Marafiki wa mahakama na kesi ya mgombea binafsi

Lawkeys

JF-Expert Member
Nov 16, 2009
1,118
287
MAPROFESA WAJA NA MAONI TOFAUTI KATIKA KESI YA MGOMBEA BINAFSI

Kesi ya mgombea binafsi imeendelea leo, marafiki wa Mahakama Prof. Palamagamba Kabudi na Prof. Juan Mwaikusa watofautiana katika maoni.

Prof. Kabudi alikuwa na hotuba ndefu iliojaa reference mpaka Chief Justice amesema Professor alikua analecture panel. Professor kabudi amesema Mahakama haina uwezo wa kutengua kifungu cha katiba ikiwa kina kinzana na ibara nyingine kwani Katiba ndio sheria mama ambayo ipo juu ya mahakama na mihimili mingine yote ya serikali. Amesema Katiba inawakilisha makubaliano ya wananchi. Amesisitiza kwamba Mahakama inauwezo tu wa kushauri bunge kufanya marekebisho ya katiba na sio vinginevyo kwani Katiba ni tofauti na sheria zingine zote.

Kwa upande mwingine Prof. Mwaikusa amesema kwamba, katiba haitoi haki za binadamu ila tu inaziguarentee, haki za binadamu ni inborn rights mtu anazaliwa nazo. Hivyo mahakama ndio chombo pekee kinachoweza kuhakisha kwamba haki hazivunjwi. Akaendelea kusema kwamba Mahakama kwahiyo inauwezo na inajukumu la kutangaza kifungu chochote cha Katiba ambacho kinaenda kinyume na haki za binadamu.

Prof. Mwaikusa ametoa angalizo kwamba kama mahakama haitakuwa na mamlaka hiyo basi haki za binadamu zitakuwa hatarini kwani sheria yoyote ambayo itatangazwa na Mahakama kwamba inakinzana na Katiba basi serikali itaiweka sheria hiyo kuwa sehemu ya Katiba mahali ambapo Mahakama haitaweza kuifikia kama ilivyo kwa habari ya mgombea binafsi na hivyo kuhatarisha haki za binadamu.

Prof. Mwaikusa kuhusiana na uamuzi uliotolewa na Mahakama kuu, amesema. Mahakama kuu haikukosea kutangaza kifungu cha katiba kinacho hitaji mgombea kuwa mwanachama wa chama fulani iliaweze kumbea kuwa ni kinyume na katiba ila amesema uamuzi huo haukuwa sahihi pale ulipo toa agizo kwa Bunge kutunga sheria itakayowezesha mgombea binafsi.

Mahakama imesema itatoa hukumu on notice yaani baada ya kuwapatia parties taarifa.

"Shoka kali isitumike kukatia mgomba"
 
Na serikali nayo inasemaje juu ya mambo haya na pia kama wamekubali juu ya mgombea binafsi
 
Prof Palamagamba Kabudi ni mwanasiasa na ametumia muda mwingi kutafiti ilimradi hoja ya mwanasheria wa serikali ikaziwe. Asante Mwaikusa walau ameona hatari za kuachia Serikali kutunga sheria na kuipitisha bungeni - kama vile tulivyozoea! Ni mara ngapi tumeona serikali ikijichukulia maamuzi na kuyatungia sheria, bunge likiridhia! Katika hali ya kawaida ni nani atathubutu kusema bunge linatunga sheria zaidi ya kuridhia. Bill zote zinaanzia serikali, mwanasheria mkuu anazitengeneza na kuzipeleka cabinet kabla ya kwenda bungeni, na tena hata bunge likipitisha ni mwenye kaya ndiye mwenye kutoa ridhaa itumike. Na msisahau kabla hajatoa ridhaa hupitia tena kule kwa Mwanasheria wa Serikali na yeye anaweza akashawishika akatupa huko kitu kidogo au akanyofoa(aombe Mungu tu Silaa asigundue!). KWA HIYO BASI BILA MAHAKAMA KUWA NA UWEZO WA KUTENGUA KATIBA YENYE KUNYAKUA HAKI ZA WATU(BILA SHAKA KWA KUFUATIA TARATIBU FULANI FULANI) WATZ TUNAWEZA KUWA MAHALI PABAYA SANA, Palamagamba down with you, hujanifurahisha, hata kama umenukuu vyema, si hata Hitler alikuwa na visheria vyake na vimeandikwa, na vinanukulika!?

 
Huyu "Palamagamba Kabudi," si mnaona hata jina lake halina ushirikiano? Hongera Prof Mwaikusa, haki za Binadamu ni "in born" na kazi ya Katiba ni kuzitambua tu, haiziongezi wala kuzipunguza! Jambo jingine, hilo suala la mgombea binafsi liliingizwa kwa hila na Serikali baada ya Rev Mtikila kushinda katika kesi ya kwanza mwaka 1993, Serikali ilijifanya inakata rufaa katika Mahakama ya Rufani, wakati rufaa iko pending mahakamani, Serikali kwa ujanja ilipeleka Muswada Bungeni wa kupachika suala la mgombea binafsi katika Katiba! Katika kesi ya Attorney General v. Rev. Christopher Mtikila, [1998] TLR 100 katika uk 101 Mahakama ya Rufani ilisema (obiter) hivi: "The Government drew the Judiciary into conflict with Parliament by asking the two organs to deal with the same matter simultaneously, ending into two conflicting results: the court upholding the rights of private candidate and the Parliament barring that right; such a state is regrettable and undesirable, and is incompatible with the smooth adminstration of justice. Once the Government decides to pursue a remedy through the courts of law, it should desist from pursuing another line of remedy in respect of the same matter until the court process comes to an end."
Nafikiri Serikali isiogope kuweka mgombea binafsi, ikubaliane tu na hali halisi!
 
Kinachoendelea hapa ni mchezo ule ule, Kama CCM inaona mgombea binafsi hana maslahi kwa chama hicho basi hatakubaliwa, hawa wote Kina Kabudi na majaji wapo hapo kuangalia unga wao na mtoa unga huo ni serikali ya CCM. Hii kesi hakuna kitu hapo na mahakama ya rufaa itatoa notice ya ku-overturn maamuzi ya mahakama kuu. Maoni tofauti kutolewa na marafiki wa mahakama ni strategy ya kuongeza confusion to the public so that to prepare mahakama ya rufaa kuridhia matakwa ya serikali. Case closed
 
Kinachoendelea hapa ni mchezo ule ule, Kama CCM inaona mgombea binafsi hana maslahi kwa chama hicho basi hatakubaliwa, hawa wote Kina Kabudi na majaji wapo hapo kuangalia unga wao na mtoa unga huo ni serikali ya CCM. Hii kesi hakuna kitu hapo na mahakama ya rufaa itatoa notice ya ku-overturn maamuzi ya mahakama kuu. Maoni tofauti kutolewa na marafiki wa mahakama ni strategy ya kuongeza confusion to the public so that to prepare mahakama ya rufaa kuridhia matakwa ya serikali. Case closed

Well said mkuu,
Mimi binafsi nilikuwa na mashaka sana na huyo prof. Kabudi, pamoja na kubobea kwake katika sheria lakini ni dhahiri kwamba ni mzalendo halisi wa ccm. Mara kadhaa nimekuwa nikimuangalia, kumsikiliza au kumsoma akichangia mijadala mbalimbali mathalani TBC (This week in perspective) nikahisi kwamba atakuwa na kadi mfukoni(sina tatizo na yeye kuwa nayo) lakini katika mtazamo wa kuzingatia maslahi ya taifa, hawezi kutufaa watanzania, hata juzi alipotoa maoni kuhusu Mpendazoe kujiengua CCM maoni yake yalikuwa sawa sawa na ya msekwa!!!
Huyu mkulu anataka waendelee kumkumbuka na pengine wampe ulaji zaidi, subirini tu muda si mrefu kama hii kesi ikiisha na ccm wameshinda, kabudi anaweza kuwa mshauri wa raisi!! Lakini mimi binafsi hadi sasahivi naamini kwamba mahakama ya rufaa haiwezi kuwasaliti watanzania, bado nina imani kubwa na Jaji Ramadhani Augustino.
 
Niliposikia tu Prof.Kabudi ameteuliwa na jaji mkuu kuwa rafiki wa mahakama,nilikuwa na uhakika msimamo wake utaegemea wapi,ningekuwa upande wa utetezi katika kesi hii,ningepinga uwepo wa Prof.Kabudi.

Sababu ya kumpinga ingekuwa kuwa huyu jamaa ni mkereketwa wa chama tawala ambacho ndicho kinachoongoza serikali ambayo inapingana na uwepo wa mgombea binafsi,Kabudi amesikika mara nyingi akikisemea chama tawala,hata juzijuzi tu hapa ametoa kauli ya kumbeza Mpendazoe aliyehamia CCJ.

Hata hivyo ninampongeza sana Pro.Mwaikusa kwa kulijadili hili suala bila kufanya upendeleo.
 
Huyo profesa ni sawa tu na wazee wa sheria mahakamani ambao hutoa tu maoni yao ila hawashiriki katika kutoa hukumu. Hivyo kama ilivyokuwa kesi ya kina Zombe, MAJUDGE watatoa hukumu yao, tuvute tu subira.
 
Huyu mwenye jina la ajabuajabu sijui kalamagamba au palamagamba kahongwa nini? Anyways ni uhuru wa mawazo lakini sijajua kinachoifanya serikali akatae mgombea binafsi. Au CCM wanaogopa kuendelea kugawanyika?
 
KABUDI...NI KADA NAMBA MOJA WA CHAMA CHA MAPINDUZI

kabudi.jpg


NI MTU ANAYEPENDA KUONGEAAAAAAAA.SAAAANA...KWA MUDA MREFU PASSI KUPISHA WENGINE.

HAWEZI KWENDA KINYUME NA CCM BANA KWANI YEYE NDO MIONGONI MWA THINK TANKS WA SERIKALI ILIYOPO MADARAKANI NA NI MTAALAMU MWELEKEZI KWENYE MASUALA MENGI SERIKALINI KUHUSU SHERIA ZA MAZINGIRA, HABARI, MASUALA YA MAJI, MAMBO YA KATIBA NA HAKIMILIKI (INTELLECTUAL PROPERTY RIGHTS - IPR).

MIONGONI MWA KAZI AMBAZO AMEHUSUKA KATIKA SERKALI HII KAMA MTAALAMU MWELEKEZI NI MAPMJA UNADAAJI WA SHERIA ZIFUATAZO AMBAZO UKIZISOMA NI KAMA ZINAFANANA MUUNDO NA MAHUDHUI YAKE KWA MTITIRIRIKO:
  1. Sheria ya Misitu ya Mwaka 2002
  2. Sheria ya Ufugaji wa Nyuki ya Mwaka 2002
  3. Sheria ya Samaki ya Mwaka 2003
  4. Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004
 
KABUDI...NI KADA NAMBA MOJA WA CHAMA CHA MAPINDUZI

kabudi.jpg


NI MTU ANAYEPENDA KUONGEAAAAAAAA.SAAAANA...KWA MUDA MREFU PASSI KUPISHA WENGINE.

HAWEZI KWENDA KINYUME NA CCM BANA KWANI YEYE NDO MIONGONI MWA THINK TANKS WA SERIKALI ILIYOPO MADARAKANI NA NI MTAALAMU MWELEKEZI KWENYE MASUALA MENGI SERIKALINI KUHUSU SHERIA ZA MAZINGIRA, HABARI, MASUALA YA MAJI, MAMBO YA KATIBA NA HAKIMILIKI (INTELLECTUAL PROPERTY RIGHTS - IPR).

MIONGONI MWA KAZI AMBAZO AMEHUSUKA KATIKA SERKALI HII KAMA MTAALAMU MWELEKEZI NI MAPMJA UNADAAJI WA SHERIA ZIFUATAZO AMBAZO UKIZISOMA NI KAMA ZINAFANANA MUUNDO NA MAHUDHUI YAKE KWA MTITIRIRIKO:
  1. Sheria ya Misitu ya Mwaka 2002
  2. Sheria ya Ufugaji wa Nyuki ya Mwaka 2002
  3. Sheria ya Samaki ya Mwaka 2003
  4. Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004

Nilikuwa na imani na huyu Profesa, sasa hivi nimeanza kupoteza imani naye!
 
The government which squanders all its resources, including intellectual resources -like Prof. Kabudi-, in oder to deny its own people their basic rights, just for the sake of remaining in power, is misarable, irrelevant and doomed to fail. It won't take much longer time before CCM becomes useless in the hearts of the Tanzanians. Let them know that they are still squandering Nyerere's political capital, soon it will be over!CCM's clandestine alias NEC has no right to gamble our future like they did for all those years since independence; leaving us in abject poverty. Let them know that the threshold is about to be reached... We want change and we won't rest until change comes.
 
Prof. Kabudi is a Professor of law at the Faculty of Law of the University of Dar es Salaam. He is one of the founder members of the Tanzania Legal Education Trust (TANLET) which founded the LHRC. Prof. Kabudi joined the LHRC's Board of Director's in 1998 when he returned from his doctoral studies. He is known for being a human rights advocate. He was elected Vice Chairperson in 2007. Prof. Kabudi is a member of the LHRC.

He is a Member of the Board and a Senior Lecturer at the University of Dar-es-Salaam, United Republic of Tanzania. He is also advisor to the Office of the Vice President on the environment in the United Republic of Tanzania. Prof. Kabudi is a member of the Board of the Lawyers' Environment Action Team (LEAT) and the Human Rights and Legal Resource Centre- two leading partner NGOs in Tanzania. He therefore brings with him immense experience in NGO management.

Jamaa kama kweli yuko Human Right, basi nikipata matatizo, Mgogo huyu ntamkimbia kama ukoma. Kabudi, umetoka familia iliyo karibu na dini ya Anglikan huko Mvumi Mision. Kama ulikuwa kwenye human right basi ulikuwa nyumbani na sasa unachokifanya kwa kweli ni kinyume kabisa. Siamini kama kweli umeamua kutetea wezi na vibaka. Naogopa kuwa "umeshikwa pabaya" na sasa wanakutumia wanavyotaka. Pole sana.

Hivi hawa Waalimu wa sherria wa UDSM ni vipi? Juzi hapa tumesoma mwingine Mlimuka akipinga wafanyakazi kugoma. Tunashukuru kuwa wapo wengine bado HAWAJANUNULIKA na wanaridhika na wanachokipata.
 
Huyu "Palamagamba Kabudi," si mnaona hata jina lake halina ushirikiano? Hongera Prof Mwaikusa, haki za Binadamu ni "in born" na kazi ya Katiba ni kuzitambua tu, haiziongezi wala kuzipunguza! Jambo jingine, hilo suala la mgombea binafsi liliingizwa kwa hila na Serikali baada ya Rev Mtikila kushinda katika kesi ya kwanza mwaka 1993, Serikali ilijifanya inakata rufaa katika Mahakama ya Rufani, wakati rufaa iko pending mahakamani, Serikali kwa ujanja ilipeleka Muswada Bungeni wa kupachika suala la mgombea binafsi katika Katiba! Katika kesi ya Attorney General v. Rev. Christopher Mtikila, [1998] TLR 100 katika uk 101 Mahakama ya Rufani ilisema (obiter) hivi: "The Government drew the Judiciary into conflict with Parliament by asking the two organs to deal with the same matter simultaneously, ending into two conflicting results: the court upholding the rights of private candidate and the Parliament barring that right; such a state is regrettable and undesirable, and is incompatible with the smooth adminstration of justice. Once the Government decides to pursue a remedy through the courts of law, it should desist from pursuing another line of remedy in respect of the same matter until the court process comes to an end."
Nafikiri Serikali isiogope kuweka mgombea binafsi, ikubaliane tu na hali halisi!
.

Asante Buchnan, Huyu Prof. Kabudi, binafsi namfahamu sana sana sana, tangu akiwa mwandishi wa habari magazeti ya Uhuru na Mzalendo, yeye na mwenzake Mwakiyembe na Mvungi, ndipo wakaipa kisogo habari na kujiunga na sheria ambako wote sasa wamebobea.

Kabudi alikuwa mwalimu wangu wa sheria pale UD na ndiye supervisor wangu wa LL.B Desertation, ni msomi aliyebobea, very genuine, na very fair, ila kwa maoni yake leo, japo nayaheshimu maoni yake hata kama sikubaliani nae, leo teacher amechemka big time!, na ataaibika milele, kwa sababu mahakama itaamua ku uphold hukumu ya mahakama kuu, na yeye kama dean wa faculty, atatafuta pa kuiweka sura yake, na ataonekana kituko kwenye tasnia ya sheria, na atakuwa subject to ridicule for a long time to come kisa kujikomba kwa CCM!.

Nimefurahishwa sana na msimamo wa Jwan Mwaikusa, pale alikuwa aitwe mtu kama Prof. Issa Gulamhussein Shivji na Prof. Gamaliel Mgongo Fimbo, au Prof. Chris Peter Maina, serikali ingeogelea kwenye tope la aibu. Nadhani jama wa TISS walipenyeza majina ya nani aitwe, wakawachukua wale modarate, Kabudi alitakiwa kama msomi kwanza aichambue hii constutional yetu iliyotungwa bila kuwa na constitutionalism, leo ndio yeye anasimama na miguu yake miwili kuitetea unconsitutionalism ya katiba yetu utumbo aliomwaga!.

All and all, baada ya mahakama kufanywa dekio au tambara la deki kwa muda mrefu kuusafisha uchafu wa serikali, sasa itasimama na kujipambanua kuwa ndio mhimili wa haki. Jaji Ramadhani with nothing to loose, atasimama na kuhesabiwa akileave behind a legacy of force to recon with.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Watanzania, tuacheni huu ulimbukeni wa kumchambua mtu binafsi kwa sababu tumetofautiana kwa maoni. Prof Kabudi yupo kazini, ameitwa na mahakama kutoa maoni yake...key word "maoni yake" sasa hizi personal attacks ni za nini?

Kama hatuwezi kujadili hoja alizozitoa kuwa upande wa Serikali basi ni vizuri sasa tuwaachie majaji kazi yao kutoa uamuzi.
 
mwanasiasa, sheria yetu ni ya ajabu.. hata kama mahakama inasema sheria fulani ni kinyume na katiba, sheria hiyo haikomi kuwa na nguvu hadi Bunge liibadilishe sheria hiyo au kipengele husika. Hivyo basi, kama ukitokea uchaguzi kesho, hakuna mgombewa huru atakayeruhusiwa!!!! hilo ndilo lililokuwa tatizo la hukumu ya awali 1994.

Hata hivyo jopo la majaji wa sasa wameamua kuiweka serikali kwenye kona. Ukitokea uchaguzi kesho, na serikali haijaweka utaratibu wa kuruhusu wagombea binafsi basi Mtikila anaweza kwenda mahakamani na kusimamisha uchaguzi huo!! So unless, serikali ikate rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa na hukumu ibadilishwe, basi wagomba huru watakuwepo... kwani bila ya kufanya hivyo hakuna uchaguzi utakaoweza kufanyika!!!


Kwa hali ilivyo, inaonyesha huu utabiri wa Mwanakijiji huenda ukatimia. Maamuzi ya hii Rufaa ya Serikali yana implications kubwa sana kwenye nchi yetu. I can't wait kujua majaji wanatoa uamuzi gani.
 
Ninavyoona tunakoelekea kuna baadhi ya wasomi kuumbuka, Kabudi anaposema mahakama haikuwa na uwezo wa kutengua kifungu cha katiba hata kama kikiwa kibovu kwa maana hiyo anatuambia anajua kabisa kuna vifungu kwenye katiba vinakinzana lakini kwa kutumia katiba hiyo hiyo anazidi kuvitetea, naanza kukubaliana na watu wanaosema kadri mtu unavyosoma zaidi unajikuta unasahau hata msingi wa kile unachokisomea.
 
Nilikuwa na imani na huyu Profesa, sasa hivi nimeanza kupoteza imani naye!


Na huu ndo utatu wa Prof. Kabudi mbele ya jamii ya mataifa, na hapa ndo unaona anavyojaribu kujikanganya na kuonekana kama mnafiki, huku anazungumzia msimamo huu na kule huu!!.

Workshop A: COALITION GOVERNMENTS PARLIAMENTARY DEMOCRACY IN DILLEMMA?



Prof.Parramagamba Kabudi; Lecturer, University of Dar es Salaam. In his presentations he mentions four types of governments;
  • A government formed by a majority political party i.e fast- past- the post
  • Coalition governments, he said this is a situation where there is no single winner but small parties come together to form a government. These he said may sometime come out of necessity while they can also emerge as a result at a negotiated settlement.
  • National Unity governments; he said these are deliberately formed such as in a post-apartheid South Africa and Ruanda. They are formed as part of National healing.
  • The Mischief or National Rescue/Survival, he said if the National Rescue Governments. Under this ideology people learn to leave together
He said it is time to move away from political competition to complementary politics which is an all inclusive ideology. This includes everybody in governance where the leaders are servants of the people and not masters of the people. He said most of the constitutional arrangements in our countries today are unconstitutional in order to protect those who want to cling to power by all means, and thus we shall continue to have National Rescue governments. He said the solutions were on the hands of the politicians and urged them to behave as citizens also. He argued third generation coalitions to learn from the experiences of India.


http://webcache.googleusercontent.c....doc+Prof+Kabudi+CV&cd=13&hl=en&ct=clnk&gl=uk

 
Back
Top Bottom