Marekani Wanamaanisha Nini Hapa?

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Kwa matukio yanayoendelea huko nchini Misri dhidi ya raisi Hosni Mubarak aondoke madarakani kwakua wananchi wamechoshwa na utawala wake wa kidikteta,raisi wa Marekani bwana Obama naye tumemnukuu eti akimshauri Hosni Mubarak aruhusu demokrasia nchini Misri. Lakini cha kushangaza ni kua hatukusikia Obama akisema Mubarak alaaniwe kama anavyolaaniwa Gbagbo! ni jambo lakushangaza sana na hapa ndio napata picha Marekani huwa na maslahi na nchi fulani fulani za Kiafrika na hii inajionyesha ni jinsi gani Obama na serikali yake ya Marekani wanavyouma na kupuliza. kwa mfano Obama kabla hajawa rais alilaani sera za Bush kuunga mkono madikteta wa nchi za Kiarabu.Lakini baada ya Obama kuingia White House naye akaendelea kuyapatia majeshi ya Mubarak dola bilioni 1.5 kila mwaka na kwataarifa kutoka kwa wataalamu wa mambo ya nnje wanasema Misri ndio nchi ya pili ulimwenguni katika misaada kutoka Marekani! Je hapa Marekani inamaniisha nini?
 
ni fursa nyeti ya kuzielewa rangi zote za hawa watu..muhimu ni kwamba wanacholinda ni maslahi yao na marafiki zao wa karibu tuu, hata kwa kuny'onga demokrasia wanayojifanya kuihubiri..
 
Mkuu,
Inamaanisha kuwa Marekani wanasimamia interest zao tu!
Kama hakuna interest zao, kafilie mbali...lakini kama kuna kitu wanataka basi watakupaka mafuta na kukusifu na kukuspray perfume kidogo.
Wakipata chao bomba..
Siku hizi si unasikia pia hapa kwetu mara balozi wa marekani ametoa milioni 20, mara marekani wamechangia nini...unafikiri wanatupenda?
Wanatia grease kulainisha deals zao tu.... Uliona vita ya Iraq, walipoingia walifanya nini? Kwanza kulinda visima vya mafuta...na demokrasi unaiona huko Iraq hadi hii leo au vipi?
Kwa hiyo mkuu, Marekani ni kulinda interest zao tu, hapendwi mtu!!
Umesahau wikileaks documents? Ni move zao kusambaratisha nchi ambazo walikwishazi/target zamani na unauona moto wake...wameuwasha kweli...
Hata ya kwetu wametoa ya Hosea na ushughulikiaji wa ufisadi na rushwa...wamemtaja nani ni kikwazo? Kwa hiyo hata hii yetu wanataka vitu vyao...
 
Kwa matukio yanayoendelea huko nchini Misri dhidi ya raisi Hosni Mubarak aondoke madarakani kwakua wananchi wamechoshwa na utawala wake wa kidikteta,raisi wa Marekani bwana Obama naye tumemnukuu eti akimshauri Hosni Mubarak aruhusu demokrasia nchini Misri. Lakini cha kushangaza ni kua hatukusikia Obama akisema Mubarak alaaniwe kama anavyolaaniwa Gbagbo! ni jambo lakushangaza sana na hapa ndio napata picha Marekani huwa na maslahi na nchi fulani fulani za Kiafrika na hii inajionyesha ni jinsi gani Obama na serikali yake ya Marekani wanavyouma na kupuliza. kwa mfano Obama kabla hajawa rais alilaani sera za Bush kuunga mkono madikteta wa nchi za Kiarabu.Lakini baada ya Obama kuingia White House naye akaendelea kuyapatia majeshi ya Mubarak dola bilioni 1.5 kila mwaka na kwataarifa kutoka kwa wataalamu wa mambo ya nnje wanasema Misri ndio nchi ya pili ulimwenguni katika misaada kutoka Marekani! Je hapa Marekani inamaniisha nini?

usishangae sana. foreign policy ya america imeshandikwa for the next hundred years. Hata wewe ukiamka kesho ukawa president wa america lazima uifuate.
 
Na tusishangae hiyo siku Hosni Mubarak ataondoka Misri kama hajakimbilia Marekani basi atakimbilia nchi ambayo Wamarekani wanaibeba nchi hiyo na wana maslahi nayo! sidhani kabisa kama atakimbilia Uarabuni!
 
Hao ndio wazungu bwana hawana rafiki wala adui wa kudumu ....aklil mukichwa!
 
Good point. Anaother Issue ni kwamba, issue ya Misri ipo zaidi ktk interest za Israel kuliko hata Marekani yenyewe. Unajua Mubarak aliweza kuwasikiliz nchi za West ktk benefit nyingi za Israel, kama vila peace process na kuitambua Israel. Ktk vita vya Gaza, Mubaraka aliwaekea blockade Wapalestine kwa ajili ya kuwabenefit Israel. Hii yote inatokana na Marekani kuipatia Egypt foreign aid approximately 1.3 annually.

Sasa hivi kuna issue kwamba kama Mubarak ataondoka basi Israel peace process na nchi zake jirani itakuwa mashakani, especially kuiangalia nchi kama Jordan ambayo ina urafiki mkubwa na Israel ipo ktk matatizo kama hayo.

Waisrael wanamuogopa Muhammad Elbaradei kuongoza nchi; kwa sababu huyu jamaa anaipinga sana Israel. Inasemekana Israel wanampa pressure Obama, ili amwambie Mubarak asiachie adaraka mpaka apatikane mtu ambaye atakuwa kibaraka wa USA na Israel.

Sasa hivi kuna mpango wa kuwapiganisha wenyewe kwa wenyewe wa Egypt ili issue ya Mubarak ya iuzulu iishe na iwe sababu ya Mubarak kuendelea kutawala mpaka apatikane kibaraka wao.
 
marekani nao watu maana watu ni nyutu zao hakuna nyutu...no watu..mimi tena ndo nasubiri yanayotokea misri ntawatafuta wamarekani katika kila kona hata kwa baiskeli.....:sick::sick::sick::sick: wavuta bangi wakubwa sana hawa wamarekani na ngoja ije vita ya kugombea mali ghafi na vile ziko chache watanyukana hadi watie akili....natural resources ni chache oneday itaibuka vita tu.....
 
:clap2::clap2::clap2:....kweli nonda.... wanatupaka grease? nooo... wanatupaka mate hadi tulainike maana msaada wanaotoa hautafanana na uranium yetu...tukiwa laini wanabeba chao na maumivu yatakuja kwa wajukuu zetu....grease gharama sisi yetu mate tu kwenye vipaza sauiti hujui hilo?
 
haki...ameongea kitu ambacho amechanganya kidogo tu ...ngoja nitie neno hapa ili nisakafie{cementation}.....kwani wamarekani ni nani ni wayahudi kwa sasa wengine ni wahamiaji tu obama baba ni mkenya mama ni myahudi.. na mwenye uhalali wakujua mtoto ni wa nani ni mama ok ...ukweli ni huo once you talk of the real americans at the time present ...you talk of exiled jews in america..palestina iliwekewa vikwazo na mabepari wa wakimarekani ..who are they to do that na hata dunia iliogopa?
 
Back
Top Bottom