Wa Mjengoni
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 480
- 128
Leo asubuhi katika kipindi cha jambo TBC ulikuwa unamhoji Mama mmoja Katibu wa Chama cha Waandishi wa habari Tanzania alikujibu wazi kuwa kitendo cha Mwandishi wa habari kuegemea wazi upande mmoja kinamaanisha hajui aliyofundishwa kwenye taaluma hiyo na hivyo ana kiwango cha chini. Wewe ni mmoja wa hao waandishi wenye viwango hivyo kwa sababu unapenda kulitumia jukwaa la Jambo Tanzania hasa baada ya mapitio ya magazeti kukejeli vyama vya upinzani. Binafsi nishakusikia mara mbili:
Mara ya kwanza: "Hawa akina Dr. Slaa wasindikizaji tu...... au unasemaje Bw. (Msomaji wa magazeti)" ...bahati nzuri huyo msomaji anajua profession yake hakukuunga mkono, simply alisema tungoje oktoba mwishoni.
Mara ya pili: "Walisema watu wao wana viwango sasa huyu darasa la saba, vipi tena" ukimaanisha Mgombea mwenza wa CHADEMA.
Kwa taaluma yako hutakiwi kusema hivyo unless unavua utangazaji na kuja kwenye ulingo wa siasa. Vilevile usitumie kipindi hiki cha Jambo kujitetea kwa yale yaliyojiri siku ya ufunguzi wa kampeni za CHADEMA jangwani. Leo ulisema Mh. Lwakatare aliwafukuza waandishi wa TBC. Ni vizuri ukiongea hivyo na mwenyewe awepo hapo kwenye kipindi, na ndio taaluma inataka.
Mara ya kwanza: "Hawa akina Dr. Slaa wasindikizaji tu...... au unasemaje Bw. (Msomaji wa magazeti)" ...bahati nzuri huyo msomaji anajua profession yake hakukuunga mkono, simply alisema tungoje oktoba mwishoni.
Mara ya pili: "Walisema watu wao wana viwango sasa huyu darasa la saba, vipi tena" ukimaanisha Mgombea mwenza wa CHADEMA.
Kwa taaluma yako hutakiwi kusema hivyo unless unavua utangazaji na kuja kwenye ulingo wa siasa. Vilevile usitumie kipindi hiki cha Jambo kujitetea kwa yale yaliyojiri siku ya ufunguzi wa kampeni za CHADEMA jangwani. Leo ulisema Mh. Lwakatare aliwafukuza waandishi wa TBC. Ni vizuri ukiongea hivyo na mwenyewe awepo hapo kwenye kipindi, na ndio taaluma inataka.