Mapovu toka CCM; waandishi wamenangwa na Tundu, tusubiri tamko

Mtoa mada hajui anachokiongea. Ameweka hii hoja ili awayumbishe watu wasio makini. Hana tofauti na yule mpuuzi aliyesema huenda Mwangoka alitaka kujilipua.
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli,waandishi wa habari tz hamna kitu,mfano mzuri ww mwenyewe unaandika bila kufanya hata editing,mfano mzuri ni pale mliposhindwa kumpiga picha mmiliki wa dowans baada ya kununuliwa juice Kempisky,ww kama mwandishi mbona unaandika kwa kuwalamba viongozi miguu?mkiambiwa ukweli mnaona mnatukunwa,sasa kama hujui usiambiwe?
 
Mimi mpaka sasa sijaelewa kitu kimoja, kwanini ni CDM ndio wameshupalia hiyo tume na sio familia ya mfiwa. Afadhali hata waandishi wa habari wangeshupalia tungeelewa.

Inawezekana wanafamilia bado hawajazinduka kwenye majonzi kutokana na msiba huu mkubwa mno.
 
Kiganyi wewe ni msanii mzuri sana kusanii kwenye jamii ya wasiowachambuzi wa mambo. Yawezekana kweli umeumizwa na matamshi ya Lisu lkn mimi sidhani kuwa ndiyo hivyo na kwa kiasi hicho.

Naijua mipango ya kisiasa ya chama chako ktk kutafuta na kufanya kila litakalowezekana ili kupata fursa ya kurejesha heshima ya chama chenu ktk jamii.

Hapa unachokitafuta ni siasa ya majitaka ya kutaka kumchonganisha huyu dogo lisu na waandishi wa habari. Mbinu unayotaka kuitumia iko very weak kaka.

Mkuu huwa unakosea sana kuni label hivo lakini sikulaumu!

Mimi nimeshangaa mwandishi ambaye haelewi Lissu alikuwa anasimamia Sheria ya kuunda tume na he just came out loud kwamba jamaa kawadhalilisha wanahabari!

Nadhani nakusaidia kuwatambua waandishi wanaopaswa kupuuzwa lakini kumbe inakukera! Na ndio maana nimeonesha kuwa hiyo habari nimeichagua toka wapi!

N vizuri kuelewa na kuziona pumba na Mchele wakati huu kuliko kungoja hadi pale watu watapoanza kupotoshwa moja kwa moja!

Sorry Mkuu! Ila mimi ni Mwanachadema na najivunia katika hilo!
 
Siku wanahabari watakapokuwa na taaluma nyingine zaidi ya uandishi vile kama sheria, uchumi, kilimo, afya, elimu, uhandisi, nk. weledi wao utakuwa juu kuliko ilivyo sasa. Uandishi ni kama chombo cha kufikisha ujumbe kwa umma. Mwandishi akiwa na taaluma nyingine uwezo wa kutetea kundi fulani analolielewa habari itakamilka vizuri. Waandishi wajitahidi kuchukua masomo ya ziada ya taaluma nyingine ili wasiendelee kunangwa ila waheshimike.
 
Huyu Makunga si ana kesi ya uhaini? bado serikali inamuamini kufanyiwa kazi na yeye? je atafanya kazi kwa uhuru huku akijua nae ana kimeo chake? bora hata kibanda alijitoa kwenye vazi la taifa ambalo mpaka leo hatujatangaziwa kaka limepatikana. Makunga kama ana akili atajitoa naye...
 
Alisema tume inaundwa na rais!.. Nami nasema...Hakuna haki wala haki haitatendeka iwapo wafuatao hawatajiuzulu au kuchomolewa na Kikwete kupisha uchunguzi:1. Waziri Nchimbi;2. Mkuu wa mkoa wa IRINGA; 3. RPC;4. Mkuu wa wilaya;5. OCD; na 6. mkuu wa upelezi mkoa (RCO), 7. Chagonja.
 
Mkuu Kiganyi! Kwanza napingana na hoja ya kuwa Mh Lissu amedharau taaluma ya Uandishi. Mh Lissu ameanza na mfumo wa tume, then akamchambua mwenyekiti wa tume na wajumbe. Alichosema ni kwamba hawa wajumbe wamekosa nguvu za kisheria kimwita na kuwahoji viongozi kama Dr.Nchimbi, IGP Mwema ambao ni watuhumiwa wa kifo hiki? akapendekeza kama tume itakayoundwa na Rais iwe na Majaji wa mahakama kuu au ya Rufaa ambao watakuwa na mamlaka na nguvu za kisheria kuhoji kila mtu but Rais.
Mkuu kama CCM na serikali yake unajari na kuthamini taaluma ya uandishi wa habari
1) Mbona mpaka leo Mwenyekiti wa CCM Taifa hajatoa salamu za Rambirambi kwa Waziri wa Habari juu ya kifo hiki
2) Kama serikali ya CCM inathamini Taaluma ya Uandishi wa Habari, kwanini limetumia sheria kandamizi kufungia MwanaHalisi?
3) Kama Serikali ya CCM inathamini vyombo vya habari, Mbona TBC, Uhuru na Mzalendo ni vyombo vya umma, lakini vinafanya kazi za CCM?
 
Mwandishi alie andika hii makala lazima atakuwa ametumwa na ccm ili kuchonganisha CDM na waandishi. Lakini wajanja tumesha gundua, kwa nini waziri aunde kamati kuchunguza wakati yeye mwenyewe ni mtuhumiwa ,waziri amekurupuka au anataka kuficha jambo.
 
Mimi mpaka sasa sijaelewa kitu kimoja, kwanini ni CDM ndio wameshupalia hiyo tume na sio familia ya mfiwa. Afadhali hata waandishi wa habari wangeshupalia tungeelewa.

Kwa sababu wahahusika na mauaji wanataka kupoteza ushahidi.
 
Mtoa hoja hajui alichokiandika...shame eti tume ya MV Bukoba ilienda vizuri kwa sababu ilikuwa na mwandishi wa habari aliebobea? Sijui anamaanisha nini kusema ilienda vizuri? Eti TL anatakuaamisha umma kuwa tume (tume au kamati?) haina uwezo! Kwanza siku hizi watanzania awaaminishwi na mtu wana weledi wa kutosha kuelewa mambo mengi.

Narudia mtoa hoja hajua alichokiandika imagine eti mtu ukiwa mwanahabari wa siku nyingi au umebobea katika fani fulani basi unaweza kuchunguza mauaji/kifo...this is ignorance.
 
Culled from Daily Nkoromo Blog

TAALUMA ya uandishi wa habari nchini kila kukicha imeendelea kudharauliwa na wanasiasa na baadhi ya viongozi ambao wanajiona taaluma zao ndio bora na zenye uwezo wa kuhoji na kuakisi mambo.

Mfumo huo umeendelea kuota mizizi huku hata zile klabu, majukwaa na mabaraza ya uandishi wa habari yakiwa kimya na badala yake kuzungumzia mambo mengine ambayo hayana faida kwa mwandishi wa habari.

Uandishi wa habari Tanzania unakumbukana na changamoto lukuki ambazo zilipaswa kuwa sehemu ya mjadala kwa vyama vilivyopewa dhamana ya kuwaongoza waandishi wa habari ambao maisha na mfumo wa kazi zao umekuwa kama mchezo wa bahati nasibu.

Kitendo ambacho kinafanya thamani na hadhi ya mwandishi kila kukicha kupotea huku majina ya dharau nayo yakizidi mara 'watu wamshiko', 'makanjanja' au 'vihiyo'. Yote haya yanasababishwa na ubinafsi na ukasuku wa kukariri matamko.

Kauli ya kashfa na Mbunge Tundu Lissu (Singida Mashariki - CHADEMA) kuhusiana na wajumbe wa tume walioteuliwa na serikali kuhusiana na kifo cha Mwandishi wa habari Daud Mwangosi kuwa baadhi yao hawana uwezo ni fedheha kubwa kwa wajumbe hao na tasnia nzima.

Mbunge huyo aliitisha mkutano na waandishi wa habari kuelezea msimamo wa chama chake kutokuwa na imani na tume hiyo hasa kutokana na kuwa na wajumbe baadhi aliodai wasiokuwa na ueledi wa mambo wanaochunguza.

Katika mkutano huo, Lissu alizungumza mambo mengi juu ya tume hiyo, lengo likiwa kuaminisha umma kuwa tume hiyo haifai na ndiyo maana chama chao wanaikataa huku akitaja majina ya wajumbe wa tume hiyo ambayo kimtazamo wake yeye anasema hawana uwezo.

Hata hivyo, muktadha wa hoja hii hautakuwa kuzungumzia uwezo wa kila mjumbe ndani ya tume hiyo, bali ni udhaifu wa vyama vyetu ambavyo navyo vinapotezwa katika mlengo wa kusimamia maslahi ya waandishi na kuanza kuwa watoa sauti ya wanasiasa kushindana kuikataa tume.

Kuchaguliwa kwa Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Stephen Ihema na wajumbe wengine wakiwemo mahiri katika tasnia ya habari kama Theopil Makunga (Jukwaa la Wahariri) na Pili Mtambalike (Baraza la Habari Tanzania) ilikuwa ni sehemu ya waandishi na klabu za habari kufurahia na kuipongeza serikali.

Kufurahia huko kunatokana na kifo cha Mwangosi ambaye ni mwenzetu kuwa kinachunguzwa na waandishi wenyewe, hivyo kutolewa kwa kauli za dharau kuwa waandishi wa habari hawawezi kuchunguza kifo ni tusi kubwa ambalo lilipaswa kukemewa na si kuachwa kama inavyotaka kufanywa.

Nakumbuka katika jali ya MV Bukoba, mmoja wa wana habari mahiri nchini Jenerali Ulimwengu alikuwa mjumbe wa tume iliyochunguza chanzo cha ajali hiyo. Mbona mambo yalikwenda sawa au kwa kuwa Lissu alikuwa hajapata umaarufu?

Japokuwa katika suala zima kuhusiana na tukio hilo waandishi walitofautiana kimtazamo na kifikra, lakini linapokuja suala la kudharauliwa, tunapaswa kuwa pamoja na kukemea. Kinyume chake baada ya kunang'wa na Lissu tunatakuja kupewa tusi kubwa zaidi.

Mwenye uwezo na ueledi wa kuchunguza kifo si mwanasheria pekee? Lisu anapaswa kutambua hilo na kuachana na mawazo ya Mfalme Jua, juu ya kile anachokiamini kuwa ni sahihi na hapaswi kupingwa au kukatazwa na mtu.

Jamii inaelimishwa na kufundishwa kupitia mifumo tofauti ya maisha na ndiyo maana wanasaikolojia wanaamini tabia ya mtu ni rahisi kuifahamu kupitia matamshi na matendo yake kuwa ni makuzi gani aliyapata utotoni.

Sitaki niamini kuwa klabu, jukwaa na hata baraza lenyewe halijasikia maneno ya kejeli ya Lissu, bali naamini yapo makundi ndani ya waandishi wa habari likiwemo la wale walio tayari kwa lolote ili mradi wawanufaishe wengine na hasa wanasiasa au watwana wao.

Hilo litapongezwa kwa matamko au hata kwa kujitokeza na kusukuma magari yao kuwa hawa kwa mtazamo wao kuwa hao ni mashujaa na wazalendo wa nchi hii .

Hivyo, ningetamani nguvu iliyotumika kutoa tamko la kuwataka polisi wakae meza moja na CHADEMA kumaliza tatizo, ingetumika kutoa tamko juu ya dharau ya Lissu na chama chake kwa waandishi wa habari nchini.

Ur very clear wewe ni ant lissu jinsi ulivyoweka andiko lako unaonyesha uwezo wako katika kuripoti habari.Kwanza kabisa hakuna tume iliyoteuliwa bali ni kamati.kwajinsi nilivyomsikia lissu alichokuwa analalamikia ni uwezo wa waziri kuunda tume wakati ana mamlaka hayo kikatiba,hilo la uwezo wa wajumbe alizungumza kwa ujumla kuzingatia uwezo na mazingira ya tukio lenyewe.Lengo lako ni kutaka kuuaminisha umma wa watanzani na waandishi wa habari kuwa lissu amewananga.kama huu ndiyo aina ya uhandishi basi twafa
 
Mimi mpaka sasa sijaelewa kitu kimoja, kwanini ni CDM ndio wameshupalia hiyo tume na sio familia ya mfiwa. Afadhali hata waandishi wa habari wangeshupalia tungeelewa.
mkuu lazma maana wao wanatuhumiwa kwa kuua katika mikutano yao, ndo mana jana lisu aliwaambia iundwe tume na raisi ya kuchunguza vifo vyote vinavyotokea kwenye mikutano ya cdm ili ukweli ujulikane nini hasa kiini cha mauaji hayo
 
Mimi mpaka sasa sijaelewa kitu kimoja, kwanini ni CDM ndio wameshupalia hiyo tume na sio familia ya mfiwa. Afadhali hata waandishi wa habari wangeshupalia tungeelewa.

ni rahisi mwandishi wa habari kununuliwa kuliko chadema, na chadema wana haki kushupalia kwa sababu CCM imefanya wimbo wa chadema ndio chanzo na wanasahau kuwa polisi ndio chanzo, inaonekqna unatumia . . . . . kufikiria
 
Mtoa mada hajui anachokiongea. Ameweka hii hoja ili awayumbishe watu wasio makini. Hana tofauti na yule mpuuzi aliyesema huenda Mwangoka alitaka kujilipua.

Naungana na wewe, maana waandishi waliyoteuliwa kwenye hiyo kamati hawana uzoefu na habari za uchunguzi.
 
Alafu nakumbushia kuwa aandishi wengi wanaandika na kuripoti habari kwa mazoea, mwandishi anatakiwa awe na taaluma ya habari anazo ziandika {habari za afya, habari za uchumi, habari za kiuchunguzi n.k} sasa leo mwandishi kila habari yeye anaandika tu bila kuwa amebobea upande huo na ndio maana kuna kipindi wanakosea bila wao kujua kama amekosea hiyo habari, maana ni kitu ambacho hakijui.
 
Lisu alipinga uhalali wa hiyo iliyotangazwa kuwa ni tume,pia akaanza kuchambua sifa za waundaji wa tume yenyewe ambapo ilikuwa kama mchezo wa kesi ya nyani kupelekwa kwa ngedere,nin kitaendele hapa? Waandishi wengi ni makasuku wenye ushupaliaji wa mambo badala ya uchanganuzi yakinifu na hii inatokana na fani husika kuvamiwa na wale wasio na taaluma na maadili baada ya kutolewa kwa vyeti kila kona kama njugu na kuwa kimbilio la wengi waloshindwa kujiendeleza,hapa anajaribu kuchochea chuki kati ya waandishi na chadema kiujumla lakini ukweli ukijulikana ni upi 'read between the lines'
 
Back
Top Bottom