mgen
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 22,629
- 8,416
Sintasahau siku yangu ya kwanza kumfahamu Mtikila!Ilikuwa hivi;Nilipanda basi kutokea G/mboto kueleke posta, kufika tazara trafic police akatusimamisha kwa madai kwamba gari ni mbovu iende kituoni hivyo abiria wote shukeni! Wakati tunajiandaa kushuka akajitokeza mtu mmoja mfupi huku amekasirika na kumwambia yule police hapa hashuki mtu! Unaiona hii ticket? Huu ni mkataba kati yangu na mwenye basi kunipeleka posta. Na wewe kama police kazi yako ni kulinda huu mkataba, kwa nini unataka kuvunja mkataba? Yule police alipofahamu kwamba anaongea na Mtikila akamgeukia dereva na kumwambia wapeleke posta kisha ulete gari kituoni ikaguliwe! Ndipo alipo muongeza hasira Mtikila na kumwambia yule police! We we si ulisema gari mbovu? Hujui kwamba lazima hii gari ifanye kazi ili alipe kodi.Ili na wewe upate mshahara?Wakati police anabung'aa bung'aa akamtupia donge jingine kuwa nyie police badala ya kujifunza sheria mnajifunza kulinda mafisadi na kupiga virungu walalahoi, huku akimuamuru dereva endesha gari na kumuacha yule police pale haamini!My take; raia tunapoelewa haki zetu lazima police watuheshimu!