Mapishi ya pilipili mboga na ngisi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040
Mapishi ya pilipili mboga na ngisi




Mahitaji
23-1-54-816.jpg

Pilipili mboga gramu 250, ngisi gramu 250, chumvi kijiko kimoja, mvinyo wa kupikia vijiko viwili, maji ya wanga vijiko vitatu, chembechembe za kukoleza ladha kijiko kimoja, kiasi kidogo cha vitunguu maji na tangawizi
Njia
1. kata pilipili mboga ziwe vipande, kata ngisi awe vipande.
2. chemsha maji, halafu tia slesi ya pilipili mboga kwenye maji, korogakoroga, ipakue. Na tia vipande vya ngisi kwenye maji korogakoroga, ipakue.
3. washa moto, tia mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya vitunguu maji na tangawizi korogakoroga, tia vipande vya pilipili mboga na ngisi, korogakoroga, halafu tia chumvi, chembechembe za kukoleza ladha, mvinyo wa kupikia, maji ya wanga, korogakoroga, halafu mimina mafuta ya ufuta, korogakoroga, ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.


Mapishi ya kuku na limao




Mahitaji:
200771991740806.jpg

Nyama ya kuku gramu 300, wanga gramu 100, maji juisi ya limao gramu 250, sukari gramu 30, nyanya gramu 100, chumvi gramu 3, mvinyo wa kupikia gramu 5, vitunguu maji gramu 3, tangawizi gramu 3.
Njia:
1? Osha nyama ya kuku halafu uikate iwe vipande, koroga pamoja na chumvi, mvinyo wa kupikia, pilipili manga, tangawizi na vitunguu maji. Koroga maji juisi ya limao pamoja na unga, chumvi, pilipili manga, yai na mafuta.
2? Washa moto, mimina mafuta kwenye sufuria, weka vipande vya nyama ya kuku kwenye unga uliokorogwa, halafu weka ndani ya sufuria vikaange, halafu vipakue.
3? Washa moto tena, mimina maji kwenye sufuria, halafu tia chumvi, sukari, maji juisi ya limao, korogakoroga halafu mimina maji ya wanga, korogakoroga, tia vipande vya nyama ya kuku korogakoroga vipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Mapishi ya slesi ya ngisi




Mahitaji:
041007-0849-1.jpg

Ngisi gramu 250, nyama ya nguruwe gramu 100, machipukizi ya mianzi gramu 80, chumvi gramu 5, mchuzi wa sosi gramu 2, mvinyo wa kupikia gramu 6, chembechembe za kukoleza ladha gramu 2, mafuta ya ufuta gramu 2.
Njia:
1. mkate ngisi awe slesi, halafu washa kwa maji na uikaushe.
2. kata nyama ya nguruwe na mianzi ya vichipukizi iwe vipande vipande, halafu chemsha maji, tia vipande vya machipukizi ya mianzi kwenye maji, korogakoroga vipakue.
3. washa moto, tia mafuta kwenye sufuria, halafu tia slesi ya ngisi, korogakoroga, mimina mvinyo wa kupikia korogakoroga, tia vipande vya nyama ya nguruwe na machipukizi ya mianzi korogakoroga, tia chumvi, mchuzi wa sosi, korogakoroga, tia chembechembe za kukoleza ladha, mimina mafuta ya ufuta korogakoroga. Ipakue mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.




Mapishi ya maharagwe na pilipili manga




Mahitaji
234204770.jpg

Maharagwe gramu 250, karanga gramu 100, karoti moja, koliflawa gramu 200, pilipili manga gramu 50,mchuzi wa sosi kijiko kimoja, siki vijiko viwili, sukari vijiko viwili, chumvi kijiko kimoja
Njia
1. kata maharagwe yawe vipande, kata karoti iwe vipande vipande, na kata koliflawa iwe vipande. Kila weka kwenye maji joto, halafu vipakue. Weka karanga kwenye maji moto ichemsha kwa dakika 15, ipakue. Weka vipande vya maharagwe, karanga, koliflawa na karoti kwenye bakuli moja.
2. tia mafuta kwenye sufuria, tia pilipili manga, halafu tia mchuzi wa sosi, siki, sukari na chumvi korogakoroga, ondoa pilipili manga, mimina mafuta hayo kwenye bakuli, korogakoroga. Mpaka hapo kitoweo ni tayari kuliwa.





Mapishi ya kamba-mwakaje na uyoga



Mahitaji
caoguxiaoren.jpg

Kamba-mwakaje gramu 400, mafuta gramu 30, uyoga gramu 70, mafuta ya ufuta kijiko kimoja, ute wa yai, mvinyo wa kupikia vijiko viwili, chumvi kijiko kimoja, sukari kijiko kimoja, pilipili hoho moja, wanga vijiko viwili, chembachembe za kukoleza ladha nusu ya kijiko.
Njia
1. osha kamba-mwakaje, koroga pamoja na ute wa yai, mvinyo wa kupikia, chumvi na wanga. Kata pilipili hoho iwe vipande. Kata uyoga uwe vipande.
2. washa moto, tia mafuta kwenye sufuria, tia kamba-mwakaje kwenye sufuria korogakoroga, tia vipande vya uyoga, pilipili hoho, halafu tia chumvi, sukari, chembechembe za kukoleza ladha, korogakoroga, mimina maji ya wanga, korogakoroga, ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.


print.gif
tj.gif
mail.gif

Mapishi ya nyama ya kuku na pilipili manga


20070814_0fdec5a1c109ed880ef8kVbsfOj2cWd6.jpg
Mahitaji

Nyama ya kuku gramu 200, pilipili hoho gramu 50, pilipili manga gramu 20, pilipili mboga gramu 20, kiasi kidogo cha vipande vya vitunguu maji, vitunguu saumu na tangawizi, sukari kijiko kimoja, chumvi kijiko kimoja, na mchuzi wa sosi vijiko viwili.
Njia
1. kata nyama ya kuku iwe vipandevipande. Kata pilipili mboga iwe vipande.
2. washa moto , tia mafuta kwenye sufuria punguza moto kidogo, tia pilipili hoho na pilipili manga kwenye sufuria, korogakoroga. Tia vipande vya vitunguu maji, vitunguu saumu na tangawizi, korogakoroga, tia vipande vya nyama ya kuku korogakoroga, mimina mchuzi wa sosi, korogakoroga, tia vipande vya pilipili mboga, sukari na chumvi, korogakoroga, ipakue. Mpaka hapo kitoweo kiko tayari kuliwa.



Mapishi ya kuchemsha doufu kwa mvuke ndani ya majani ya yungiyungi



Mahitaji:
0808.jpg

Doufu gramu 300, nyama ya kuku gramu 30, uyoga gramu 10, uyoga mweusi gramu 10, yai moja, vipande vya paja la ash la nguruwe gramu 10, majani ya yungiyungi, chumvi kijiko kimoja, sukari kijiko kimoja, vipande vya vitunguu maji na tangawizi kila kimoja gramu 5, mafuta ya ufuta kijiko kimoja, wanga wa pilipili manga kijiko kimojra, siki kijiko kimoja, mchuzi wa sosi vijiko viwili, mharadali kijiko kimoja
Njia:
1. kata kata doufu iwe kama iliyosagwa, saga nyama ya kuku. Kata uyoga na uyoga mweusi viwe vipande vipande. Koraga yai halafu washa moto mimina mafuta kwenye sufuria, mimina yai lililokorogwa kwenye sufuria likaange. Halafu lipakue na vikata liwe vipande vipande.
2. koroga doufu, nyama ya kuku, vipande vya paja la ash la nguruwe, uyoga, chumvi, sukari, vipande vya vitunguu maji na tangawizi, mafuta ya ufuta, wanga wa pilipili manga, siki, mchuzi wa sosi na mharadal, halafu weka kwenye majani ya yungiyungi, weka vipande vya yai na uyoga mweusi. Washa moto tena mimina maji kwenye sufuria weka majani ya yungiyungi kwenye sufuria chemsha kwa mvuke kwa dakika 10, ipakua. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom