Mapinduzi hayaletwi na watu wanaofurahia viyoyozi maofisini; ni hao walala hoi tunaowaona mitaani

everybody

JF-Expert Member
Oct 30, 2010
337
103
Huwa nawashangaa sana watu wanaowabeza walalahoi kama wamachinga, wapiga debe and vijana wa mtaani kujihusisha na kushabikia matukio (kama vile maandamano na mikutano ya hadhara) yanayolenga kufikisha ujumbe kwa ajili ya kuboresha maisha ya mtanzania. Siku zote hawa ndio watu wanaoguswa na hali duni ya maisha na siku zote ndio watakua wa kwanza kwenye matukio kama haya. Tunahitaji viongozi wachache tu kama wanavyofanya viongozi wa CHADEMA kwa sasa kuwaongoza jinsi watakavyoweza kutimiza azma yao ya kupata maisha bora.
Hivyo nawashangaa sana watu wanaokaa kubeza mikutano na maandamano ya wanamapinduzi Tanzania eti imejaa wavuta bangi, wezi na vijana wasio na la kufanya. Kwa hali halisi hawa ndio wenye kujua uchungu wa maisha magumu ya Tanzania na siku zote ndio watakua mstari wa mbele na ni halali yao kufanya hivyo. Wewe unashinda ofisini ukienjoy kiyoyozi huwezi kujua hali ngumu wanayokutana watu wa mitaani. Sana sana wewe hali ngumu utakayoiongelea ni kwamba umekosa hela ya kukaa kwenye kiti kirefu kunywa bia kumi na badala yake unakunywa mbili ili upate hela ya kumpeleka mtoto wako Academia school. Mwenzako mlala hoi anayeingia kwenye maandamano hana hata uhakika wa hiyo hela ya kupata sembe la mchana. Walala hoi wanaoingia mtaana kudai haki ya maisha bora kwa sababu wamekosa ajira na hawana jinsi ya kujipatia kipato kutimiza mahitaji yao ya msingi inabidi wapewe support badala ya kuwabeza. Watu kama hawa ndio wanaowasaidie nyie mnaokuwa kwenye maofisi yenu kufikisha ujumbe.

Nawasilisha..
 
Mkuu nimekugongea thnks hapo, mageuzi hayategemei watu wanaokaa nyuma ya keyboard na kuanza kutoa maelezo mareeefu ya weredi wa nini kingefanyika au kifanyike bali wale wenye njaa wasiojua hata computer ni nini wasio na tumaini la mlo mmoja kwa siku. Hawa hudharauliwa sana but ndo wenye nguvu ya kuleta mageuzi popote duniani, wakaa kwenye keyboard walimdanganya Gadaff, Mubarak na wengine wanamdanganya M7, na hata JK sasa hivi but walalahoi wataleta mabadiliko tu
 
We Everybody nashukuru everybody can understand why u are verybody and everybody can think different! Walalahoi kama ulivyowaita ni kweli ndo wenye kuleta mabadiliko kama ilivyotokea Kenya na nchi zingine kama Libya, but try to think critically hawa watu ni very easy kuwashawishi kuingia barabarani kwa kutumia njaa zao, kumbuka hata cdm wataingia madarakani hakuna chochote watakachofanya miracle hawa walala hoi wakaachana na ulalahoi wao! Na kama ccm watakuwa bench then na wao wakawatumia haohao walalahoi kuwasingizia cdm maovu na nakujifanya wao walifanya mazuri zaidi for fifty years basi hapa hapatakalika! Solution ni kifanya mabadiliko ya amani na wala si kuhamasisha fujo na chuki ambazo hazitafutika katika maisha yetu na vizazi vyetu, Mungu ibariki nchi yetu, nakemea pepo mbaya huyu anaenyea huko Arusha na viongozi wote watumie busara badala ya jazba!
 
Revolution usually starts with the dissatisfaction group whether the poor or the elite on the periphery. If it started by the dissatisfied poor then the elite out of power/on the fringes will join and ultimately forming the next elite group to exploit again the poor masses, if it started by the elite out of power then they have to get the poor masses on their side to really have an effect in toppling the elite in the center of power
 
vijana tujishirikishe na vyama vya kijamii, ushabiki wa kisiasa unaendelea bila ya hizi pressure groups ni kazi bure, real democracy, real development comes from a wider participation of all members of society in governance through electorate-politics and planned and organized politics of the people through pressure groups/civil societies..bila ya hizi tutakalia kupiga makelele tu chademaaaaaaa! ccmmmmmmmm, slaaaaaaa, lowassaaaaa, sijui nani tena mwisho wake tutagawanywa kiukanda, kidini, kikabila kwa sababu wanasiasa wanchotaka ni kushinda chaguzi na hamna kingine

Amkeni vijana!!!
 
Back
Top Bottom