Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Inasikitisha.. sababu ya umasikini unapoteza roho yako kwa malipo ya elfu 50!!!!
 
Nawapongeza sana wana nzengo kwa kuchukua sheria mkononi ili kupambana na 'wavamizi'
 
huu ndo uwekezaji ...damu ya watanzania wenzetu inatutaka watanzania kufia urithi wetu (Ardhi) dhidi ya waporaji,wahuni,wanaharamu,wanyonyaji (BLACK SETTLERS) chini ya uongozi wa kitharimu na kidikteta wa CCM
 
Hili jambo lilikuwa linasubiri litokee wakati wowote. Wananchi wamechoka kuonewa kunyanyaswa na wenye fedha wachache, unyanyasaji ambao umekuwa ukiendelea kwa muda mrefu sasa. Imefika wakati wananchi wanaamua kutetea haki zao kwa namna yoyote hilo. Hili tukio tulichukulie kama tahadhari na alama ya nyakati zijazo. Hatua za kurekebisha hali inatakiwa kuchukuliwa mapema ili 'amani' iendelee kudumishwa.
 
Serikali ya Kikwete. Nyumba 26 za waathirika wa mabomu zinajengwa kwa gharama ya sh.96, 000, 000 zote pamoja.


Mkuu binafsi sijakuelewa, hiyo miloni 96 kwa nyumba 26 umeiona ni kubwa au ni ndogo? naomba uniweke wazi ili tuelimishane kitu
 
Huo ni mwanzo tuu wa kudai haki, watu hawana imani kabisa na dola. Waache waendeleee kupokonya mashamba ya raia huko vijijini kwa visingizio vya uwekezaji then waone moto wake. Watu wamechoka.
 
Mauwaji ya watu watano waliofanywa Tegeta yanaletea kujiulizama ni wapi Watanzania tunakoelekea? Ni watu kuchoka na vyombo vya dola ikiwamo polisi na mahakama? Polisi walpotakiwa kuingilia katim walisema wache wauwane na atakaebakia atakuja kuripoti. Mahakama nayo ilitowa hukumu ya kumpendelea mtu mmoja dhidi ya mamia ya wananchi. Wananchi nao wanapoamuwa kuuwa eti kulinda haki yao? Naomba msaada jamani.
 
Nimekuwa nikipinga huu msemo kuwa Tanzania kuna amani. Nimerudia tena na tena kuwa amani sio kutokuwa na vita, bali ili pawe na amani utawala wa haki kwa kila binadamu utumike. Amani iko wapi kama mahakama, polisi, na huduma zingine hazifanyi kazi vizuri? Watu wanakufa kila siku kwa majanga mbalimbali, kukitokea watu ambao wanataka kuleta mabadiliko mazuri wanaambiwa wanavunja 'amani'.
 
Mkuu binafsi sijakuelewa, hiyo miloni 96 kwa nyumba 26 umeiona ni kubwa au ni ndogo? naomba uniweke wazi ili tuelimishane kitu

hili halina kuuliza, ni ndogo kupita maelezo. Wewe unaweza jenga nyumba kwa gharama ya 3,600,000/= ?
 
Hii story imebaki inaning'inia. Aliyeileta hayuko kuielezea wala kutoa ufafanuzi. Tutakupaje msaada kama haupo kuupokea?
 
Story kamili ni kwamba watu 5 wamekufa ktk mapigano ya kugombea ardhi kati ya wananchi na mabaunsa wa kampuni ya udalali ya Mwangata huko Mivumoni, Tegeta.

Habari ni according to Radio One Srerio katika huduma yao ya SMS.


My Take: Pengine ni size yao -- yaani hao mabaunsa. Hawa na ile breed iliyozuka ya madalali huwa wanaonea sana wanavijiji wasiyojua haki zao katika kupora ardhi zao kwa njia za utapeli mkubwa huku serikali ikiwa haichukui hatua zozote za kuwalinda wanavijiji.

Lakini hata hivyo vifo hivyo siyo njia sahihi.
 
Nimekuwa nikipinga huu msemo kuwa Tanzania kuna amani. Nimerudia tena na tena kuwa amani sio kutokuwa na vita, bali ili pawe na amani utawala wa haki kwa kila binadamu utumike. Amani iko wapi kama mahakama, polisi, na huduma zingine hazifanyi kazi vizuri? Watu wanakufa kila siku kwa majanga mbalimbali, kukitokea watu ambao wanataka kuleta mabadiliko mazuri wanaambiwa wanavunja 'amani'.
Tanzania hakuna amani, wanaodai kuna amani ni waongo wakubwa, hakuna amani bila haki, na tz hakuna haki, ni swala la muda tuu machafuko yatarindima kila kona. Watawala wetu wakiendelea na ubabe wao pamoja na kuziba masikio yao kuusu katiba huru mpya hapatatawalika.
Nimezunguka sehemu nyingi TZ, kuusu migogoro ya wawekezaji na wanachi, yaani serekali imeziba masikio inawabeba sana wawekezaji ambao wamebebwa na wanasiasa mafisadi,yaani wananchi wengi wamekata tamaa kabisa na serekali ni swala la muda tuu, siju nani atatuepusha na hili maana watawala hawana vision ni watu walioshiba na mitoothpic mdomoni.
 
Hii yote ni kutokana na wananchi kutopata haki zao na ndio maana wanajichukulia sheria mkononi!
 
duh iyo ni kali,bt yasemekana police waliitwa ,hawakufika ktk mda ule ,na majibu waliokua wanatoa hayaridhishi so w2 wakajichukulia hatua mkonon,
 
Nimeona itv jioni hii katika jiji letu, kwa kweli hali ilikuwa mbaya!
 
Back
Top Bottom