mwitaz
JF-Expert Member
- Feb 19, 2012
- 315
- 93
Taarifa kutoka Jamhuri ya
Demokrasi ya Congo
zinaeleza kuwa mapigano
yanaendelea mashariki
mwa nchi baina ya
wanajeshi wa serikali na wanajeshi walioasi. Msemaji wa waasi, Vianney
Kazarama, aliliambia
shirika la habari la
Ufaransa, kwamba jeshi la
serikali linashambulia
kituo chao kimoja kwa silaha nzito, huko Kivu-
Kaskazini. Mapigano hayo yalianza
kama siku 10 zilizopita. Umoja wa Mataifa unasema
maelfu ya watu
wamekimbia ghasia hizo,
wengi wao wameelekea
Uganda na Rwanda. Waasi hao wanasema wao
wamo kwenye vuguvugu
la March 23, ambalo asili
yake ni kundi la
wapiganaji wa Kitutsi, la
CNDP. Walikubali kujumuika na
jeshi la Congo, lakini sasa
wanadai kuwa wanataka
makubaliano ya amani ya
mwaka wa 2009
yatekelezwe kikamilifu.
Source: Wankuru Stephen Mwita
Demokrasi ya Congo
zinaeleza kuwa mapigano
yanaendelea mashariki
mwa nchi baina ya
wanajeshi wa serikali na wanajeshi walioasi. Msemaji wa waasi, Vianney
Kazarama, aliliambia
shirika la habari la
Ufaransa, kwamba jeshi la
serikali linashambulia
kituo chao kimoja kwa silaha nzito, huko Kivu-
Kaskazini. Mapigano hayo yalianza
kama siku 10 zilizopita. Umoja wa Mataifa unasema
maelfu ya watu
wamekimbia ghasia hizo,
wengi wao wameelekea
Uganda na Rwanda. Waasi hao wanasema wao
wamo kwenye vuguvugu
la March 23, ambalo asili
yake ni kundi la
wapiganaji wa Kitutsi, la
CNDP. Walikubali kujumuika na
jeshi la Congo, lakini sasa
wanadai kuwa wanataka
makubaliano ya amani ya
mwaka wa 2009
yatekelezwe kikamilifu.
Source: Wankuru Stephen Mwita