kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
WANAFUNZI watano wa shule ya Sekondari Mbagala ya jijini Dar es Salaam wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kuwafanyia fujo wanafunzi wenzao wa shule ya Sekondari Nzasa kwa sababu za kimapenzi.
Mwishoni mwa juma lililopita wanafunzi hao waliwavamia wanafunzi wenzao wakiwa na silaha za ugomvi yakiwemo mawe, misumari kwa madai na kuchukuliwa mpenzi wao kwa madai kuna mwanafunzi wa kiume wa shule hiyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi wa kike ambae alikuwa na mpenzi wake katika shule hiyo
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Missime, amesema kuwa chanzo cha vurugu hizo zilisababishwa na mwanafunzi mmoja wa shule ya Mbagala alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana mmoja wa shule hiyo na baadae mwanafunzi huyo alibaini kuwa mpenzi wake huyo ana mahusiano na mwanafunzi mwingine anayesoma Nzasa.
Kamanda Misime amesema kuwa, kutokana na ugunduzi huo mwanafunzi huyo aliamua kwenda na kundi lake shuleni hapo kwenda kumfanyia vurugu mwanafunzi huyo.
Waliokamatwa kwa kusababisha vurugu hizo ni Said Muhibu wa kidato cha tatu, Reuben Hosea wa kidato cha tatu, Shana Reagan wa kidato cha nne wa shule ya Mbagala na Twahir Sultan wa shule ya Nzasa
Hivyo kamanda huyo alivifafanulia vyombo vya habari kuwa upelelezi utakapokamilika wanafunzi hao watafikishwa Mahakamani.
Mwishoni mwa juma lililopita wanafunzi hao waliwavamia wanafunzi wenzao wakiwa na silaha za ugomvi yakiwemo mawe, misumari kwa madai na kuchukuliwa mpenzi wao kwa madai kuna mwanafunzi wa kiume wa shule hiyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi wa kike ambae alikuwa na mpenzi wake katika shule hiyo
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Missime, amesema kuwa chanzo cha vurugu hizo zilisababishwa na mwanafunzi mmoja wa shule ya Mbagala alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana mmoja wa shule hiyo na baadae mwanafunzi huyo alibaini kuwa mpenzi wake huyo ana mahusiano na mwanafunzi mwingine anayesoma Nzasa.
Kamanda Misime amesema kuwa, kutokana na ugunduzi huo mwanafunzi huyo aliamua kwenda na kundi lake shuleni hapo kwenda kumfanyia vurugu mwanafunzi huyo.
Waliokamatwa kwa kusababisha vurugu hizo ni Said Muhibu wa kidato cha tatu, Reuben Hosea wa kidato cha tatu, Shana Reagan wa kidato cha nne wa shule ya Mbagala na Twahir Sultan wa shule ya Nzasa
Hivyo kamanda huyo alivifafanulia vyombo vya habari kuwa upelelezi utakapokamilika wanafunzi hao watafikishwa Mahakamani.