Marekani kupewa Kigamboni

jinalangu

Member
Dec 7, 2010
17
0
Hivi ni kweli Wamarekani wamezawadiwa eneo la kigamboni in exchange na ujenzi wa Daraja?

Swali langu: Hivi iwapo watajenga hilo daraja, litakuwa ni kwa faida ya waTanzania au wa Marekani watakaokuwa ndio wakazi? Je, iwapo hao waMarekani watajenga, je wakazi waTanzania wataendelea kuvumiliwa nao kwenye majengo yao hafifu au watahamishwa?

Nawakilisha
 
Nimeamini wa mbili havai moja. Hawa watu tunawagawia tu bila hata kuombwa. Halafu tukishafanya hivyo tunajisifu kama tumelewa pombe
 
mAREKANI WAMENUNUA KIGAMBONI! KITAMBO HATA KAMA HUTAKI NDO HIVYO HII NDO SILIKALI!
 
kigamboni iko dar iko marekani au kujenga daraja ndo imekuwa ya kwao?
Kigamboni iko Dar es salaam Tanzania, Wamarekani wamemilikishwa maeneo, hatutarajii wawe na hati ya kumiliki na tuendelee kuyaita yetu. Swali ni kwamba, hilo daraja lililoombwa ni kwa manufaa ya nani atakayekuwa akiishi huko Kigamboni? Mmarekani au mTZ?
 
nawakaribisha sana nyumbani...WELCOME.zaidi ya yote wacha waweke military camp.
 
Hii siyo kupewa bali inaitwa development na hiyo kampuni inayofanya development wanaitwa developers. Hii ni kitu cha kawaida kwa Investor kuingia mkataba na serikali kuu au ya mikoa kufanya development. NSSF wanafanya development Kinyegeli, Mlimani city ni development na Botswana sasa kuna ubaya gani Investor wa marekani kufanya development!. Hii ni hali nzuri kwasababu serikali kazi yake si kujenga business bali kuweka hali nzuri kwa biashara kufanyika na pesa za serikali zitumike kwa maendeleo mengine ya kijamii kama barabara, afya, elimu n.k.
 
Wamezawadiwa? wanaipeleka wapi hiyo Kigamboni? au unataka kueleza nini?
 
Hivi ni kweli Wamarekani wamezawadiwa eneo la kigamboni in exchange na ujenzi wa Daraja?
Swali langu: Hivi iwapo watajenga hilo daraja, litakuwa ni kwa faida ya waTanzania au wa Marekani watakaokuwa ndio wakazi? Je, iwapo hao waMarekani watajenga, je wakazi waTanzania wataendelea kuvumiliwa nao kwenye majengo yao hafifu au watahamishwa?
Nawakilisha
mbona Waarabu wamepewa Loliondo au kwa vile Wamarekani si Waarabu?
 
Hii siyo kupewa bali inaitwa development na hiyo kampuni inayofanya development wanaitwa developers. Hii ni kitu cha kawaida kwa Investor kuingia mkataba na serikali kuu au ya mikoa kufanya development. NSSF wanafanya development Kinyegeli, Mlimani city ni development na Botswana sasa kuna ubaya gani Investor wa marekani kufanya development!. Hii ni hali nzuri kwasababu serikali kazi yake si kujenga business bali kuweka hali nzuri kwa biashara kufanyika na pesa za serikali zitumike kwa maendeleo mengine ya kijamii kama barabara, afya, elimu n.k.

Ahsante sana. Waelimishe wakurupukaji wa JF.
 
Hivi ni kweli Wamarekani wamezawadiwa eneo la kigamboni in exchange na ujenzi wa Daraja?
Swali langu: Hivi iwapo watajenga hilo daraja, litakuwa ni kwa faida ya waTanzania au wa Marekani watakaokuwa ndio wakazi? Je, iwapo hao waMarekani watajenga, je wakazi waTanzania wataendelea kuvumiliwa nao kwenye majengo yao hafifu au watahamishwa?
Nawakilisha

Nani alikuambia "tunawagawia", source yako ya "kuwagawia" umeitowa wapi? mbona mnakurupuka tu? wagawiwe waipeleke wapi?
 
Hiyo ndiyo Tanzania muijuayo. Subiri tutakapoona wahusika wakikutana na firing squad miaka michache ijayo, just as it happened in Iraq
 
Kuna mengi kati ya TZ na Marekani. Tutaambulia vyandarua, lakini kuna tetesi kuwa hata Uranium yetu wanaitaka kwa nguvu zote - sijui itakuwa in exchange na vyandarua!
 
Loliondo iko wapi? Uarabuni? wamepewa kivipi? au wamewekeza na wanalipia kodi zote zinazohusu uwekezaji? hebu fafanuwa.
Uwekezaji gani anafanya yule mwana mfalme kule Loliondo? Kuchukua wanyama wetu na kuwapeleka Uarabuni kunaitwa kuwekeza?
Kuwapiga marufuku Wamasai wetu katika maeneo waliyokuwa wanatumia ulishaji mifugo ni uwekezaji?
 
Kuna mada nyingine huwa zinadanya mtu u-question level ya uelewa wa baadhi ya member

Naomba ninyamaze
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom