Sokomoko
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,915
- 127
Marafiki walimuonya Kikwete
Ansbert Ngurumo
MWISHONI mwa mwaka 2005, baada ya Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani, baadhi ya watu waliokuwa karibu naye kikazi na kifamilia walimuonya.
Walimpa onyo katika mfumo wa ushauri kwa kuogopa kumuonya rais; kwa maana baadhi yao walikuwa wateule wake na wasaidizi wake wa karibu, jambo lililowafanya kupima vema kila kauli waliyompa mkuu wao wa kazi.
Ushauri waliompa rais ulihusu maswahiba wake wakuu, ambao baadhi ni wafanyabiashara maarufu, ambao walifikia hatua ya kutoa fedha kuchangia kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizompa Kikwete ushindi mnono.
Walimwambia rais afanye awezavyo kuwaweka mbali marafiki zake katika masuala ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne, kwa maelezo kwamba: Malengo na masilahi yao ya kisiasa yangeweza kuingiliana na kutuingiza kwenye matatizo.
Baada ya kuwasikiliza, Rais Kikwete alifanya mambo mawili. Kwanza, alifuta mpango wa kuwateua serikalini. Pili, hakukubaliana na ushauri wa kuwaweka baadhi yao mbali na serikali.
Hadi mapema mwaka huu lilipozuka sakata la ufisadi wa Richmond, mmoja wa maswahiba wake alikuwa mmoja wa washauri wake wakuu wasio rasmi, na anasemekana alikuwa karibu naye kuliko hata baadhi ya mawaziri.
Mmoja wa mawaziri wa Kikwete wakati huo aliwahi kusema mahali fulani kwamba wapo baadhi ya viongozi wenzake ambao wakitaka kuvuka utaratibu wa kimangimeza wa kuomba miadi ya kuonana na rais, wanamtumia swahiba wake huyo.
Na mambo ya Richmond yalipozidi kuwa magumu, zikaanza kusikika tetesi kutoka kwa watu wake wa karibu kwamba ndiye aliyeileta kampuni hiyo feki na kuitetea kwa mkuu wa nchi.
Maelezo haya yalisaidia baadaye kueleza kwa nini Rais Kikwete alishikwa na kigugumizi cha kushughulikia wezi wa EPA na Richmond; na kwa nini amekuwa akitumia mifumo ya chama chake na serikali kujaribu kuwasafisha na kuwalinda watuhumiwa.
Wanaokumbuka majibu yake aliposhauriwa amtose rafiki yake mwaka 2006, wanasema rais alingaka kwamba asingeweza kufanya hivyo, kwani Si utu kumweka mbali, kwani ametumia pesa zake nyingi kutusaidia sana katika mchakato mzima wa kampeni na uchaguzi
Utu huu ambao rais aliusisitiza wakati ule, umemfunga mikono katika kuchukua hatua dhidi ya wezi wa EPA na Richmond licha ya mamlaka makubwa aliyonayo. Na baadhi ya watuhumiwa, akiwamo swahiba wake huyu, wanadaiwa kumtisha rais kwa kusambaza maneno ya chini chini kwamba akitugusa tu, naye tunamvua nguo.
Hata sasa, ambapo inajulikana wazi kwamba pesa hizi zilizowasaidia sana hazikuwa za wafanyabiashara hao, bali ni sehemu ya pesa zile zinazohusishwa na miradi na wizi huo, serikali imeshindwa kuchukua hatua kali, ikisingizia inaogopa kuvunja haki za binadamu.
Inashangaza kwamba binadamu wanaolindiwa haki zao hawazidi 10, huku binadamu wanaodhulumiwa haki zao ni Watanzania milioni 40 wanaoathirika kwa wizi huo na matumizi mengine mabaya ya madaraka.
Waliojua mazingira hayo mapema ndio walikuwa wa kwanza kutilia shaka hatua za serikali kuunda tume ya kuchunguza ufisadi wa EPA.
Ndio waliokuwa wanatilia shaka muda mrefu wa tume hiyo kufanya kazi, huku ikiundwa na baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi mwingine, uliowahusu watu wale wale.
Walijua serikali inafanya mchezo mchafu wa kuchezea akili za Watanzania. Na kwa sababu hiyo, ndiyo maana wapo watu ambao wamekuwa wakitamka bila woga kwamba serikali ya wezi haiwezi kushughulikia wezi wale wale walioiweka madarakani!
Baadhi yetu tulipotilia shaka uwezo, nia na umakini wa rais katika suala hili tulishauriwa na baadhi ya wasaidizi na mashabiki wake kwamba tumpe muda. Tumempa muda, ameutumia vibaya.
Sasa baada ya hotuba yake ndefu bungeni wiki iliyopita, tunaweza kujivuna kwa kuwa na viongozi wa aina hii? Tunaweza kumnasua Kikwete kwenye ufisadi wa EPA na Richmond? Je, sasa tunaelewa vema kinachozuia mikono yake kushika rungu tulilomkabidhi kuwatwanga wahalifu?
Jambo moja ni dhahiri. Rais bado anatetea utu ule ule ambao washauri wake walimwambia auweke pembeni mapema, akakataa.
Kwangu, hii ndiyo tafsiri ya haraka ya kauli ya Rais Kikwete bungeni alipodai serikali inashindwa kuchukua hatua kali dhidi ya mafisadi kwa kuogopa kuvunja haki za binadamu.
Ndiyo! Kwake, hawa ndio binadamu. Hawa ndio wenye haki zinazopaswa kulindwa na Serikali ya Awamu ya Nne. Haki za Watanzania milioni 40 hazimo miongoni mwa haki za binadamu!
Wala tusijiulize sana kwa nini serikali inayojidai kuwa ya kasi mpya inatumia miezi kuchunguza ufisadi ulio wazi, halafu inakuja na matamko yasiyo na mashiko! Hatuna sababu ya kushangaa kwa nini hata baada ya nusu mwaka, inashindwa kutekeleza mapendezo ya kamati ya Bunge kuhusu ufisadi wa Richmond.
Hii ni serikali goigoi ya kasi mpya, ambayo inasifika kwa kuomba ipewe muda, huku nayo ikitoa muda kwa wasiostahili; tangu pale Rais Kikwete aliposema anawafahamu wala rushwa, lakini anawapa muda wajirekebishe.
Ilikuwa mwaka 2006. Leo, miaka miwili baadaye, bado hajaridhika kama wamejirekebisha. Analinda haki zao!
Tusisahau kwamba ni huyu huyu ambaye katika mwaka huo huo (2006) alijitapa jinsi ambavyo anataka kuunda mabilionea wa Kitanzania.
Bila shaka si kwa mabilioni yale yaliyochotwa CRDB na kusambazwa mikoani kwa jina la Mabilioni ya Kikwete!
Hayo yameshasahaulika.
Mabilionea waliodhamiriwa ndio hawa, hawa wa EPA na Richmond, wafadhili wa serikali. Halafu tunatarajia serkali ile ile itoe tamko kali na kuchukua hatua kali dhidi yao?
Ikumbukwe kuwa serikali imetoa matamko juu ya EPA na Richmond baada ya muda mrefu wa maandalizi ya kutosha na upotoshaji wa hali ya juu kuhusu ufisadi unaoikabili serikali.
Wamejaribu, lakini bado wameshindwa kutuhadaa kuhalalisha wizi wao. Hapo ndipo uwezo wa upotoshaji wa serikali ulipoishia.
Na huu ni ushahidi mwingine kwamba tunaongozwa na watu wenye uwezo mdogo sana au wasio makini kabisa, au wasioitakia mema nchi hii!
Wafanye watakavyo, watutenge katika makundi ya binadamu na wasio binadamu. Rais aendelee kuwa katika kuchukua hatua.
Mwisho wa yote, ajue kwamba tunatambua kuwa anafanya hivyo makusudi, kwa sababu alipuuza ushauri aliopewa. Alionywa mapema, akapuuza. Haya ndiyo matokeo yake.
ansbertn@yahoo.com
+447853850425
www.ngurumo.blogspot.com
Ansbert Ngurumo
MWISHONI mwa mwaka 2005, baada ya Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani, baadhi ya watu waliokuwa karibu naye kikazi na kifamilia walimuonya.
Walimpa onyo katika mfumo wa ushauri kwa kuogopa kumuonya rais; kwa maana baadhi yao walikuwa wateule wake na wasaidizi wake wa karibu, jambo lililowafanya kupima vema kila kauli waliyompa mkuu wao wa kazi.
Ushauri waliompa rais ulihusu maswahiba wake wakuu, ambao baadhi ni wafanyabiashara maarufu, ambao walifikia hatua ya kutoa fedha kuchangia kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizompa Kikwete ushindi mnono.
Walimwambia rais afanye awezavyo kuwaweka mbali marafiki zake katika masuala ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne, kwa maelezo kwamba: Malengo na masilahi yao ya kisiasa yangeweza kuingiliana na kutuingiza kwenye matatizo.
Baada ya kuwasikiliza, Rais Kikwete alifanya mambo mawili. Kwanza, alifuta mpango wa kuwateua serikalini. Pili, hakukubaliana na ushauri wa kuwaweka baadhi yao mbali na serikali.
Hadi mapema mwaka huu lilipozuka sakata la ufisadi wa Richmond, mmoja wa maswahiba wake alikuwa mmoja wa washauri wake wakuu wasio rasmi, na anasemekana alikuwa karibu naye kuliko hata baadhi ya mawaziri.
Mmoja wa mawaziri wa Kikwete wakati huo aliwahi kusema mahali fulani kwamba wapo baadhi ya viongozi wenzake ambao wakitaka kuvuka utaratibu wa kimangimeza wa kuomba miadi ya kuonana na rais, wanamtumia swahiba wake huyo.
Na mambo ya Richmond yalipozidi kuwa magumu, zikaanza kusikika tetesi kutoka kwa watu wake wa karibu kwamba ndiye aliyeileta kampuni hiyo feki na kuitetea kwa mkuu wa nchi.
Maelezo haya yalisaidia baadaye kueleza kwa nini Rais Kikwete alishikwa na kigugumizi cha kushughulikia wezi wa EPA na Richmond; na kwa nini amekuwa akitumia mifumo ya chama chake na serikali kujaribu kuwasafisha na kuwalinda watuhumiwa.
Wanaokumbuka majibu yake aliposhauriwa amtose rafiki yake mwaka 2006, wanasema rais alingaka kwamba asingeweza kufanya hivyo, kwani Si utu kumweka mbali, kwani ametumia pesa zake nyingi kutusaidia sana katika mchakato mzima wa kampeni na uchaguzi
Utu huu ambao rais aliusisitiza wakati ule, umemfunga mikono katika kuchukua hatua dhidi ya wezi wa EPA na Richmond licha ya mamlaka makubwa aliyonayo. Na baadhi ya watuhumiwa, akiwamo swahiba wake huyu, wanadaiwa kumtisha rais kwa kusambaza maneno ya chini chini kwamba akitugusa tu, naye tunamvua nguo.
Hata sasa, ambapo inajulikana wazi kwamba pesa hizi zilizowasaidia sana hazikuwa za wafanyabiashara hao, bali ni sehemu ya pesa zile zinazohusishwa na miradi na wizi huo, serikali imeshindwa kuchukua hatua kali, ikisingizia inaogopa kuvunja haki za binadamu.
Inashangaza kwamba binadamu wanaolindiwa haki zao hawazidi 10, huku binadamu wanaodhulumiwa haki zao ni Watanzania milioni 40 wanaoathirika kwa wizi huo na matumizi mengine mabaya ya madaraka.
Waliojua mazingira hayo mapema ndio walikuwa wa kwanza kutilia shaka hatua za serikali kuunda tume ya kuchunguza ufisadi wa EPA.
Ndio waliokuwa wanatilia shaka muda mrefu wa tume hiyo kufanya kazi, huku ikiundwa na baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi mwingine, uliowahusu watu wale wale.
Walijua serikali inafanya mchezo mchafu wa kuchezea akili za Watanzania. Na kwa sababu hiyo, ndiyo maana wapo watu ambao wamekuwa wakitamka bila woga kwamba serikali ya wezi haiwezi kushughulikia wezi wale wale walioiweka madarakani!
Baadhi yetu tulipotilia shaka uwezo, nia na umakini wa rais katika suala hili tulishauriwa na baadhi ya wasaidizi na mashabiki wake kwamba tumpe muda. Tumempa muda, ameutumia vibaya.
Sasa baada ya hotuba yake ndefu bungeni wiki iliyopita, tunaweza kujivuna kwa kuwa na viongozi wa aina hii? Tunaweza kumnasua Kikwete kwenye ufisadi wa EPA na Richmond? Je, sasa tunaelewa vema kinachozuia mikono yake kushika rungu tulilomkabidhi kuwatwanga wahalifu?
Jambo moja ni dhahiri. Rais bado anatetea utu ule ule ambao washauri wake walimwambia auweke pembeni mapema, akakataa.
Kwangu, hii ndiyo tafsiri ya haraka ya kauli ya Rais Kikwete bungeni alipodai serikali inashindwa kuchukua hatua kali dhidi ya mafisadi kwa kuogopa kuvunja haki za binadamu.
Ndiyo! Kwake, hawa ndio binadamu. Hawa ndio wenye haki zinazopaswa kulindwa na Serikali ya Awamu ya Nne. Haki za Watanzania milioni 40 hazimo miongoni mwa haki za binadamu!
Wala tusijiulize sana kwa nini serikali inayojidai kuwa ya kasi mpya inatumia miezi kuchunguza ufisadi ulio wazi, halafu inakuja na matamko yasiyo na mashiko! Hatuna sababu ya kushangaa kwa nini hata baada ya nusu mwaka, inashindwa kutekeleza mapendezo ya kamati ya Bunge kuhusu ufisadi wa Richmond.
Hii ni serikali goigoi ya kasi mpya, ambayo inasifika kwa kuomba ipewe muda, huku nayo ikitoa muda kwa wasiostahili; tangu pale Rais Kikwete aliposema anawafahamu wala rushwa, lakini anawapa muda wajirekebishe.
Ilikuwa mwaka 2006. Leo, miaka miwili baadaye, bado hajaridhika kama wamejirekebisha. Analinda haki zao!
Tusisahau kwamba ni huyu huyu ambaye katika mwaka huo huo (2006) alijitapa jinsi ambavyo anataka kuunda mabilionea wa Kitanzania.
Bila shaka si kwa mabilioni yale yaliyochotwa CRDB na kusambazwa mikoani kwa jina la Mabilioni ya Kikwete!
Hayo yameshasahaulika.
Mabilionea waliodhamiriwa ndio hawa, hawa wa EPA na Richmond, wafadhili wa serikali. Halafu tunatarajia serkali ile ile itoe tamko kali na kuchukua hatua kali dhidi yao?
Ikumbukwe kuwa serikali imetoa matamko juu ya EPA na Richmond baada ya muda mrefu wa maandalizi ya kutosha na upotoshaji wa hali ya juu kuhusu ufisadi unaoikabili serikali.
Wamejaribu, lakini bado wameshindwa kutuhadaa kuhalalisha wizi wao. Hapo ndipo uwezo wa upotoshaji wa serikali ulipoishia.
Na huu ni ushahidi mwingine kwamba tunaongozwa na watu wenye uwezo mdogo sana au wasio makini kabisa, au wasioitakia mema nchi hii!
Wafanye watakavyo, watutenge katika makundi ya binadamu na wasio binadamu. Rais aendelee kuwa katika kuchukua hatua.
Mwisho wa yote, ajue kwamba tunatambua kuwa anafanya hivyo makusudi, kwa sababu alipuuza ushauri aliopewa. Alionywa mapema, akapuuza. Haya ndiyo matokeo yake.
ansbertn@yahoo.com
+447853850425
www.ngurumo.blogspot.com
Last edited by a moderator: