Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga

Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga:
Mahitaji:
1. bamia gram 250
2. Majani ya maboga 200
3. Nyanya chungu (kama utapenda) gram 100
4. Magadi 1/4 kijiko cha chai
5. chumvi - to taste
6. nyanya ndogo 1
7. Karanga zilizosagwa gram 100
8. maji - kikombe 1

Matayarisho:
1. Osha na kata bamia na nyanya chungu vipande vidogovidogo
2. Osha na kata majani ya maboga ndogondogo

Jinsi ya kupika
1. Bandika maji mpaka yachemke
2. weka chumvi na magadi
3. Weka majani ya maboga, bamia, na nyanya chungu
4. vikishachemka kwa kama dakika 5, weka nyanya, acha ichemke kidogo.
5. weka unga wa karanga na acha uchemke kwa kama dakika 5 - 7.
Tayari kwa kuliwa.
Mboga hii inapendeza kuliwa na ugali

Umenikumbusha kwetu sikonge sana..
 
Ngoni...apa job kwangu kuna wangoni wawili...
Mmoja ver shy akiwa na watu asiowajua ila muongeaji akiwa na kampani aliyoizoea. Ni mzushi mno na promiseless balaa. Never likes to hang out...baba na mama wote ni wangoni.

Huyu wa pili ndo kama nyie...she loves cooking. Yupo friendly tu kwa wote. Alikuja kwangu cku moja akatupikia ugali ila aling'ang'ania ninunue kuku...now i know y. Heheheheh
 
Ngoni...apa job kwangu kuna wangoni wawili...
Mmoja ver shy akiwa na watu asiowajua ila muongeaji akiwa na kampani aliyoizoea. Ni mzushi mno na promiseless balaa. Never likes to hang out...baba na mama wote ni wangoni.

Huyu wa pili ndo kama nyie...she loves cooking. Yupo friendly tu kwa wote. Alikuja kwangu cku moja akatupikia ugali ila aling'ang'ania ninunue kuku...now i know y. Heheheheh
lazima aling'ang'ania kuku wa kienyeji, ha haaaaaaaaaaaaaaaa (utakoma kama huko uliko hakuna kuku wa kienyeji). mimi pia muoga kuanzisha mazungumzo na watu ambao sijawazoea, hata wadada, ila nikishawazoea sina shida tena
 
lazima aling'ang'ania kuku wa kienyeji, ha haaaaaaaaaaaaaaaa (utakoma kama huko uliko hakuna kuku wa kienyeji). mimi pia muoga kuanzisha mazungumzo na watu ambao sijawazoea, hata wadada, ila nikishawazoea sina shida tena

oook...now i get it! nimeonana naye tena leo asubuhi..ana aibu! ananikumbusha wadada wa miaka ya 80 na early 90s...

Hahaha..kuku wa kienyeji hakupatikana ila nitamuuliza kama anajua hivo vikitu mlivotaja hapo juu!!!
 
oook...now i get it! nimeonana naye tena leo asubuhi..ana aibu! ananikumbusha wadada wa miaka ya 80 na early 90s...

Hahaha..kuku wa kienyeji hakupatikana ila nitamuuliza kama anajua hivo vikitu mlivotaja hapo juu!!!
akikupikia uje utoe taarifa ilikuwaje. kwa huku uliko kama hakuna karanga unaweza hata kutumia peanut butter
 
mh..kumbe pitiku ni majani ya maboga..mlivotaja nkadhani bonge la meeenu...yaani nyie!
wai..heri aje tupike chapati ndo somo langu la wikiendi...
ha haaaaaaaaaaa, yaani Mentor mpaka umeenda kutafuta desa la pitiku? ulidhani boooonge la menu.......... ngoja snowhite aje kutuwekea recipe ya hiyo kitu
 
Niko jikoni nikitengenez mlenda na ugali wa matoke
Kalibuni lunch saa saba
 
ha haaaaaaaaaaa, yaani Mentor mpaka umeenda kutafuta desa la pitiku? ulidhani boooonge la menu.......... ngoja snowhite aje kutuwekea recipe ya hiyo kitu

ahahahhahah sijui ilinipitaje hiii!
pitiku bana haina makuu!
ni majani ya maboga
chumvi
maji
na kapilipili
unakata majani ya maboga vidogo dogo,unaweka maji,na pilipili unabadnika jikoni!
maji yakichemka unaweka mboga
inaiva kama dk 8-10 hiv
halafu weka chumvi!
ehehehheheheh Kaunga come zis way!
Mentor hebu do ze nidful kwa huyo kamwali af unoe mambo!
A LOT IN STORE FOR YU!
lol!
 
Last edited by a moderator:
Napenda mlendaa...lakini wa aina hii sijakula bado itabidi niufanyie majaribio...Ahsante kwa receipe
 
Mtolilo_matembele
pitiku au likolo la nanyungu_majan ya maboga
chimbembesu

hizo ndo mboga zetu a.k.a likolo kutoka songea.
Deo corleone_mwanza kwa muda.
 
ahahahhahah sijui ilinipitaje hiii!
pitiku bana haina makuu!
ni majani ya maboga
chumvi
maji
na kapilipili
unakata majani ya maboga vidogo dogo,unaweka maji,na pilipili unabadnika jikoni!
maji yakichemka unaweka mboga
inaiva kama dk 8-10 hiv
halafu weka chumvi!
ehehehheheheh Kaunga come zis way!
Mentor hebu do ze nidful kwa huyo kamwali af unoe mambo!
A LOT IN STORE FOR YU!
lol!

Duh! dada snowhite, a lot has hapenned between then and now.... :frusty::frusty::frusty::frusty:
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom