Marais wastaafu wasishiriki kampeni za uchaguzi ndogo

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040
mwananchilogo.jpg
KATIKA hali isiyo ya kawaida, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa amejikuta akiingia katika siasa chafu za uchaguzi baada ya kutoa matamshi yaliyomfanya ashambuliwe kwa maneno makali na kejeli kutoka vyama vya upinzani na watu wa kada mbalimbali.

Hali hii ilijitokeza baada ya Mkapa kusema wakati wa uzinduzi wa kampeni cha CCM katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki Machi 12, mwaka huu kwamba Vecent Nyerere hana undugu na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere. Kauli hiyo ilijibiwa na Madaraka Nyerere ambaye ni mtoto wa marehemu Nyerere aliyethibitisha kuwa Vicent ni mtoto wa baba yao mdogo hivyo ni ndugu yao kabisa.

Baada ya ufafanuzi Madaraka, Vicent alijibu kwa kumshangaa Mkapa huku akimkebehi kwa kauli yake iliyoonesha wazi kuwa alikosea kutamka maneno hayo hadharani, jambo ambalo lilionyesha kuwa hakujua ukweli kuhusu uhusiano wa Vecent na Marehemu Baba wa Taifa.

Si hivyo tu, rais mstaafu huyo ameshambuliwa kwenye majukwaa ya kampeni za Chadema na nje ya jukwaa kutoka wa wanaharakati na wadau mbalimbali hapa nchini ambao kwa nyakati tofauti walishangaa ni kwa nini aliingia katika siasa hizo chafu ambazo zimemshushia hadhi na heshima aliyojijengea katika nchi hii kutokana na mambo mazuri aliyoifanyia Tanzania kwa kipindi cha miaka 10 alipokuwa rais.

Tunajua Mkapa bado ni mwanachama hai wa CCM, ambaye anaheshimika sana kwani mbali ya kuwa Rais, alikuwa Mwenyekiti wa chama hadi alipomaliza kipindi chake cha urais, hivyo anastahili kukisaidia chama chake kinapokuwa katika kampeni mbalimbali za uchaguzi.

Lakini je, katika nafasi ya rais aliyofikia katika uongozi wa nchi hii anatikiwa kushiriki kampeni? Je, ni halali rais mstaafu anayeheshimiwa apelekwe hata kwenye kampeni za uchaguzi mdogo jimboni ambao siasa zake mara nyingi ni za kupakana matope badala ya kunadi sera za kuwakomboa wananchi?

Kwa bahati mbaya katika chaguzi mbili alizoshiriki Mkapa(wa Igunga mwishoni mwa mwaka jana na huu wa Arumeru Mashariki), alishambuliwa na kukashifiwa kwa maneno machafu ya siasa za uchaguzi wa ngazi hiyo, ambayo kwetu tunaona kuwa anashushiwa hadhi.

Kilichojitokeza kwamba, Mkapa alitumia propaganda ambazo ni za chini ikilinganishwa na nafasi, ufahamu, hekima na heshima yake. Tunadhani alifanya hivyo kwa sababu alitaka kufikisha ujumbe kwa mashabiki na wapiga kura kwa lugha aliyoamini atakubalika kutokana na vuguvugu la siasa za uchaguzi katika ngazi hiyo kutawaliwa na maneno ya kuchafuana, kama wanavyoropoka viongozi wengine katika kampeni zinazoendelea sasa huko Arumeru Mashariki.

Kuonyesha kuwa Mkapa hakustahili kusema hayo, kauli hiyo ingetolewa na mtu mwingine kama ambavyo viongozi wengine wanavyosema, hakuna ambaye angeshtuka wala kushangaa na kuanza kumshambulia.

Hiyo inadhihirisha kwamba, Mkapa kama rais mstaafu amewekwa kwenye nafasi ya juu ambayo hategemewi kusema maneno rahisi kama hayo, bali walitegemea angemwaga sera za chama chake.

Kutokana na hali hiyo, sisi tunaona kwamba, marais wastaafu kushiriki katika kampeni za uchaguzi mdogo ni kuwadhalilisha na zaidi ya hapo, hao ni viongozi wa kitaifa ambao kwa nafasi yao wanabeba jukumu la kuwa walezi na washauri wa kitaifa yanapotokea mambo magumu; ndiyo maana CCM ilishaamua kuwaondolea majukumu mengine katika chama na kubakia kuwa wazee na washauri wa chama, ili wanapoombwa kutoa ushauri na kufanya usuluhishi wasitiliwe shaka na upande wowote.

Hata kama chama chao kinawahitaji wakati wa kampeni hizo, isiwe kwa kupanda jukwaani bali wasaidie kwa kuwashauri na kuwapa mbinu za ushindi kuliko kupanda jukwaani ambapo kila analosema hupewa uzito wa juu na kisha kumhusisha nalo moja kwa moja.

Kwa sababu hiyo basi, tunashauri kwamba marais wastaafu wasitumiwe kwenye kampeni za uchaguzi hasa ngazi ua uchaguzi mdogo ili kulinda heshima yao.
Marais wastaafu wasishiriki kampeni za uchaguzi ndogo

 
Arumeru Mkapa alipaswa kuongelea masuala ya msingi ya jumla ikiwemo kuhamasisha kampeni za kistaarabu na misingi ya demokrasia kwa ujumla.
Alipaswa kuongea kama mtu wa watanzania pamoja na kuwa ni mtu wa CCM.
Alipaswa kujitambua kuwa yeye ni Rais mstaafu.
Mkapa anapaswa kusaidiwa kujitambua.
 
Wataacha kumtumia wakati yeye ndo anaonekana walao afadhali kuliko wote ccm japo siyo
 
Nimerudi. Mi sidhani kama ni busara kwa marais wastaafu kutoshiriki kampeni za vyama vyao katika chaguzi ndogo. Na siyo sahihi kusema kwamba chaguzi ndogo zina mazingira tofauti ya undeshaji wa kampeni ukilinganisha na kampeni za uchaguzi mkuu. Kwa uelewa wangu ni kuwa chaguzi zote zinaensheshwa kwa misingi na taratibu zilizowekwa na tume ya uchaguzi. Kama kuna ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi katika hizi chaguzi ndogo, tume inapaswa kuchukua hatua staili. Rais mstaafu kutoshiriki kwenye kampeni za chaguzi ndogo hakuwezi kuondoa kasoro (kama zipo). Mi nadhani mzee mkapa alitamka hayo maneno kwa makusudi na pengine pia ameanza kuchuja kisiasa.
 
Mkuu mimi nakubaliana na wewe kuhusu wataafu wetu wa ngazi za juu sio tu marais bali hata makamu na waziri mkuu, hawa kwa mujibu wa katiba iliyopo wanastahili kilipwa stahilki mbalimbali ili kujikimu kimahisha, malipo haya ni kodi zetu sisi wananchi (wapenzi wa CCM, CUF, NRA etc) naamini si haki na sahihi kwetu wengine ambao si CCM kumlipia mtu ISHI yake halafu aje kusimama kututukana/kutupinga. Naamini itakuwa sahihi sheria ikitamka wazi kwamba kama bado wana hamu ya siasa za majukwaani badala ya kupumzika kama ambavyo wanatakiwa,basi wasistahili kulipwa- Walipwe wale tu wanaopumzika kweli
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom