Marando na watuhumiwa wa ufisadi

Viongozi wetu wanaogopa kuchangia hii sredi kuogopa kuonesha msimamo wao! Basi walau wahaidi "kuyafanyia kazi" maoni yetu yaishe!
 
Pamoja na kukatwa kodi zetu kiaina,mawakili wa serikali wanalipwa mishahara yao na kutetea wauwaji ambao kwa mazingira ya nje ya mahakama huonekana wanamakosa.
 
Sawa mpaka hapo tunakubaliana.

Vizuri

Hao mawakili wasiofungamana na chama chama chochote ni akina nani na wanapatikana wapi hapa Tanzania.

Chris Maina Peter ni mmoja wapo. Huyu sijawahi kumuona kwenye jukwaa lolote la kisiasa. Kuna jirani yangu wa zamani Darajani - Kapwete John..kaolewa siku hizi na sijui jina la mumewe. Kuna Agnes Sayi...huyu naye kaolewa sijui jina la mumewe. Wapo wa kutosha tu.

Sijui una maana gani na neno makada, lakini nimepitia listi ya viongozi wa Chadema na sijaliona jina la Marando.

Una kamusi hapo? Kama unayo angalia maana yake.

Sawa sawa hakuna miiko yoyote ya kitaaluma (ethics) aliyovunja Marando. Sana sana kaweka ushabiki pembeni kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake na hapa Marando yafaa apewe sifa.

Hakuna aliyewakataza kumpa sifa. Na sisi tunaomuona yeye ni mnafiki tuna haki hiyo.

Swali ni je, ungependa kuona vibaka wakichomwa moto ?

Hapana.

Lazima tuwe waangalifu sana tunapolitumia neno public opinion tusije tukawa tunaombea laws of the jungle. Kuna mtu kauliza, je mtuhumiwa wa mauaji asipate huduma ya daktari bingwa, mtuhumiwa wa ubakaji asipewe huduma yoyote na mtuhumiwa wa wizi asipewe ulinzi wa polisi. Wakili au jaji akiruhusu mahakama ya maoni ya watu kuzuia utoaji wa haki, huyo haswaa ndiye kakosa maadili ya kitaaluma. Je kwa hawa watuhumiwa kutetewa na Marando, kutazuia vipi kutendeka au kuonekana kutendewa kwa haki ?

Court of public opinion na implications zake kisiasa unaijua wewe?
 
NN ukishupalia kitu! Mbona ufisadi wa magamba mishipa haikutoki? Hivi bandugu FF = NN au? Hahahahaha!
 
Wana JF

Kwanza na-declare interest mm ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA, Hili swala la Marando kuwa wakili wa baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi km vile manji na mahalu litakuja kuwa na madhara makubwa sana hapo badae ktk harakati za chama za kuchua dola natambua kabisa ile ni professional yake na ni vigumu aache kazi aliyoisomea kwa muda mrefu, lakini kabla ya kuchua kazi lazima mtu ufanya client assessment.

Kwa kuwa ameamua kuwa ktk siasa na kufanikiwa kuwa mjumbe wa cc ya cdm ni wakati wake muafaka wa kuhakikisha kimoja kati ya professional yake na siasa hakuna kinacholeta madhara kwa kingine. Kwa hiyo moja ya criteria ya kutumika kwake kum-accept client iwe ni asiwe mtuhumiwa wa ufisadi. Nionavyo mm professional yake kwa sasa inaleta madhara ktk siasa si kwake tu bali kwa Chadema kwa ujumla coz ni vigumu sana mtu kupinga ufisadi majukwaani na kuukubali mahakamani na watu wote wakaamua kukuamini ww ni mpiganaji wa kweli wa ufisadi.

Swala kubwa la sisi wana-chadema tunalotakiwa kulielewa ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawawezi kutofautisha professional na siasa kiasi kwamba point tutakayoitumia kuuelezea uma ya kuwa hii ni siasa na hii ni professional haitaweza kuzaa matunda yeyote. Marando na uongozi wa juu ulitazame hili kwa mapana na marefu ili nguvu iliyokwisha tumika kukifikisha chama hapa isije kupotea kirahisi kisa mtu mmoja ambae ana uwezo wa kuchua kesi zingine na kuendelea na maisha.

Tujiulize swali dogo kwa mfano leo ROSTAM amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa KAGODA na marando akafanya km anavyofanya kwa wale wa EPA itakuwa sahihi? Au kuwatetea wa EPA itakuwa halali na kumtetea Rostam itakuwa haramu wakati wote ni mafisadi?

Nawasilisha

Wewe ni chadema tawi gani na kadi namba ngapi Mkuu? Ilinikusaidie husiyo ya fahamu!

Unaposema achague mteja kwa kuangalia aina ya kosa analoshtakiwa nalo sijui unajenga hoja yako juu ya nini? unataka kusema kuna makosa ya jinai ambayo CDM inayaunga mkono na yapo mbayo CDM haiyaungi mkono!


Kama ikiwa CDM haiungi mkono makosa yote ya jinai kwanini husiseme kuwa wanachama wa CDM wasimtete mtu yeyote anayeshtakiwa na serikali mahakamani? kama ikiwa vyama vya siasa vitafanya ujinga huo vyote nani atamtetea nani? and then! nini kitafuata au CDM ikichuwa madaraka itapereka mswada wa sheria kuomba mawakili wote wasiruhusiwe kuwa wanachama wa vyama vya siasa? Hii hoja ya ajabu sana.

Kwanini husiseme kuwa watuhumiwa waiperekwe Mahakamani wafungwe moja kwa moja na polisi? Maana Wakili ni sehemu ya Mahakama na kazi ya Wakili si kusaidia mtuhumiwa hasifungwe bali ni kuisaidia mahakama itende haki na itoe hukumu kwa mujibu wa sheria za nchni bila upendeleo wowote.


Haki ya watanzania wanaoshtakiwa ni haki ya kikatiba chama chochote ambacho kinafikia kupingana na haki hizo hakifai mbele ya Jamii kwa ujumla wake maana huwezi kuubiri haki na wakati mwingine ukaipinga, unachotaka wewe kifanyike ndio kinyume na mataraji ya wengi, maana kuitaka CDM ipingane na haki za msingi za watanzania walizopewa kwa mujibu wa sheria.
 
Wewe ni chadema tawi gani na kadi namba ngapi Mkuu? Ilinikusaidie husiyo ya fahamu!

Unaposema achague mteja kwa kuangalia aina ya kosa analoshtakiwa nalo sijui unajenga hoja yako juu ya nini? unataka kusema kuna makosa ya jinai ambayo CDM inayaunga mkono na yapo mbayo CDM haiyaungi mkono!


Kama ikiwa CDM haiungi mkono makosa yote ya jinai kwanini husiseme kuwa wanachama wa CDM wasimtete mtu yeyote anayeshtakiwa na serikali mahakamani? kama ikiwa vyama vya siasa vitafanya ujinga huo vyote nani atamtetea nani? and then! nini kitafuata au CDM ikichuwa madaraka itapereka mswada wa sheria kuomba mawakili wote wasiruhusiwe kuwa wanachama wa vyama vya siasa? Hii hoja ya ajabu sana.

Kwanini husiseme kuwa watuhumiwa waiperekwe Mahakamani wafungwe moja kwa moja na polisi? Maana Wakili ni sehemu ya Mahakama na kazi ya Wakili si kusaidia mtuhumiwa hasifungwe bali ni kuisaidia mahakama itende haki na itoe hukumu kwa mujibu wa sheria za nchni bila upendeleo wowote.


Haki ya watanzania wanaoshtakiwa ni haki ya kikatiba chama chochote ambacho kinafikia kupingana na haki hizo hakifai mbele ya Jamii kwa ujumla wake maana huwezi kuubiri haki na wakati mwingine ukaipinga, unachotaka wewe kifanyike ndio kinyume na mataraji ya wengi, maana kuitaka CDM ipingane na haki za msingi za watanzania walizopewa kwa mujibu wa sheria.

Hoja yako bado ndugu yangu,

Hakuna aliyesema wanachama wa CHADEMA ambao ni mawakili wasitetee watuhumiwa wenye kesi za jinai...Hakuna mtu anayeleta hoja hiyo. Labda wewe ndiye unaianzisha.

Tatizo ni mwanachama wa CHADEMA, kada na kiongozi wa juu (Mabere Marando), ambaye amekuwa mstari wa mbeke kupinga ufisadi kiasi cha kuwataja mafisadi hadharani (naamini unakukumbuka kasheshe ya Jangwani mwaka jana) na halafu huyo asimame mahakamani kuwatetea wateja wanaokabiliwa na kesi za ufisadi. Hii haikubaliki kabisa hata kama hajavunja sheria yoyote au maadili ya kazi yake ya uwakili.

Wananchi wanajua kuwa mafisadi ni sawa na mumiani (blood suckers) na hawawezi kumwelewa mtu anayewatetea hata kama nyie wasomi mnamulewa.

Ila kama hamtaki kuwasikiliza wananchi wa kawaida basi msubiri siku ya siku watawaeleza kwa sauti ambayo mtaielewa hata kama hamtaipenda!!
 
Nimefuatilia mjadala na naona kuna mchanganyiko wa mambo ambayo yaweza kuwa hatuyaelewi au tunayatafsiri vibaya.
Kwanza nakubaliana na Kobello kuwa kazi ya wakili(stand to be corrected) ni kusimamia haki ili itendeke (Fair trial) hata kama mtuhumiwa amethibitika kutenda kosa ili mambo mengine ya kisheria yazingatiwe katika kutoa adhabu.

Mawakili ni weledi sana wa sheria na kama taaluma zingine wanongozwa na sheria, principles na ethics. Moja kati ya Ethics zao ni kulinda public interest iwe katika kikundi au mtu binafsi kwa kuhakikisha haki inatendeka kwa kila raia anayestahili bila kujali itikadi ya kisiasa ya wakili au mtuhumiwa kama wanavyofanya madaktari hospitali.

Profesa Sarungi mtaalamu wa upasuaji alikuwa mkuu wa mkoa wa Pwani, Mbunge mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya CCM na kada muhimu. Kuna nyakati alilazimika kutumia taaluma yake katika hospitali ya tumbi pale kulipotokea matukio kama ya ajali, au kuhudumia majeruhi wanaotokana na uhalifu kama ujambazi, wizi, fumanizi n.k.

Sarungi hakufanya kazi kama kada wa chama bali mtaalamu anayelinda kiapo chake cha udaktari cha kuhudumia binadamu bila kuangalia jambo lolote bali uninadamu na utabibu kwa kutenda haki.
Court of public opinion ilimhukumu kama mtu, daktari na kiongozi anayejali na kuenzi taaluma yake kwa kuthamini utu.

Popote duniani mtuhumiwa bila kujali wajihi, hadhi au nafasi yake katika jamii analindwa na haki ya kisheria. Wauaji wa Albino ambao wengine hawamudu hata kununua mkate, bado wanahaki ya kuwekewa uwakili na cha kushangaza zaidi ni kuwa mawakili wao wanalipwa na serikali ambayo ni kodi yangu mimi na wewe. Kwa maneno mengine, tunalaani mauaji ya albino na wakati huo huo tunatoa pesa za kuwawekea mawakili.
Court of public opinion inapaswa kutusuta sisi tunaolipia gharama za kumuokoa muuaji au kabla ya kumlaumu wakili.

Tunapoiba pesa za halmashauri au wizara na kisha kuwaambia mawakili siri zetu na wao kututetea hata kama wanajua tumeiba au tumefanya ujambazi, court of public opinion inatupa haki kama ambavyo inapaswa kutoa haki kwa mtuhumiwa mwingine wa fumanizi au ufisadi.

Ni jambo gumu kuwa na mtu asiyefungamana na itikadi ya kisiasa hasa katika kada ya wasomi.
Wapo watakaosema hawafungamani kama ninavyoweza kusema lakini ukweli unabaki mioyoni mwao na wala hatupaswi kusadiki kauli zao.

Mfano, sheria inakataza viongozi wa majeshi kuwa washabiki wa vyama vya siasa. Mwaka jana tumeona kamanda mkubwa wa polisi aliyestaafu miezi 3 tu nakuchukua form za ubunge. Hivi huyu tunaweza kusadiki kuwa alikielewa chama chake katika miezi 3 tu hadi kufikia hatua ya kuchukua form za ubunge kama si kuwa alikuwa kada asiyesema? Sasa tutasemaje tuwe na mawakili neutral, kwa evidence gani.

Marando anapokuwa mahakamani anasimamia haki kama wakili na mtaalamu kwa mtuhumiwa na sio mhalifu na si kama ni mwakilishi wa Chama cha kisiasa kwa mantiki ile ile ambayo Profesa Sarungi anakuwa theatre akimshona nyuzi jambazi.

Profesa kwa wakati ule si mkuu wa mkoa au kada wa chama bali daktari aliyekula kiapo kutoa huduma ya haki kwa binadamu.
Ikifika hapo lazima tujiulize kwanini kuna double standard?
Why court of public opinion is not applicable across the board!

Kisiasa ni kweli hili jambo lina political ramifications hasa kwa nchi zenye wananchi ambao ufahamu wao una limit. Kibaya zaidi ni kuwa hata sisi tunaopaswa kuwaambia kuwa kuna politics na professionalism tunaelekea kuwashadidia waelewe tofauti.Je huku si kuendelea kuwapotosha!!
Tatizo lingine ni sisi kuchomeka siasa kwenye kila jambo hata yale ya kitaaluma na kitaalamu ndiyo maana hata mambo ya megawatts, resuscitation, economy, tumewaachia wao wapange na wasaini mikataba. Sio engineers, doctors au economists.

Tumeruhusu na kukubali wanasiasa kuchomeka siasa katika taaluma na sasa tuneshaingia huko haya ndiyo matokeo yake.

Tunadhima ya kuuambia umma wetu uliochanganywa na siasa za Nape Nnauye kuwa kuwa, alichosema Nape ni political mudsling and confusion, ukweli ni kuwa Marando kama professional hajakiuka Laws, regulations, principles au ethics kwa namna yoyote na kwamba court of public opionion imhukumu kwa kauli na matendo yake kisiasa katika chama chake bila kuchanganya na utaalamu wake kama vile court of public opinion ilivyomuelewa profesa Sarungi alipokuwa ana repea mifupa na kuzuia damu isivuje kwa majambazi.

Ni maoni yangu senti sumuni.
 
Role ya Marando ni kubwa sana hasa upande wa kotini kwa maslahi ya wapinzani wote nchini. Siku zote amekuwa akisema hakubaliani na aina ya watu wanaoletwa kotini kwa tuhuma za ufisadi kwakuwa ni dagaa tu, mapapa hayaletwi. Hivi karibuni aliulizwa swali hilo kwenye mdahalo na akina Nape akaeleza hivyo hivyo. Kwa maneno rahisi ni kuwa washitakiwa wa ufisadi wanabambikwa kesi. Fikiria kubambikwa kesi na machungu yake? Ulishawahi kufuatilia au hata kuiskia kesi ya Mahalu? Umeshaskia mashahidi wanaotakiwa Mahakamani kumtetea mshitakiwa? Dogo, TAFAKARI!
yah, umejibu sahihi kabisa
 
Hata mm nimekuwa najiuliza maswali mengi sana kuhusu huyu bw. Marando. Anachukua majukumu ya kuwatetea mafisadi mahakamani lakini anakwenda kuwasema majukwaani. Yaani hii inawachanganya sana watu ambao tayari walishaanza kujenga imani na CHADEMA. Kama Dr. Slaa kwa bahati atapita hapa atolee ufafanuzi suala hili akiwa kama Katibu mkuu wa chama.
nimependa avatar yako
 
wewe jamaa .... hivi ukiwa kama daktari halafu mwizi akaletwa hospitalini ameumizwa vibaya je hautamtibu kwasababu ni mwizi ?
tofautisha kati ya daktari na mwanasheria; unapozungumzia daktari unazungumzia uhai wa mtu, lakini c dhani kama unapomtetea fisadi unaokoa uhai wake! kwamba usipomtetea atakufa! kilichompeleka huko marando ni njaa, sasa ili kuinusuru chadema inabidi achagua kati ya siasa au kuwatetea mafisadi! kinyume cha hapo chadema inabidi ifyate mkia kuzungumzia mafisadi, maana huwezi kukipinga kitu ambacho mwenyewe unakitetea huo utakuwa ni unafiki! yaani itakuwa ni sawa na kusema nyama ya kiti ni haramu lakini mchuzi wake unakunywa!!!!!!!!!!!
 
Mimi nina kaswali kadogo tu kwa mtoa mada, je ni kosa kumtetea mtuhumiwa ? Kama jibu ni hapana, wewe ungetaka hao watuhumiwa watetewe na mawakili wa aina gani au wa chama gani ? Je, kama swala la ethics linazingatiwa katika kuwatetea watuhumiwa, unataka kusema kuwa wale mawakili wasio na ethics ndio wajitokeze kuwatetea ? Na kama ni hivyo hao mawakili wenye sifa za kukosa ethics ni mawakili wa namna gani na ni kama yupi kwa mfano hapa Tanzania.

Sasa wakili kama tayari anayo sifa ya kutokuwa na ethics, kwa nini na yeye asifunguliwe kesi na kama itakuwa hivyo yeye mwenyewe atatetewa na wakili wa aina gani ? Na mwisho hebu tupe mwanga kidogo tu, Marando ungependekeza awatetee wahalifu wa aina gani kwani uhalifu si ni uhalifu tu mbele ya sheria ? Labda mimi ni mzito na sio great thinker lakini kwa kawaida ninavyoelewa, kosa linavyozidi kuwa kubwa ndivyo wakili mashuhuri na makini zaidi anavyohitajika kutoa utetezi.

Je, kwa mfano tu, mtuhumiwa wa kosa kubwa kama la uuaji hastahili kutetewa na Marando kwa sababu Chadema inalaani mauaji ?
na mimi naomba nikuulize kaswali kadogo; hivi mh. marando anapokwenda kuwatetea hawa mafisadi anapoulizwa na hakimu kuwa watuhumiwa wake ni wezi, wameiba pesa za epa kwa mfano; huwa anajibu nn? ndio au hapana? yaani kwa niaba ya watuhumiwa marando huwa anakubali au huzikana tuhuma?
 
kwa uelewa wako ni &lt;span style=&quot;font-family: &amp;amp;quot&quot;&gt;v&lt;/span&gt;igumu sana kuweza kutambua professionalism and its ethical codes o&lt;span style=&quot;font-family: &amp;amp;quot&quot;&gt;f&lt;/span&gt; conduct ...... kazi ya wakili ni kumtetea mhali&lt;span style=&quot;font-family: &amp;amp;quot&quot;&gt;f&lt;/span&gt;u na sio kuhukumu yupi ni mhali&lt;span style=&quot;font-family: &amp;amp;quot&quot;&gt;f&lt;/span&gt;u na yupi si mhali&lt;span style=&quot;font-family: &amp;amp;quot&quot;&gt;f&lt;/span&gt;u .... kwani hii kazi ya wakili ni kutetea watu wasio na makosa? ... silly mind ! .... as well daktari jukumu lake ni kutoa tiba kwa mgonjwa pasipo kuangalia ameathirika &lt;span style=&quot;font-family: &amp;amp;quot&quot;&gt;v&lt;/span&gt;ipi na ugonjwa wake .... your thinking capacity is very low &lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
hata wewe ukifanya uhalifu sasa hivi ... katiba inasema you have the right for an attorney (legal representative ) na serikali pia ina jukumu la kugharamia wakili wa kukutetea&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
kwa hiyo chadema na uongozi wote haioni hili na kukemea ni wewe tu mwenye narrow mind unaeona ?&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
try to be analytical ....
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Chukulia wewe in lawyer mzuri sana, na kuna kibaka mmoja amembaka binti yako na kafikishwa mahakamani. Sasa anataka kukukodi umtetee. Je utamtetea?
 
Hapa napata shida kidogo kuelewa, Dr Slaa, anapambana kupiga vita ufisadi halafu ndani ya chama chake anatokea mtu anawatetea Mafisadi kisa eti Uwakili ni taaluma hana haki ya kuwatetea!
Kama kweli ana dhamira ya dhati angejitoa kwenye siasa aendelee na kazi yake ya kutetea Mafisadi kama kuna watu watahoji chochote
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Chukulia wewe in lawyer mzuri sana, na kuna kibaka mmoja amembaka binti yako na kafikishwa mahakamani. Sasa anataka kukukodi umtetee. Je utamtetea?

Sawa kabisa mkuu,

Hata mimi niliwauliza hao watu wa sheria na maadili ya uwakili swali kama hilo.....Unaweza kumtetea mtu ambaye ana tuhuma za kumuua baba yako?????
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Chukulia wewe in lawyer mzuri sana, na kuna kibaka mmoja amembaka binti yako na kafikishwa mahakamani. Sasa anataka kukukodi umtetee. Je utamtetea?

kamwe mshitaki hawezi kuwa mshitakiwa naturally (plaintiff as defendant ), hiyo haitakuwa kesi
 
kamwe mshitaki hawezi kuwa mshitakiwa naturally (plaintiff as defendant ), hiyo haitakuwa kesi
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Mshitaki ni Jamhuri na sio wewe. Binti yako anaweza kuwa kabakwa chuoni.
 
hoja yako ni nzuri sana na ina tahadhali na mtazamo mkubwa sana wa mbele! ninachokiona hapa kuna wana chadema wamekua wavivu wa kufikiria sana! hawaoni hatari ya kuichafua chadema jukwani kupitia hili analolifanya marando! ni bahati mbaya sana wanachadema wameiweka akili yao kw aupande wa kishabiki kwa kila jambo! hili la marando linatia doa kwa chadema katika vita yake ya kupinga ufisadi! ni doa!
 
Sawa kabisa mkuu,

Hata mimi niliwauliza hao watu wa sheria na maadili ya uwakili swali kama hilo.....Unaweza kumtetea mtu ambaye ana tuhuma za kumuua baba yako?????
ni simple logic too! unahubiri la kupinga ufisadi kesho unaenda kisutu kuwatetea mafisadi!
 
Back
Top Bottom