Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Kwa matukio yanayoendelea huko nchini Misri dhidi ya raisi Hosni Mubarak aondoke madarakani kwakua wananchi wamechoshwa na utawala wake wa kidikteta,raisi wa Marekani bwana Obama naye tumemnukuu eti akimshauri Hosni Mubarak aruhusu demokrasia nchini Misri. Lakini cha kushangaza ni kua hatukusikia Obama akisema Mubarak alaaniwe kama anavyolaaniwa Gbagbo! ni jambo lakushangaza sana na hapa ndio napata picha Marekani huwa na maslahi na nchi fulani fulani za Kiafrika na hii inajionyesha ni jinsi gani Obama na serikali yake ya Marekani wanavyouma na kupuliza. kwa mfano Obama kabla hajawa rais alilaani sera za Bush kuunga mkono madikteta wa nchi za Kiarabu.Lakini baada ya Obama kuingia White House naye akaendelea kuyapatia majeshi ya Mubarak dola bilioni 1.5 kila mwaka na kwataarifa kutoka kwa wataalamu wa mambo ya nnje wanasema Misri ndio nchi ya pili ulimwenguni katika misaada kutoka Marekani! Je hapa Marekani inamaniisha nini?