Mapinduzi Yaliyoshindwa ya DARUSO 2002/3

Status
Not open for further replies.
Where is Fransis Kayombo..bado ni engineer au ameshakuwa political engineer tayari
 
Nakubali kuwa Kayombo hawezi kugombea kupitia upinzani. Ni mwoga kidogo. Ila watu wanabadilika.
 
Sidhani kama kayombo ana element yoyote ya kuwa kiongozi maana hao ni wale ambao CCM ilikuwa inapandikiza kuvuruga mandeleo ya wanafunzi na serikali zao basi kwisha habari hata Deo ni type hiyo hiyo, tunawaita mapandikizi; Ruge alipandikizwa na Malecela John Samwel kumbukeni ndio wakati huo anajiandaa kugombea Urais, Zitto na Omar walikuwa wing ya kikwete then wakati Ruge anaondoka wakakubaliana na Malecela nani apewe kupitia kwa Mzee Mungai wakasema wana-trust kwa kayombo ndio chanzo cha yeye kuachiwa maana mwanzoni Albeto alikuwa kambi ya Malecela ila baada Zito akamchukua then akawa kambi yao. kwa ufupi siasa za DARUSO halisi ziilishia mwaka 2000; baada ya hapo ni chezo wa kuigiza na akili za tuition hata Engineering hiyo mnayo semakwa maana ya FoE miaka ya 2002 haikuwepo tena; naweza kusema serikali halisi ya siasa ya watu wenye kujua nini ya mwisho ni Kitila sijui kwa sasa nini kinaendelea maana hata zito wewe umwkuwa ukitumiwa sana na TIIS kumbuka ata mgomo uliperekea kuondoka kwa wakina Magabe na Marehem Mkiri wewe ulikuwa imformer wa serikali good day.
 
damn i feel ancient...
mkuu, ulikuwa ushasepa eeh?

Mi nakumbuka tulishushwa kwenye gari na rafiki yangu alichapwa kadhaa.
Zitto mi nakumbuka wewe na Alberto bana mlihusu, bila kumsahau Rizi.

tulipitiwa room baada ya room kuonywa tusiingie clas the next day vinginevyo.....

Wakati huo masikini mimi hata siasa za daruso nilikuwa sizielewi
 
kwani umekumbuka nini mkuu?

Nimekumbuka kwa Sababu Wahandisi tuliendesha Siasa za Nguvu kuanzia pale Nkurumah, lilipigwa Zengwe na Wagombea wengine wakashindwa kabisa Kujieleza, Ushindani Mkubwa ulikuwa kati ya Kayombo na Deo, Kwa Kweli kayombo aliperform kwa Kiwango cha Chini sana huwa najiuliza je Ule Mgomo haukuwa Mahsusi ili kumdisturb Kayombo Ashindwe kufanya Kazi ili Ionekane Wahandisi hawawezi?

Ila Siwezi kusahau Msisimko uliokuwepo kwenye zile Kampeni
 
Alberto sasa ni Diwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro na leo anachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo.
In our days wazee wa. FOE lazima upige kura ! Na unasaini kabisaa..hiyo ni 2000 wakati wa Kitila Mkumbo..not sure kama ndio alikuwa presdaa ama vipi?..however personnaly sioni kama a good freedom fighter can be the best kupewa wizara au urais..have watched my share of trade union leaders getting posns and fail..so do the freedom fighters they are needed to get the revolution on bt then step out watching trouble makers..not running the show!
 
salaam,

Ukweli kuhusu mapinduzi ya 2003.

Alberto aliongoza mapinduzi ya kipuuzi akishirikiana na haka kajamaa basi nakumbuka tuliandamana.... Msando are you there? can you tell us what happened?

maneno hayo hapo juu yana mapungufu mawili. kwanza mapinduzi yale hayakuwa ya kipuuzi. Pili sikushirikiana na Deo Mtui katika mapinduzi yale.

Kwangu binafsi na wote walioshiriki mapinduzi yale inabaki kuwa historia ya pekee katika masha yetu ya Mlimani.

Kilichotokea siku ya tukio ni mkutano ulioitishwa kwa ajili ya kujadili hoja ya mikopo na malipo ya field. Kipindi hicho mimi sikuwa kiongozi kwenye serikali ya Daruso. Wakati mkutano huo unaendelea nilipita eneo la Rev Square nikakuta wanafunzi wamekusanyika na ndipo nikaombwa kupanda jukwaani kutoa muongozo!

Baada ya kupanda jukwaani nilwataka wanafunzi tuwatafute viongozi wa Daruso, Bwana Kayombo na serikali yake ili watoe majibu kwa wanafunzi lakini hawakuwepo popote! Tukawatafuta 'wabunge' (class representatives') na wao wakawa wameingia mtini!!

Baada ya hapo nikatoa wazo kwamba hatuwezi kuendelea na mkutano ule Rev Square hivyo tuhamie Nkurumah Hall!! Hoja hiyo ilikubaliwa tukaelekea Nkurumah!

Kufika uwanja wa vita tukamkuta Prof. Issa Shivji akiwa anatoa lecture kwa wanafunzi wa mwaka wa pili Sheria. Nikamfuata mbele nikamwambia Prof tuna kazi ya kufanya tunaomba microphone. Alichosema Prof 'kama ni suala la kudai haki Albert the floor is all yours'. akafunga vitabu vyake akatuachia Nkurumah wanafunzi wakashika nafasi zao.

Kipindi chote hicho Zitto alikuwa mjini pamoja na Omar Ilyas nadhani. Nikawapigia simu kuwaambia kwamba Nkurumah moto umewaka tukubaliane way forward. Zitto alikuwa wa kwanza kusema hakuna kurudi nyuma tuendeleze shughuli ile. Hivyo hivyo Omar Ilyas.

Wakati wote huo hakukuwa na kiongozi wa Daruso anayeonekana!! Mtu ambaye nilikuwa nashirikiana nae ni Emanuel Mvula na ndiye aliyepokea mikoba yangu ya lecture ambayo sikuweza kuhudhuria tena!!

jambo la kwanza tulilokubaliana ni kuchagua Raisi wa muda ili aweze kuendesha shughuli zile. Lilipendekezwa jina la Bwana mmoja anayeitwa Siriwa lakini wanafunzi walipiga kelele kupinga ndipo jina langu likapendekezwa. Wanafunzi wote wakaridhia nikabeba jukumu la kuongoza wanafunzi kuelekea ofisi ya Dean. Kipindi hicho alikuwa Mama Kitula ndiye Dean. Tulipofika ofisini mwake ikawa mchakamchaka akinilaumu kwamba mimii ndiye chanzo cha mgomo huku akijua kabisa mimi sikuzuia mikopo wala posho za field kwa wanafunzi!! Akizidi kunilaumu kwamba nimevunja katiba ya Daruso ambayo mimi ndie nilikuwa Spika (Zitto waziri Mkuu, Ruge Raisi, Omar Ilyas waziri wa Haki za binadamu na engineo wengi) wakti inapitishwa na nilichangia kwa kiasi kikubwa kufanikiwa kwa kupitisha katiba hiyo.

Hayo yote hayakusaidia kwani baada ya malumbano ya muda mrefu wanafunzi walielekea ofisi za Daruso ambapo nilikabidhiwa rasmi desk la Kayombo. Kwa makusudi kabisa nikijua siasa za chuo niliwaashauri wanafunzi wote walioshiriki waweke saini zao na walifanya hivyo kuonyesha mshikamano!!

Muda ulikuwa umeenda sana tukakubaliana tulianzishe kesho yake. Kwa bahati mbaya siku iliyofuata hali ilikuwa tofauti! Usiku mapema polisi walizingira chuo ikiwa ni pamoja na vyumba vyetu vya kulala. Niliamka nikamfuata Zitto ambapo ikatulazimu kukimbilia Hall One kujificha. Kila aliyefungua chumba tulipogonga alipotuona alifunga mlango. Ikabidi tukimbilie Hall Three tukapata hifadhi kwa rafiki yetu mmoja (jina linahifadhiwa ni mke wa mtu sasa). Asubuhi Mary Mugurusi akaja kutuchukua kwenye gari yake akatupeleka Mabibo Hostel. Wakati tunapita maeneo ya Hall one polisi walikuwa bado wanarandaranda kututafuta! Tukaenda mpaka Mabibo Hostel tukapolewa na John Mnyika na rafiki yake Reginald. Hawa ndio watu waliotuhifadhi kwa muda na kutusaidia sana kwani tulikuwa choka mbaya!

Baada ya kujadiliana tuliamua kurudi chuo kudai barua zetu a kufukuzwa chuo. Tulipofika ofisi ya Dean akatuambia twende tukachukue Auxiliary polisi. Hapo shida ilianza ubishi kati ya Zitto na Dean kwamba kwa nini tukachukue barua polisi!! Ikabidi polisi waitwe watuletee barua zetu za kufukuzwa chuo!!

Tulipopokea tukaondoka na baada ya siku chache tulifanya mawasiliano na chuo tukaruhusiwa kufanya mitihani kwa masharti kwamba baada ya mitihani Disciplinary Hearing itafanyika kujua hatma yetu. Hayo yalifanyika. Kwenye Disciplinary Hearing tulikuwa tisa kama sikosei na baada yakutoa utetezi wetu mimi na Bwana Siriwa tulikuala 'rustication' ya miezi tisa!! wengine hawakukutwa na hatia.

Walichofanya uongozi wa chu ni kutugawa na walijua kabisa kwamba wanafunzi watakuwa busy na mitihani na baada ya hapo wataondoka kwenda makwao kwa hiyo uamuzi wowote usingekuwa na shida kutekeleza.

Wanafunzi waliporudi chuo hakuna aliyekumbuka kwamba Albert Msando na Siriwa wamesimamishwa kwa miezi tisa. Ikabidi kuanza kupambana kurudi chuo ili kumaliza Degree etu! Zitto na Omar wao walishamaliza hivyo chuo kikabaki na Bwana mmoja anaita Tweve kama mbishi aliyebaki na wengine wachache!

Baada ya kupambana tukarudishwa chuo kwa masharti makali kabisa. Kutokushiriki katika mkusanyiko wowote wa watu zaidi ya watano! Hata group discussion ikizidi watu watano inabidi tusishiriki!

Kwa kiasi kikubwa chuo kikawa kimepoteza hamasa ya migomo ya wanafunzi. Upole na sera za amani na utulivu zikatawala zaidi.

Wakati tunafika mwisho ukatokea Mgomo mwingine ambao na wenyewe haukufanikiwa. Nakumbuka Mabibo Hostel tulikusanyika baada ya mimi na John Mnyika kupanda gari usiku kutokea Morogoro kuwahi mgomo ambapo wanafunzi walijaa kwenye eneo la wazi la Mabibo lakini kuna gari iliingia getini wakadhani ni polisi hakuna alieybaki zaidi yangu na Mnyika! Kuanzia pale nikawaeleza wanafunzi hakuna wa kuendesha mgomo ukakamilika kutokana na woga ambao tayari umlishajengeka! Mnyika anawezakuuelezea zaidi mgomo huo!!

Mwisho, mgomo ambao ulikuwa na mafanikio ni ule ambao uliweza kushinikiza serikali kumuachia Marehe Gervas Mkil (RIP) na wanafunzi wengine wa Muhimbili kutoka rumande. Mgomo huo uliendeshwa na Zitto, Mimi, Rugemalira, Omary Ilyas na wengine siwakumbuki majina vizuri. Nakumbuka nilichaguliwa kwenda ITV kutoa Tamko kwamba wanafunzi warudi madarasani na Mkili atatoka. Nilienda na Raisi alieyekuwa anamaliza muda wake kwa jina la John wa Engineering (siyo John Kusaja). kitendo kile kidogo kiniletee shida kwa wanafunzi kwani wengi waliamini tumesaliti.

Nakumbuka nilikaa na Zitto nyuma ya Nkurumah hall tukiomba Mungu kwamba Prof Luhanga atimize ahadi yake ya Mkili kuachiwa!! Ahadi hiyo ilitimia na Mkili alisimama Nkurumah Hall akawasalimia wanafunzi! It was the happiest moment!

Tulitumia mafanikio hayo kumuuza Julius Rugemalira kama mgombea Urais dhidi ya Fundikira. Julius alishinda na Mkili na Fundikira wote walipewa wizara za kuongoza. Ila baada ya uchaguzi ule ambao uliwaingia madarakani baadhi yetu tuliokuwa tunaonekana ni wapiganaji matumaini ya wanafunzi yalipotea ghafla!!

Kutokuelewana kulianza mara moja, Raisi na Makamu, Zitto na Raisi, Albert na Zitto etc etc. Wan JF wengi wataelezea zaidi ile hali!!

Mpaka hapa niwachie wenzangu kusahihisha pale nilipokosea kutokana na kumbukumbu au vinginevyo!! Na pale ambapo nimesahau wengine waongezee kuweka historia sawa!!
 
Kwa sasa nipo Arusha, nina kampuni yangu ya uwakili, AlbertMsando Legal Consultants na kampuni ya bima, HakiYako Insurance Consultans. Vile vile ni Diwani wa Kata ya Mabogini Jimbo la Moshi vijijini. Niligombea nafasi ya Uenyekiti, nikiwa na madiwani wa TLP na CHADEMA 23, CCM wakiwa 22. Lakini matokeo yalipotangazwa nilikuwa na kura 22 CCM 23.

Kazi iliyoko mbele yangu nikumburuza Mkurugenzi mahakamani kama hatajibu barua yangu na kutoa maelekezo ya kuridhisha kuhusu uchaguzi ule. Barua hiyo nitaipost soon ili wanaJF waweze kuionana na kutoa mawazo yao!!
 
Atafutwe mtu anaitwa Siriwa ndiye anajua mkakati ulianzia wapi na akina nai walihusika. Hao hapo wanaotajwa wala hawakuwepo na waliokuwepo walidandia basi ndio maana lilizama. Niko Tite kusaka LEAKS ZA TANZANIA niacheni kwanza na hivi vijimambo vidogo vidogo. Wewe uliyechukua fedha za China kupitia benki fulani hivi inaanza na jina la N ama M nisubiri nabandika cable zako humu siku sii nyingi
 
Atafutwe mtu anaitwa Siriwa ndiye anajua mkakati ulianzia wapi na akina nai walihusika. Hao hapo wanaotajwa wala hawakuwepo na waliokuwepo walidandia basi ndio maana lilizama. Niko Tite kusaka LEAKS ZA TANZANIA niacheni kwanza na hivi vijimambo vidogo vidogo. Wewe uliyechukua fedha za China kupitia benki fulani hivi inaanza na jina la N ama M nisubiri nabandika cable zako humu siku sii nyingi

Join DateWed Dec 2010Posts1Thanks0

Unapokuja na shutuma kama hizi inabidi angalau uwe umepost atleast one credible story.... sio kwamba sikuamini lakini as you know so many wazushi around
 
Kudandia historia kumeifanya Tanganyika kutowashukuru na kuwaenzi watu halali walipogania uhuru wa nchi hii. Na hali hii ikaharibiwa na kuudwa kwa Tanzania ambako kukawa na lengo la kuficha historia ya Tanganyika kwa kuigeuzia jina la Tanzania Bara.

Nimemsoma Msando kwa umakini na uwazi ni huu kuwa mapinduzi hayo hakuwahi kushiriki kuyaandaa na hao wote aliowataja hawakuhusika katika maandalizi bali walidandia basi. tena anachanganya matukio, maandamano ya kushinikiza kuanchiwa kwa Mkili wala hata akina Mnyika hawajui kuta za chuo, yamefanyika wakati kukitakiwa kufanyika uchaguzi ambao uliahirishwa na kisha kuchaguliwa kwa Rugemalila na yeye Msando baadaye kuwa Spika. Nasikitika kama huyu mtu anaweza kusahau hata tukio linalohusu uchaguzi wake sasa aibuke kuandika historia tena ya jambo ambalo hakushiriki kuliandaa zaidi ya kulirukia. Nadhani anaweza kuja hapa kuomba radhi kwa kuwa alipitiwa na shughuli za kusaka uenyekiti wa halmashauri ambayo pole sana kaukosa! Nitarudi na hiyo ya TANleaks ya kigogo huyo ambaye amekuwa akichota fedha China, kumbuka kuwa Wikileaks imeionyesha Tanzania kuwa inakumbatia biashara za China.
 
Sidhani kama kayombo ana element yoyote ya kuwa kiongozi maana hao ni wale ambao CCM ilikuwa inapandikiza kuvuruga mandeleo ya wanafunzi na serikali zao basi kwisha habari hata Deo ni type hiyo hiyo, tunawaita mapandikizi; Ruge alipandikizwa na Malecela John Samwel kumbukeni ndio wakati huo anajiandaa kugombea Urais, Zitto na Omar walikuwa wing ya kikwete then wakati Ruge anaondoka wakakubaliana na Malecela nani apewe kupitia kwa Mzee Mungai wakasema wana-trust kwa kayombo ndio chanzo cha yeye kuachiwa maana mwanzoni Albeto alikuwa kambi ya Malecela ila baada Zito akamchukua then akawa kambi yao. kwa ufupi siasa za DARUSO halisi ziilishia mwaka 2000; baada ya hapo ni chezo wa kuigiza na akili za tuition hata Engineering hiyo mnayo semakwa maana ya FoE miaka ya 2002 haikuwepo tena; naweza kusema serikali halisi ya siasa ya watu wenye kujua nini ya mwisho ni Kitila sijui kwa sasa nini kinaendelea maana hata zito wewe umwkuwa ukitumiwa sana na TIIS kumbuka ata mgomo uliperekea kuondoka kwa wakina Magabe na Marehem Mkiri wewe ulikuwa imformer wa serikali good day.

DARUSO ni darudo tu, hata leo ipo, kuwa iliishia mwaka 2000 ni mtazamo wako akina Mtatiro wametokea wapi na wamemaliza lini mlimani?

Kuhusu Zito kwenye swala la Mkiri unamwonea sio kuwa namtetea, tulikuwa wote tukiimba nyimbo za solidarity forever na huku akipata misukosuko mingi ambayo ilimuyumbisha hata masomo, sijajua informer wa serikali ipi ambayo alikuwa restless kwayo!
 
salaam,

Ukweli kuhusu mapinduzi ya 2003.

Alberto aliongoza mapinduzi ya kipuuzi akishirikiana na haka kajamaa basi nakumbuka tuliandamana.... Msando are you there? can you tell us what happened?

maneno hayo hapo juu yana mapungufu mawili. kwanza mapinduzi yale hayakuwa ya kipuuzi. Pili sikushirikiana na Deo Mtui katika mapinduzi yale.

Kwangu binafsi na wote walioshiriki mapinduzi yale inabaki kuwa historia ya pekee katika masha yetu ya Mlimani.

Kilichotokea siku ya tukio ni mkutano ulioitishwa kwa ajili ya kujadili hoja ya mikopo na malipo ya field. Kipindi hicho mimi sikuwa kiongozi kwenye serikali ya Daruso. Wakati mkutano huo unaendelea nilipita eneo la Rev Square nikakuta wanafunzi wamekusanyika na ndipo nikaombwa kupanda jukwaani kutoa muongozo!

Baada ya kupanda jukwaani nilwataka wanafunzi tuwatafute viongozi wa Daruso, Bwana Kayombo na serikali yake ili watoe majibu kwa wanafunzi lakini hawakuwepo popote! Tukawatafuta 'wabunge' (class representatives') na wao wakawa wameingia mtini!!

Baada ya hapo nikatoa wazo kwamba hatuwezi kuendelea na mkutano ule Rev Square hivyo tuhamie Nkurumah Hall!! Hoja hiyo ilikubaliwa tukaelekea Nkurumah!

Kufika uwanja wa vita tukamkuta Prof. Issa Shivji akiwa anatoa lecture kwa wanafunzi wa mwaka wa pili Sheria. Nikamfuata mbele nikamwambia Prof tuna kazi ya kufanya tunaomba microphone. Alichosema Prof 'kama ni suala la kudai haki Albert the floor is all yours'. akafunga vitabu vyake akatuachia Nkurumah wanafunzi wakashika nafasi zao.

Kipindi chote hicho Zitto alikuwa mjini pamoja na Omar Ilyas nadhani. Nikawapigia simu kuwaambia kwamba Nkurumah moto umewaka tukubaliane way forward. Zitto alikuwa wa kwanza kusema hakuna kurudi nyuma tuendeleze shughuli ile. Hivyo hivyo Omar Ilyas.

Wakati wote huo hakukuwa na kiongozi wa Daruso anayeonekana!! Mtu ambaye nilikuwa nashirikiana nae ni Emanuel Mvula na ndiye aliyepokea mikoba yangu ya lecture ambayo sikuweza kuhudhuria tena!!

jambo la kwanza tulilokubaliana ni kuchagua Raisi wa muda ili aweze kuendesha shughuli zile. Lilipendekezwa jina la Bwana mmoja anayeitwa Siriwa lakini wanafunzi walipiga kelele kupinga ndipo jina langu likapendekezwa. Wanafunzi wote wakaridhia nikabeba jukumu la kuongoza wanafunzi kuelekea ofisi ya Dean. Kipindi hicho alikuwa Mama Kitula ndiye Dean. Tulipofika ofisini mwake ikawa mchakamchaka akinilaumu kwamba mimii ndiye chanzo cha mgomo huku akijua kabisa mimi sikuzuia mikopo wala posho za field kwa wanafunzi!! Akizidi kunilaumu kwamba nimevunja katiba ya Daruso ambayo mimi ndie nilikuwa Spika (Zitto waziri Mkuu, Ruge Raisi, Omar Ilyas waziri wa Haki za binadamu na engineo wengi) wakti inapitishwa na nilichangia kwa kiasi kikubwa kufanikiwa kwa kupitisha katiba hiyo.

Hayo yote hayakusaidia kwani baada ya malumbano ya muda mrefu wanafunzi walielekea ofisi za Daruso ambapo nilikabidhiwa rasmi desk la Kayombo. Kwa makusudi kabisa nikijua siasa za chuo niliwaashauri wanafunzi wote walioshiriki waweke saini zao na walifanya hivyo kuonyesha mshikamano!!

Muda ulikuwa umeenda sana tukakubaliana tulianzishe kesho yake. Kwa bahati mbaya siku iliyofuata hali ilikuwa tofauti! Usiku mapema polisi walizingira chuo ikiwa ni pamoja na vyumba vyetu vya kulala. Niliamka nikamfuata Zitto ambapo ikatulazimu kukimbilia Hall One kujificha. Kila aliyefungua chumba tulipogonga alipotuona alifunga mlango. Ikabidi tukimbilie Hall Three tukapata hifadhi kwa rafiki yetu mmoja (jina linahifadhiwa ni mke wa mtu sasa). Asubuhi Mary Mugurusi akaja kutuchukua kwenye gari yake akatupeleka Mabibo Hostel. Wakati tunapita maeneo ya Hall one polisi walikuwa bado wanarandaranda kututafuta! Tukaenda mpaka Mabibo Hostel tukapolewa na John Mnyika na rafiki yake Reginald. Hawa ndio watu waliotuhifadhi kwa muda na kutusaidia sana kwani tulikuwa choka mbaya!

Baada ya kujadiliana tuliamua kurudi chuo kudai barua zetu a kufukuzwa chuo. Tulipofika ofisi ya Dean akatuambia twende tukachukue Auxiliary polisi. Hapo shida ilianza ubishi kati ya Zitto na Dean kwamba kwa nini tukachukue barua polisi!! Ikabidi polisi waitwe watuletee barua zetu za kufukuzwa chuo!!

Tulipopokea tukaondoka na baada ya siku chache tulifanya mawasiliano na chuo tukaruhusiwa kufanya mitihani kwa masharti kwamba baada ya mitihani Disciplinary Hearing itafanyika kujua hatma yetu. Hayo yalifanyika. Kwenye Disciplinary Hearing tulikuwa tisa kama sikosei na baada yakutoa utetezi wetu mimi na Bwana Siriwa tulikuala 'rustication' ya miezi tisa!! wengine hawakukutwa na hatia.

Walichofanya uongozi wa chu ni kutugawa na walijua kabisa kwamba wanafunzi watakuwa busy na mitihani na baada ya hapo wataondoka kwenda makwao kwa hiyo uamuzi wowote usingekuwa na shida kutekeleza.

Wanafunzi waliporudi chuo hakuna aliyekumbuka kwamba Albert Msando na Siriwa wamesimamishwa kwa miezi tisa. Ikabidi kuanza kupambana kurudi chuo ili kumaliza Degree etu! Zitto na Omar wao walishamaliza hivyo chuo kikabaki na Bwana mmoja anaita Tweve kama mbishi aliyebaki na wengine wachache!

Baada ya kupambana tukarudishwa chuo kwa masharti makali kabisa. Kutokushiriki katika mkusanyiko wowote wa watu zaidi ya watano! Hata group discussion ikizidi watu watano inabidi tusishiriki!

Kwa kiasi kikubwa chuo kikawa kimepoteza hamasa ya migomo ya wanafunzi. Upole na sera za amani na utulivu zikatawala zaidi.

Wakati tunafika mwisho ukatokea Mgomo mwingine ambao na wenyewe haukufanikiwa. Nakumbuka Mabibo Hostel tulikusanyika baada ya mimi na John Mnyika kupanda gari usiku kutokea Morogoro kuwahi mgomo ambapo wanafunzi walijaa kwenye eneo la wazi la Mabibo lakini kuna gari iliingia getini wakadhani ni polisi hakuna alieybaki zaidi yangu na Mnyika! Kuanzia pale nikawaeleza wanafunzi hakuna wa kuendesha mgomo ukakamilika kutokana na woga ambao tayari umlishajengeka! Mnyika anawezakuuelezea zaidi mgomo huo!!

Mwisho, mgomo ambao ulikuwa na mafanikio ni ule ambao uliweza kushinikiza serikali kumuachia Marehe Gervas Mkil (RIP) na wanafunzi wengine wa Muhimbili kutoka rumande. Mgomo huo uliendeshwa na Zitto, Mimi, Rugemalira, Omary Ilyas na wengine siwakumbuki majina vizuri. Nakumbuka nilichaguliwa kwenda ITV kutoa Tamko kwamba wanafunzi warudi madarasani na Mkili atatoka. Nilienda na Raisi alieyekuwa anamaliza muda wake kwa jina la John wa Engineering (siyo John Kusaja). kitendo kile kidogo kiniletee shida kwa wanafunzi kwani wengi waliamini tumesaliti.

Nakumbuka nilikaa na Zitto nyuma ya Nkurumah hall tukiomba Mungu kwamba Prof Luhanga atimize ahadi yake ya Mkili kuachiwa!! Ahadi hiyo ilitimia na Mkili alisimama Nkurumah Hall akawasalimia wanafunzi! It was the happiest moment!

Tulitumia mafanikio hayo kumuuza Julius Rugemalira kama mgombea Urais dhidi ya Fundikira. Julius alishinda na Mkili na Fundikira wote walipewa wizara za kuongoza. Ila baada ya uchaguzi ule ambao uliwaingia madarakani baadhi yetu tuliokuwa tunaonekana ni wapiganaji matumaini ya wanafunzi yalipotea ghafla!!

Kutokuelewana kulianza mara moja, Raisi na Makamu, Zitto na Raisi, Albert na Zitto etc etc. Wan JF wengi wataelezea zaidi ile hali!!

Mpaka hapa niwachie wenzangu kusahihisha pale nilipokosea kutokana na kumbukumbu au vinginevyo!! Na pale ambapo nimesahau wengine waongezee kuweka historia sawa!!

Mkuu umeeleza kila kitu. Umenikumbusha sana kile kipindi. Nilikuwepo bega kwa bega, nina kukumbuka sana maana ulikuwa na ushawishi mkubwa sana pale chuo. Kinachonishangaza ni kwamba sikukusikia tena kwneye siasa maana nilitegemea sana ungekuwa bungeni. The last time we met in arusha.

Kuna mtu anaitwa KENGELE zile enzi zetu, sijamsikia hapa. Huyu jamaa alikuwa tofauti yaani very few of this kind wako hii dunia. Aliweza kutofautiana na wanafunzi wooote lakini akashikilia msimamo wake hata kama maisha yake yalikuwa hatarini. Nakumbuka naye alisimama pale r-square.

Those were the real university days. Nilijifunza mengi na nafikiri ndo kwa mara ya kwanza bomu la mchozi liliangukia mguuni kwangu.
 
kikwete alipona vp kupinduliwa kipindi chake?...mbona ni kiongozi dhaifu sana?......au hata wasomi wakipingi kilewalikuwawanafagilia zaidisura?.........siamini
 
kikwete alipona vp kupinduliwa kipindi chake?...mbona ni kiongozi dhaifu sana?......au hata wasomi wakipingi kilewalikuwawanafagilia zaidisura?.........siamini

H.C Dk. Kikwete hakuwahi kuwa Rais wa DARUSO
 
Sasa hayo mapinduzi yalishindwaje? Nani alimkwamua kayombo baada ya kufutwa na kundi la kina msando?? Bunge na daruso board ilikuwa na msimamo gani katika mapinduzi hayo?? Anayekumbuka tafadhali!!!
 
salaam,

Ukweli kuhusu mapinduzi ya 2003.

Alberto aliongoza mapinduzi ya kipuuzi akishirikiana na haka kajamaa basi nakumbuka tuliandamana.... Msando are you there? can you tell us what happened?

maneno hayo hapo juu yana mapungufu mawili. kwanza mapinduzi yale hayakuwa ya kipuuzi. Pili sikushirikiana na Deo Mtui katika mapinduzi yale.

Kwangu binafsi na wote walioshiriki mapinduzi yale inabaki kuwa historia ya pekee katika masha yetu ya Mlimani.

Kilichotokea siku ya tukio ni mkutano ulioitishwa kwa ajili ya kujadili hoja ya mikopo na malipo ya field. Kipindi hicho mimi sikuwa kiongozi kwenye serikali ya Daruso. Wakati mkutano huo unaendelea nilipita eneo la Rev Square nikakuta wanafunzi wamekusanyika na ndipo nikaombwa kupanda jukwaani kutoa muongozo!

Baada ya kupanda jukwaani nilwataka wanafunzi tuwatafute viongozi wa Daruso, Bwana Kayombo na serikali yake ili watoe majibu kwa wanafunzi lakini hawakuwepo popote! Tukawatafuta 'wabunge' (class representatives') na wao wakawa wameingia mtini!!

Baada ya hapo nikatoa wazo kwamba hatuwezi kuendelea na mkutano ule Rev Square hivyo tuhamie Nkurumah Hall!! Hoja hiyo ilikubaliwa tukaelekea Nkurumah!

Kufika uwanja wa vita tukamkuta Prof. Issa Shivji akiwa anatoa lecture kwa wanafunzi wa mwaka wa pili Sheria. Nikamfuata mbele nikamwambia Prof tuna kazi ya kufanya tunaomba microphone. Alichosema Prof 'kama ni suala la kudai haki Albert the floor is all yours'. akafunga vitabu vyake akatuachia Nkurumah wanafunzi wakashika nafasi zao.

Kipindi chote hicho Zitto alikuwa mjini pamoja na Omar Ilyas nadhani. Nikawapigia simu kuwaambia kwamba Nkurumah moto umewaka tukubaliane way forward. Zitto alikuwa wa kwanza kusema hakuna kurudi nyuma tuendeleze shughuli ile. Hivyo hivyo Omar Ilyas.

Wakati wote huo hakukuwa na kiongozi wa Daruso anayeonekana!! Mtu ambaye nilikuwa nashirikiana nae ni Emanuel Mvula na ndiye aliyepokea mikoba yangu ya lecture ambayo sikuweza kuhudhuria tena!!

jambo la kwanza tulilokubaliana ni kuchagua Raisi wa muda ili aweze kuendesha shughuli zile. Lilipendekezwa jina la Bwana mmoja anayeitwa Siriwa lakini wanafunzi walipiga kelele kupinga ndipo jina langu likapendekezwa. Wanafunzi wote wakaridhia nikabeba jukumu la kuongoza wanafunzi kuelekea ofisi ya Dean. Kipindi hicho alikuwa Mama Kitula ndiye Dean. Tulipofika ofisini mwake ikawa mchakamchaka akinilaumu kwamba mimii ndiye chanzo cha mgomo huku akijua kabisa mimi sikuzuia mikopo wala posho za field kwa wanafunzi!! Akizidi kunilaumu kwamba nimevunja katiba ya Daruso ambayo mimi ndie nilikuwa Spika (Zitto waziri Mkuu, Ruge Raisi, Omar Ilyas waziri wa Haki za binadamu na engineo wengi) wakti inapitishwa na nilichangia kwa kiasi kikubwa kufanikiwa kwa kupitisha katiba hiyo.

Hayo yote hayakusaidia kwani baada ya malumbano ya muda mrefu wanafunzi walielekea ofisi za Daruso ambapo nilikabidhiwa rasmi desk la Kayombo. Kwa makusudi kabisa nikijua siasa za chuo niliwaashauri wanafunzi wote walioshiriki waweke saini zao na walifanya hivyo kuonyesha mshikamano!!

Muda ulikuwa umeenda sana tukakubaliana tulianzishe kesho yake. Kwa bahati mbaya siku iliyofuata hali ilikuwa tofauti! Usiku mapema polisi walizingira chuo ikiwa ni pamoja na vyumba vyetu vya kulala. Niliamka nikamfuata Zitto ambapo ikatulazimu kukimbilia Hall One kujificha. Kila aliyefungua chumba tulipogonga alipotuona alifunga mlango. Ikabidi tukimbilie Hall Three tukapata hifadhi kwa rafiki yetu mmoja (jina linahifadhiwa ni mke wa mtu sasa). Asubuhi Mary Mugurusi akaja kutuchukua kwenye gari yake akatupeleka Mabibo Hostel. Wakati tunapita maeneo ya Hall one polisi walikuwa bado wanarandaranda kututafuta! Tukaenda mpaka Mabibo Hostel tukapolewa na John Mnyika na rafiki yake Reginald. Hawa ndio watu waliotuhifadhi kwa muda na kutusaidia sana kwani tulikuwa choka mbaya!

Baada ya kujadiliana tuliamua kurudi chuo kudai barua zetu a kufukuzwa chuo. Tulipofika ofisi ya Dean akatuambia twende tukachukue Auxiliary polisi. Hapo shida ilianza ubishi kati ya Zitto na Dean kwamba kwa nini tukachukue barua polisi!! Ikabidi polisi waitwe watuletee barua zetu za kufukuzwa chuo!!

Tulipopokea tukaondoka na baada ya siku chache tulifanya mawasiliano na chuo tukaruhusiwa kufanya mitihani kwa masharti kwamba baada ya mitihani Disciplinary Hearing itafanyika kujua hatma yetu. Hayo yalifanyika. Kwenye Disciplinary Hearing tulikuwa tisa kama sikosei na baada yakutoa utetezi wetu mimi na Bwana Siriwa tulikuala 'rustication' ya miezi tisa!! wengine hawakukutwa na hatia.

Walichofanya uongozi wa chu ni kutugawa na walijua kabisa kwamba wanafunzi watakuwa busy na mitihani na baada ya hapo wataondoka kwenda makwao kwa hiyo uamuzi wowote usingekuwa na shida kutekeleza.

Wanafunzi waliporudi chuo hakuna aliyekumbuka kwamba Albert Msando na Siriwa wamesimamishwa kwa miezi tisa. Ikabidi kuanza kupambana kurudi chuo ili kumaliza Degree etu! Zitto na Omar wao walishamaliza hivyo chuo kikabaki na Bwana mmoja anaita Tweve kama mbishi aliyebaki na wengine wachache!

Baada ya kupambana tukarudishwa chuo kwa masharti makali kabisa. Kutokushiriki katika mkusanyiko wowote wa watu zaidi ya watano! Hata group discussion ikizidi watu watano inabidi tusishiriki!

Kwa kiasi kikubwa chuo kikawa kimepoteza hamasa ya migomo ya wanafunzi. Upole na sera za amani na utulivu zikatawala zaidi.

Wakati tunafika mwisho ukatokea Mgomo mwingine ambao na wenyewe haukufanikiwa. Nakumbuka Mabibo Hostel tulikusanyika baada ya mimi na John Mnyika kupanda gari usiku kutokea Morogoro kuwahi mgomo ambapo wanafunzi walijaa kwenye eneo la wazi la Mabibo lakini kuna gari iliingia getini wakadhani ni polisi hakuna alieybaki zaidi yangu na Mnyika! Kuanzia pale nikawaeleza wanafunzi hakuna wa kuendesha mgomo ukakamilika kutokana na woga ambao tayari umlishajengeka! Mnyika anawezakuuelezea zaidi mgomo huo!!

Mwisho, mgomo ambao ulikuwa na mafanikio ni ule ambao uliweza kushinikiza serikali kumuachia Marehe Gervas Mkil (RIP) na wanafunzi wengine wa Muhimbili kutoka rumande. Mgomo huo uliendeshwa na Zitto, Mimi, Rugemalira, Omary Ilyas na wengine siwakumbuki majina vizuri. Nakumbuka nilichaguliwa kwenda ITV kutoa Tamko kwamba wanafunzi warudi madarasani na Mkili atatoka. Nilienda na Raisi alieyekuwa anamaliza muda wake kwa jina la John wa Engineering (siyo John Kusaja). kitendo kile kidogo kiniletee shida kwa wanafunzi kwani wengi waliamini tumesaliti.

Nakumbuka nilikaa na Zitto nyuma ya Nkurumah hall tukiomba Mungu kwamba Prof Luhanga atimize ahadi yake ya Mkili kuachiwa!! Ahadi hiyo ilitimia na Mkili alisimama Nkurumah Hall akawasalimia wanafunzi! It was the happiest moment!

Tulitumia mafanikio hayo kumuuza Julius Rugemalira kama mgombea Urais dhidi ya Fundikira. Julius alishinda na Mkili na Fundikira wote walipewa wizara za kuongoza. Ila baada ya uchaguzi ule ambao uliwaingia madarakani baadhi yetu tuliokuwa tunaonekana ni wapiganaji matumaini ya wanafunzi yalipotea ghafla!!

Kutokuelewana kulianza mara moja, Raisi na Makamu, Zitto na Raisi, Albert na Zitto etc etc. Wan JF wengi wataelezea zaidi ile hali!!

Mpaka hapa niwachie wenzangu kusahihisha pale nilipokosea kutokana na kumbukumbu au vinginevyo!! Na pale ambapo nimesahau wengine waongezee kuweka historia sawa!!


Hii chai yako haijakaa vizuri umetia sukari sna wewe hauna uwezo huo; we ni mtu wa wanawake inasemekana ulikuwa Biz na mtoto mmoja wa Kike Mkerewe babae akiwa Lecturer UDSM; sidhani kama unaweza kuwa robo ya Omary na Chembe ya Zitto Zuberi, alafu mbona una ID Mbili humu katika hii story??!!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom