hawajui kuwa wao niwatumwa tu wa mafisadi?
 
Siku zote katika maisha lazima ujue kuwa kuna WATU wananunulika. Wako pale kuhakikisha mafisadi wanaendelea kuimaliza nchi bila bughudha. Hawajui umuhimu wa upinzani katika kuifanya serikali ifanye kazi. Ni kama mbwa wa mkoloni enzi zile!!!
 
Licha ya ujuaji wake,Marin amejaa dharau,na ubabe wa wazi wazi hadi kwa watangazaji wenzake yaani ni kichefuchefu hata kumuona anaongoza kipindi cha jambo :glasses-nerdy:
 
Back
Top Bottom