Mapinduzi ya Zanzibar: Ukweli ni Upi?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,582
Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
Kwa heri ukoloni kwaheri uhuru.jpeg

kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe amiri jeshi hakuwa Mganda John Okello pekee, bali pia Mkello yumo?!.

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Jee wale mashuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, hayakutekelezwa na wapinga Mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar,
Zanzibar- John Okello.jpeg

yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya Mapinduzi Matukufuya ya Zanzibar nayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, ya Zanzibar?.
Jee yalipangwa na nani? Yalitekelezwaje?.
Nini haswa kilichotokea usiku ule wa Januari 11?.
Nani alifanya nini wapi?
Na mwisho tuzungumzie wafaidika wa Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar na bila kuwasahau wahanga wa Mapinduzi hayo ambao kwako yatakuwa sio Matukufu, ni kina nani haswa?, na kama kuleta amani na utangamano wa Zanzibar kuhusu Mapinduzi hayo kutahitajika kuundwa kwa Tume ya Ukweli na Upatanisho, "Truth and Reconciliation Commission" ili waliohasimiana kutokana na Mapinduzi hayo, wapatanishwe kwa maslahi mapana ya Zanzibar?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.


Pasco
Rejea za Mwandishi huyu kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
  1. Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
  2. Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
  3. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari
 
mmmh kwa kweli sijakisoma

kama kuna uwezekano wa kuwekwa tukakipitia si vibaya

maana walioshiriki kwenye mapinduzi wanajulikana na wengine walikuwa Polisi hapo Zanzibar na wengine ni wakwezi na wakulima

siwezi kukataa au kukubali hadi tusome na kuangalia hizo findings zake amazitoa kwenye vianzio vipi

hata hivyo historia ina ncha nyingi kila mtu akieleza ncha yake mwisho wasomaji wanapata kitu kizima
 
nakubaliana na wewe kua karume aliuawa na wanamapinduzi wa kweli, sababu kubwa ni ukatili wake na jinsi alivyokua anaua watu hovyo akiogopa kuopinduliwa, humud mwanajeshi aliyempiga risasi karume pale kisiwa ndui alikua ni mmoja ya watu waliopoteza baba kwa mkono wa karume, toka humud anasoma mafunzo ya jeshi urusi aliweka nadhiri ya kulipiza kisasi icho.

sikubaliani na wewe kua mapinduzi yaliendeshwa na low life kama hao, mapinduzi yalifanywa na vijana wa kikomunisti waliopata mafunzo ya nchini cuba, hata mpango mzima uliandaliwa na msaada mkubwa kutoka cuba, kina abdulahaman babu, kassim hanga na wengine waliosoma cuba ndio hasa walioratibu mpango mzima karume alikua kwanza hajasoma hakua na uwezo wa kuandaa mpango ule, yeye alichukuliwa huku tu bara akaenda pewa urais!
 
Ni watu wa Okello na planner mkubwa alikuwa Mwalimu Nyerere. Kuna clip ya (motion picture) iliyochukuliwa na helikopta (au ndege ndogo) iliyotoka katika manowari ya Australia (au Uingereza?) iliyokuwa jirani na Zanzibar siku hiyo ambayo ilichukuwa picha kutoka angani ikionyesha jinsi Waarabu (wakiwemo wanawake na watoto) walivyokuwa wanakimbizwa na watu wenye bunduki kuelekea ufukweni ambako huko walikuta makaburi (mass graves) yaliyochimbwa tayari na kumiminiwa risasi na kuangukia humo. Kulikuwa hakuna mapanga -- nadhani zilikuwa ni bunduki aina ya Marker Four. Hivi yale makaburi hayakupatikana?

Mwenye clip hii atuwekee hapa -- kwa upande mmoja inasikitisha sana maana ilikuwa kama vile (nimeiona picha moja) ya wale askari wa kiNazi wa Hitler walivyokuwa wakiwaua Wayahudi baada ya wao kulazimishwa kuchimba makaburi (mass graves) na kisha kuvuliwa nguo zote huku wanawake wakiwabeba vichanga vyao! Lakini hii ndiyo historia ya dunia, lakini huko kwenye karne za nyuma zaidi ukatili ulikuwa mkubwa zaidi.
 
Naweza kukubaliana na taarifa kuwa wakina Babu na Hanga na wenzao waliosoma Cuba ndio walikuwa brain behind the plotting of the 1964 Zanzibar revolution; kwani mimi binafsi nakunbuka siku moja kabla ya mapinduzi Abdulhaman Babu alikuwa anapata kinywaji pale Palm Beach hotel na vijana wengi wa kizenj na siku ile ya mapinduzi usiku aliondoka kwa mtumbwi kuelekea visiwani!! Mkitaka uthibitisho zaidi wa mambo yalivyopangwa muulizeni Salim Msoma aliyekuwa katibu mkuu wizara ya miundombinu!!
 
Ni watu wa Okello na planner mkubwa alikuwa Mwalimu Nyerere. Kuna clip ya (motion picture) iliyochukuliwa na helikopta (au ndege ndogo) iliyotoka katika manowari ya Australia (au Uingereza?) iliyokuwa jirani na Zanzibar siku hiyo ambayo ilichukuwa picha kutoka angani ikionyesha jinsi Waarabu (wakiwemo wanawake na watoto) walivyokuwa wanakimbizwa na watu wenye bunduki kuelekea ufukweni ambako huko walikuta makaburi (mass graves) yaliyochimbwa tayari na kumiminiwa risasi na kuangukia humo. Kulikuwa hakuna mapanga -- nadhani zilikuwa ni bunduki aina ya Marker Four. Hivi yale makaburi hayakupatikana?

Mwenye clip hii atuwekee hapa -- kwa upande mmoja inasikitisha sana maana ilikuwa kama vile (nimeiona picha moja) ya wale askari wa kiNazi wa Hitler walivyokuwa wakiwaua Wayahudi baada ya wao kulazimishwa kuchimba makaburi (mass graves) na kisha kuvuliwa nguo zote huku wanawake wakiwabeba vichanga vyao! Lakini hii ndiyo historia ya dunia, lakini huko kwenye karne za nyuma zaidi ukatili ulikuwa mkubwa zaidi.

mkuu, hii ni nzito sana, tena sana....unaweza kutukumbusha ni wapi uliiona hiyo clip ili tusaidiane kuitafuta??
 
Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho 'Kwaheri Ukoloni Zanzibar, Kwaheri Uhuru Zanzibar' kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said, kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe mapinduzi ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe am,iri jeshi hakuwa Okello peke yake, pia Mkello yumo?.).

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Wale mashuhuda wa mapinduzi yale matukufu, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, haykutekelezwa na wapinga mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar, yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya mapinduzi hayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, yalipangwa na nani, yalitekelezwaje, nini haswa kilichotokea, nani alifanya nini wapi? na wahanga ni kina nani haswa?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.

Tukizembea, historia ya kweli ya mapinduzi ya Zanzibar haitajulikana kamwe, ni wajibu wetu kuufahamu ukweli kwa faida ya vizazi vijavyo...
 
Kwa tuliozaliwa baada ya mapinduzi ndio tunazidi kuchanganywa zaidi, hatuelewi nani ni nani maana kila siku yanaibuka mapya! Kwa kweli kuna haja ya historia ya mapinduzi kuandikwa upya na sio sasa ambapo kila mtu anasema yake kulingana na namna alivyoathirika na mapinduzi hayo!
 
Kwa tuliozaliwa baada ya mapinduzi ndio tunazidi kuchanganywa zaidi, hatuelewi nani ni nani maana kila siku yanaibuka mapya! Kwa kweli kuna haja ya historia ya mapinduzi kuandikwa upya na sio sasa ambapo kila mtu anasema yake kulingana na namna alivyoathirika na mapinduzi hayo!

Historia haijulikani kwasababu kumekuwa na version tofauti kuhusu nini kilijiri nani alihusika na kwa vipi. Mimi binafsi nimesoma theory kama 3 ambazo zote zinachanganya tu. Wajumbe wa baraza la mapinduzi, ambao wanajua jinsi ''tombola'' lilivyopangwa, baadhi wapo hai kabisa, hawa wasipobanwa kueleza ukweli historia itafutika. Sina uhakika lakini nadhani wafuatao wanaweza kuwemo katika baraza la mapinduzi au wanajua nani alikuwemo: Mzee Hassan N Moyo, Abdalah Natepe, Aboud Jumbe, Ali Hassan M,
 
Ni watu wa Okello na planner mkubwa alikuwa Mwalimu Nyerere. Kuna clip ya (motion picture) iliyochukuliwa na helikopta (au ndege ndogo) iliyotoka katika manowari ya Australia (au Uingereza?) iliyokuwa jirani na Zanzibar siku hiyo ambayo ilichukuwa picha kutoka angani ikionyesha jinsi Waarabu (wakiwemo wanawake na watoto) walivyokuwa wanakimbizwa na watu wenye bunduki kuelekea ufukweni ambako huko walikuta makaburi (mass graves) yaliyochimbwa tayari na kumiminiwa risasi na kuangukia humo. Kulikuwa hakuna mapanga -- nadhani zilikuwa ni bunduki aina ya Marker Four. Hivi yale makaburi hayakupatikana?

Mwenye clip hii atuwekee hapa -- kwa upande mmoja inasikitisha sana maana ilikuwa kama vile (nimeiona picha moja) ya wale askari wa kiNazi wa Hitler walivyokuwa wakiwaua Wayahudi baada ya wao kulazimishwa kuchimba makaburi (mass graves) na kisha kuvuliwa nguo zote huku wanawake wakiwabeba vichanga vyao! Lakini hii ndiyo historia ya dunia, lakini huko kwenye karne za nyuma zaidi ukatili ulikuwa mkubwa zaidi.

Mkuu,
Naamini clip unayoiongelea nitakuwa nimeshaiona na iko coloured. With all honesty, I think it a fake one, simply enacted to document the event. Most genuine video clips currently available to highlight events that took place on that day are short, black & white footages lasting not longer than 3mins.
 
st Julius Nyerere was 100% behind the "Mapindunzi Daima": Babu and Hanga were the part of it! Okello was a protegee of Mkello
 
Ndugu yangu usipoteze muda mapinduzi haya yalikuwa mfano wa tamthiliya, jaribu kupitia nchi zilizopitia mapinduzi ya kweli,utaona watu wanavyojivunia asili zao sasa rudi kwa hawa ndugu zetu wa kiunguja asili bora wanayoiona wao ni ya kiaarabu, maana halisi ya mapinduzi hawaijui ndio maana kila kukicha utasikia hadithi mpya za mapinduzi haya, si rahisi kupata ukweli wa haya mapinduzi kwani wahusika wengi walikimbilia kuoa wanawake wa kiarabu baada ya mapinduzi, matokeo yake kutokana na kuwanyenyekea wake wapya wa kiarabu waliweza kupotosha ukweli wa maneno angalia baraza zima (asili) linaloitwa la mapinduzi angalia wake utaona ukweli wa jambo hilo, watu ambao wanaweza kutupa ukweli wa tamthiliya hii wote ni marehemu (Mwl. Nyerere na Karume) (RIP), kwa sasa hivi acha tuchukue maneno yao, hizo hadithi za kina Ghassany waachie wenyewe, hata wewe ukitaka kuandika historia unaweza pesa yako tu, huyu Ghassany ameandika kitabu hicho kwa uchungu wa Zanzibar au ni mwendelezo wa tamthiliya ya kiarabu? Ukweli wa mapinduzi haya utaupata waunguja watakapokuwa na mapinduzi ya kweli ndani ya nafsi zao.
 
Mkuu,
Naamini clip unayoiongelea nitakuwa nimeshaiona na iko coloured. With all honesty, I think it a fake one, simply enacted to document the event. Most genuine video clips currently available to highlight events that took plac on that day are short, black & white footages lasting not longer than 3mins.

Naona umezowea ile mikanda ya zamani,ok mimi ninazo original nitafute nikupe,bt almost aloongea zak malang ni kweli tupu..

Na kahusu historia ya znz ipo wazi kabisa.. pamoja na woote hao watajwa ambao wamehusika,lkn planner na command zoote zilikuwa zinatoka kwa Mr X (Nyerere), Dorado bado yupo mfateni akupeni dataz.. na yeye huyu alikuwa ana sapport kutoka baadhi ya mataifa makubwa..
 
Kosa la Nyerere lilikuwa lipi? mapinduzi yanapofanyika damu haina budi kumwagika, hasa ukizingatia mapinduzi haya yalikuwa ni kuondoa dhuluma za kiarabu. Sijawahi kusikia mapinduzi yakisindikizwa kwa nyimbo za taarabu, sasa anayeshangaa watu waliuliwa anashangaa kitu gani? waarabu waliuwa na walinyanyasa waafrika haikuwa ajabu na wao kuuwawa wakati wa mapinduzi. Mapinduzi yalikuwa sahihi na lengo kubwa ilikuwa kuondoa utawala wa kiarabu.
 
Mapinduzi ya Zanzibar yalipikwa na USSR (Urusi) na nchi washirika Cuba na Ujerumani Mashariki,siku hizo za vita baridi.Mrusi alikuwa anatafuta njia za kujipenyeza ukanda wa Afrika Mashariki,lakini ilikuwa ni vigumu sababu mahasimu wake walikuwa bado wana nguvu katika yaliyokuwa makoloni yao na yaliokuwa bado ni makoloni yao,Tanganyika, Kenya,Somalia,Zanzibar,Mozambique,Afrika Kusini,Uganda,Visiwa vya Comoro,Visiwa vya Usheri Sheli n.k.Hivyo walianzinsha mpango wa muda mrefu wakupeleka vijana wa kiafrika kutoka nchi hizo kuchukua masomo katika Urusi,Cuba,East Germany,Yugoslavia nk.Wanafunzi kutoka Zanzibar akina marehemu kanali Mahafudhi na wenzake walikwenda huko Cuba ndipo walipata mafunzo ya kijeshi.Kilichokuwa kinatafutwa kwa Russia ni upenyo wa kuingia Afrika Mashariki.Majasusi wa kirusi wakijua fika hali harisi ya utawala wa Sultani wa Zanzibar,na utata katika chaguzi,wakatumia wale waliokuwa wanafunzi kupanga mapinduzi,kwa kujipenyeza katika vyama vya siasa vilivyokuwa vinapigania kumgoa sultani na kutoa ushawishi mkubwa ndani ya vyama na wananchi kwa ujumla.Wananchi wakaamasika,polisi wakaasi,maghala ya silaha yakafunjwa,vita kati ya waarabu na waafrika ikalipuka.Sultani akapinduliwa akakimbilia Mombasa Kenya,akafukuzwa na Raisi Jomo Kenyata.Raisi Nyerere wa Tanganyika aliruhusu meli yake kutia nanga Dar-es-Salaam kama safe passage kwenda Uingereza.Baada ya kuundwa serikali ya Mapinduzi Warusi waliishawishi serikali ya Zanzibar kuondoa ground sattelite kubwa ya Marekani.Marekani alingoa sattelite yake,labda ndio sababu ya mshirika wa Marekani Italy alijenga ground Satellite kubwa huko Kenya Malindi kwenye kisiwa kidogo kijulikanacho kama San Marino mwaka 1964 kama subtitute ya ile iliongolewa Zanzibar.Marekani alishtuka na mwenendo wa serikali ya Mapinduzi iliokuwa ina makomredi ndani yake akina Marehemu Babu na wenzake,likatengenezwa zengwe la kuunganisha Tanganyika na Zanzibar katika siku 100,kwa kile kilichozaa serikali mbili za Tanzania.
 
nyie mnaokwepa kueleza sababu halisi ya mapinduzi mnakwepa kitu gani na kwa maslahi ya nani? leo imezuka hadithi mpya ya warusi kesho sijui itakuwaje.
 
Back
Top Bottom